Previous Prev Day Next DayNext

Beginning

Read the Bible from start to finish, from Genesis to Revelation.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Ufunua wa Yohana 20-22

Utawala Wa Miaka Elfu Moja

20 Kisha nikaona malaika akija kutoka mbinguni akiwa ameshika ufunguo wa lile shimo la kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi. Akalishika lile joka, yule nyoka wa kale ambaye ni Ibilisi au Shetani, akamfunga kwa muda wa miaka elfu moja. Akamtupa kuzi muni; akamfungia huko na kumzibia kabisa, asipate nafasi ya kudanganya mataifa tena mpaka hiyo miaka elfu moja iishe. Baada ya hapo ataachiliwa kwa muda mfupi.

Kisha nikaona viti vya enzi. Na kwenye viti hivyo vya enzi waliketi wale waliopewa mamlaka ya kuhukumu. Pia nikaona roho za wale watu waliokatwa vichwa kwa ajili ya kumshuhudia Yesu na kwa ajili ya neno la Mungu. Wao hawakuwa wamemwabudu yule mnyama wala sanamu yake na hawakuwa wamepokea alama ya yule mnyama kwenye vipaji vya nyuso zao wala mikononi mwao. Walifufuka kutoka kwa wafu wakatawala pamoja na Kristo kwa muda wa miaka elfu moja. Wafu waliosalia hawakufufuka mpaka miaka hiyo elfu moja ilipok wisha. Huu ndio ufufuo wa kwanza. Wamebarikiwa na ni watakatifu wale watakaoshiriki huo ufufuo wa kwanza. Mauti ya pili haina nguvu kwa hawa bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala naye kwa muda wa miaka elfu moja.

Kushindwa Kwa Shetani

Miaka hiyo elfu moja itakapokwisha, shetani atafunguliwa kutoka kifungoni mwake, naye atakuja kuyadanganya mataifa yali yopo katika pembe nne za dunia, yaani, Gog na Magog na kuwakusa nya tayari kwa vita. Idadi yao ni kama mchanga wa bahari. Nao walitembea juu ya eneo lote la dunia, wakaizunguka kambi ya wata katifu na ule mji mwema, lakini moto ulishuka kutoka mbinguni, ukawateketeza. 10 Na yule Ibilisi aliyewadanganya alitupwa katika ziwa la moto na kiberiti walipokuwa yule mnyama na yule nabii wa uwongo. Nao watateseka huko usiku na mchana, milele na milele.

11 Kisha nikaona kiti kikubwa cha enzi cheupe, pamoja na huyo aliyeketi juu yake. Dunia na anga zilikimbia kutoka machoni pake zikatoweka wala hazikuonekana tena. 12 Nikaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya kiti cha enzi, na vitabu vikafunguliwa. Pia kitabu kingine ambacho ni kitabu cha uzima kikafunguliwa. Na hao wafu wakahukumiwa kutokana na yale yaliy oandikwa ndani ya vitabu hivyo, kuhusu matendo yao. 13 Bahari zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake, na kifo na kuzimu nazo zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake, na wote wakahukumiwa kwa matendo yao. 14 Kisha mauti na kuzimu zikatupwa katika ziwa la moto. Hiki ndicho kifo cha pili, yaani ziwa la moto. 15 Na kama jina la mtu halikukutwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.

Yerusalemu Mpya

21 Kisha nikaona mbingu mpya na dunia mpya; maana mbingu ya kwanza na dunia ya kwanza zilikwisha kutoweka na bahari haikuwapo tena. Ndipo nikaona mji mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, ukiwa umeandaliwa kama bibi harusi aliyepambwa kwa bwana wake. Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, “Tazama, maskani ya Mungu yako pamoja na wanadamu, naye ataishi pamoja nao. Watakuwa watu wake, na Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, naye atakuwa Mungu wao. Atafuta machozi yao yote, na kifo hakitakuwepo tena, wala maom bolezo, wala kilio, wala maumivu; maana mambo hayo yote ya awali yamekwisha toweka.”

Na yule aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi akasema, “Tazama, nafanya kila kitu kuwa kipya.” Pia akasema, “Andika haya, maana maneno haya ni ya kuaminika, tena ni ya kweli.” Akaniambia, “Yamekamilika! Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Walio na kiu nitawapa maji kutoka katika chemchemi ya maji ya uzima bila malipo. Atakayeshinda atarithi baraka zote hizi, na mimi nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu. Lakini waoga, na wasioamini na wachafu, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na wanaoabudu sanamu, pamoja na waongo wote, urithi wao upo katika lile ziwa linalowaka moto na kiberiti. Hii ndio mauti ya pili.”

Kisha mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na mabakuli saba ya yale maafa saba ya mwisho akaja akaniambia, “Njoo, nitakuon yesha bibi harusi, mke wa Mwana-Kondoo.”

10 Basi, nikiwa katika Roho, akanipeleka mbali kwenye mlima mkubwa na mrefu, akanionyesha ule mji mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu. 11 Ulikuwa na utukufu wa Mungu, uking’aa kama kito cha thamani sana, kama yaspa, na safi kama kioo. 12 Ulikuwa na ukuta mkubwa mrefu wenye milango kumi na mbili na malaika kumi na wawili milangoni. Kwenye milango hiyo yaliandikwa majina ya yale makabila kumi na mawili ya Israeli . 13 Ilikuwapo milango mitatu mashariki, mitatu kaskazini, mitatu kusini na mitatu magharibi. 14 Ukuta wa mji huo ulikuwa na mis ingi kumi na mbili na juu yake yaliandikwa majina ya wale mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo.

15 Huyo malaika aliyesema nami alikuwa na kipimo cha dhahabu cha kupimia huo mji na milango yake na kuta zake.

16 Mji huo ulikuwa wa mraba, marefu yake yakilingana na mapana yake. Akaupima mji huo kwa hicho kipimo chake; ulikuwa kama kilometa elfu mbili na mia nne kwa upana wake, na urefu wake pamoja na kina chake vilikuwa sawa. 17 Kisha akapima na ukuta wake, urefu wake ulikuwa zaidi ya meta sitini kwa kipimo cha binadamu alichokuwa akitumia huyo malaika. 18 Ukuta huo uli jengwa kwa yaspa na mji wenyewe ulijengwa kwa dhahabu safi iking’aa kama kioo. 19 Misingi ya mji huo ilipambwa kwa kila aina ya kito cha thamani. Msingi wa kwanza ulikuwa wa yaspa; wa pili yakuti samawi; wa tatu kalkedoni; wa nne zumaridi; 20 wa tano sardoniki; wa sita akiki; wa saba krisolitho; wa nane zabar ajadi; wa tisa yakuti ya njano; wa kumi krisopraso; wa kumi na moja hiakintho; wa kumi na mbili amethisto. 21 Na ile milango kumi na mbili ilikuwa ni lulu kumi na mbili, kila mlango uli tengenezwa kwa lulu moja! Barabara za mji huo zilikuwa za dhahabu safi ing’aayo kama kioo.

22 Sikuona Hekalu yo yote ndani ya mji huo kwa sababu Bwana Mungu Mwenyezi na Mwana-Kondoo ndio Hekalu la mji. 23 Mji huo hauhitaji jua wala mwezi kuangaza juu yake kwa sababu utukufu wa Mungu ndio nuru yake na Mwana-Kondoo ndiye taa yake. 24 Mataifa yote yatatembea yakiangaziwa kwa nuru yake na wafalme wa duniani wataleta utukufu wao ndani yake. 25 Milango yake itakuwa wazi mchana daima, maana hakutakuwa na usiku huko. 26 Utukufu na heshima za mataifa zitaletwa humo. 27 Lakini hakuna kitu kichafu kitakachoingia humo wala mtu ye yote atendaye mambo ya aibu au ya udanganyifu. Bali wataingia humo wale tu ambao majina yao yamean dikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.

Mto Wa Maji Ya Uzima

22 Kisha yule malaika akanionyesha mto wa maji ya uzima ung’aao kama kioo na kutiririka kutoka kwenye kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo, kupitia katikati ya barabara kuu ya mji huo. Katika pande zote za mto huo kulikuwa na mti wa uzima utoao matunda ya aina kumi na mbili, na kuzaa matunda yake kila mwezi. Majani yake ni ya kuwaponya watu wa mataifa. Katika mji huo hakutakuwa na kitu cho chote kilicholaaniwa, bali kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwamo humo na watumishi wake watamwabudu. Watamwona uso wake na jina lake litakuwa kwe nye vipaji vya nyuso zao. Usiku hautakuwapo tena; wala hawata hitaji mwanga wa taa au wa jua, maana Bwana Mungu atakuwa nuru yao, watatawala milele na milele.

Bwana Yesu Anakuja

Kisha yule malaika akaniambia, “Maneno haya ni ya kuami nika na ya kweli. Bwana, Mungu wa roho za manabii, amemtuma mal aika wake kuwaonyesha watumishi wake yale ambayo hayana budi kutokea karibuni. Tazama, ninakuja upesi! Amebarikiwa anayesh ika maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki.”

Mimi Yohana, ndiye niliyesikia na kuona mambo haya. Na nil ipokwisha kuyasikia na kuyaona, nilianguka kifudifudi penye miguu ya yule malaika aliyenionyesha mambo hayo, nimwabudu. Lakini yeye akaniambia, “Usifanye hivyo! Mimi pia ni mtumishi pamoja na wewe na ndugu zako manabii na wote wanaoshika maneno ya kitabu hiki. Mwabudu Mungu!”

10 Kisha akaniambia, “Usiyawekee muhuri maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki maana wakati umekaribia. 11 Mwache atendaye uovu aendelee kutenda uovu, na aliye mchafu aendelee kuwa mchafu; na atendaye mema aendelee kutenda mema na aliye mta katifu aendelee kuwa mtakatifu.”

12 “Tazama, Ninakuja upesi! Nakuja na tuzo yangu, nimpe tuzo kila mtu kulingana na matendo yake. 13 Mimi ni Alfa na Omega, wa kwanza na wa wisho, Mwanzo na Mwisho.” 14 Wamebari kiwa wanaoosha mavazi yao ili wapate haki ya kushiriki mti wa uzima na wapate kuingia katika ule mji kupitia kwenye milango yake. 15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye udanganyifu na kuutenda. 16 Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia mambo haya kwa ajili ya makanisa. Mimi ni Shina na Mzao wa ukoo wa Daudi. Mimi ni Nyota ya asubuhi ing’aayo.”

17 Roho na bibi harusi wanasema, “Njoo!” Na kila mtu asi kiaye na aseme, “Njoo!” Na mtu ye yote mwenye kiu na aje, na kila anayetaka na apokee zawadi ya maji ya uzima bure. .

18 Namwonya kila mtu asikiaye maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki: mtu ye yote akiyaongezea cho chote, Mungu atamwongezea maafa yaliyoandikwa katika kitabu hiki. 19 Na kama mtu ye yote akipunguza cho chote katika maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, Mungu atamnyang’anya sehemu yake katika mti wa uzima na katika mji mtakatifu, ambayo yameelezwa katika kitabu hiki.

20 Yeye anayeshuhudia mambo haya anasema, “Hakika ninakuja upesi!” Amina. Njoo, Bwana Yesu!

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica