Previous Prev Day Next DayNext

Beginning

Read the Bible from start to finish, from Genesis to Revelation.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Waebrania 1-6

Ukuu Wa Mwana Wa Mungu

Hapo zamani Mungu alisema na baba zetu mara nyingi na kwa namna mbali mbali kwa kuwatumia manabii. Lakini katika siku hizi za mwisho, amesema na sisi kwa njia ya Mwanae, ambaye alim chagua kuwa mrithi wa vitu vyote. Na kwa njia ya Mwanae, Mungu aliumba ulimwengu. Yeye Mwana ni mng’ao wa utukufu wa Mungu na chapa halisi ya nafsi yake, naye huudumisha na kuuendeleza ulim wengu kwa neno lake lenye nguvu. Alipokwisha kuwapatia wanadamu utakaso wa dhambi, alikaa upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi aliye juu. Kwa hiyo Mwana alikuwa mkuu zaidi kuliko malaika, kama ambavyo jina alilorithi kwa Mungu ni kuu kuliko jina la malaika ye yote.

Kwa maana ni malaika gani ambaye Mungu aliwahi kumwambia: “Wewe ni mwanangu; leo hii nimekuzaa”? Au tena: “Mimi nita kuwa Baba yake na yeye atakuwa Mwanangu”? Na tena Mungu ana pomleta mwanae, mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, anasema: “Malaika wote wa Mungu wamwabudu yeye.” Anapozungumza juu ya malaika anasema: “Anawafanya malaika wake kuwa upepo, watumishi wake kuwa ndimi za moto.” Lakini kuhusu Mwana, anasema: “Kiti chako cha enzi, Wewe Mungu, kitadumu milele na milele, na haki takuwa fimbo ya ufalme wako. Umependa haki na kuchukia uovu. Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuchagua wewe na kukuweka juu ya wenzako kwa kukupaka mafuta ya furaha.” 10 Pia anasema: “Hapo mwanzo , Wewe Bwana, uliweka misingi ya ulimwengu, na mbingu ni kazi ya mikono yako. 11 Vyote vitaangamia lakini wewe unadumu; vyote vitachakaa kama nguo, nawe 12 utavikunja kama vazi na kuvibadilisha. Bali wewe hubadiliki, na miaka yako haitakwisha kamwe. ” 13 Lakini ni malaika gani amewahi kumwambia, “Keti kulia kwangu mpaka niwafanye adui zako kuwa kiti cha kuwekea miguu yako”? 14 Malaika ni nani basi? Wao ni roho wa utumishi waliotumwa kuwahudumia wale watakaopokea wokovu.

Kuzingatia Mafundisho

Kwa hiyo, hatuna budi kuzingatia kwa makini mambo tuliyof undishwa tusije tukatanga-tanga mbali na yale tuliyosikia. Kwa maana kama ujumbe ulioletwa na malaika ulithibitika kuwa kweli, na kila aliyeasi na kutokutii akaadhibiwa ilivyostahili, sisi je? Tutaepukaje kama tusipojali wokovu mkuu namna hii? Wokovu huu kwanza ulitangazwa na Bwana, na ulithibitishwa kwetu na wale wal iomsikia. Mungu pia aliushuhudia kwa ishara na miujiza na maaj abu mbalimbali, pamoja na karama za Roho Mtakatifu alizogawa kufuatana na mapenzi yake.

Wokovu Umeletwa Na Kristo

Maana Mungu hakuuweka ulimwengu ujao, tunaouzungumzia, chini ya mamlaka ya malaika. Bali kama inavyothibitishwa katika sehemu fulani ya Maandiko, “Mwanadamu ni kitu gani hata umfi kirie, au mwana wa binadamu ni nani hata umjali? Umemfanya kuwa chini kidogo ya malaika; wewe umemvika taji ya utukufu na heshima, umemfanya kuwa mtawala wa vitu vyote.” Mungu ali poweka vitu vyote chini ya mamlaka ya mwanadamu, hakubakiza cho chote ambacho mwanadamu hakitawali. Lakini kwa wakati huu hatuoni kama kila kitu kiko chini ya mamlaka yake. Lakini tunamwona Yesu, ambaye kwa muda mfupi alifanywa kuwa chini kidogo ya mal aika, sasa akiwa amevikwa taji ya utukufu na heshima kwa sababu aliteseka na kufa, ili kwa neema ya Mungu, aonje mauti kwa ajili ya watu wote.

10 Kwa maana ilikuwa ni sawa kabisa kwamba Mungu, ambaye kwa ajili yake na kwa uweza wake vitu vyote vimekuwepo, amfanye Mwan zilishi wa wokovu wao kuwa mkamilifu kwa njia ya mateso, ili awalete wana wengi washiriki utukufu wake. 11 Maana yule anayetakasa na wale wanaotakaswa, wote wanatoka katika uzao mmoja. 12 Ndio maana Yesu haoni aibu kuwaita wao ndugu zake, akisema: “Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katikati yao nitakusifu.” 13 Na tena anasema, “Nitamwekea Mungu tumaini langu.” Na tena, “Niko hapa, mimi pamoja na watoto niliopewa na Mungu.”

Mungu.”

14 Basi, kwa kuwa watoto hao wana mwili na damu, yeye pia alishiriki katika ubinadamu wao, ili kwa kufa kwake apate kumwan gamiza yule mwenye mamlaka juu ya kifo, yaani shetani; 15 na hivyo awaweke huru wale ambao walikuwa utumwani maisha yao yote kwa sababu ya kuogopa kifo. 16 Maana ni wazi kwamba hakuja kuwa saidia malaika bali kuwasaidia uzao wa Ibrahimu. 17 Kwa sababu hii ilibidi awe kama ndugu zake kwa kila hali, apate kuwa kuhani mkuu mwenye huruma na mwaminifu katika huduma ya Mungu, ili aweze kujitoa kama sadaka kwa ajili ya dhambi za watu. 18 Na kwa kuwa yeye mwenyewe ameteswa na kujaribiwa, anaweza kuwasaidia wanaoj aribiwa.

Yesu Ni Mkuu Kuliko Musa

Kwa hiyo, ndugu zangu watakatifu, ambao mmeshiriki wito wa mbinguni, mtafakarini Yesu, mtume na kuhani mkuu wa imani tunay oikiri.

Kwa maana Yesu alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemchagua, kama vile Musa alivyokuwa mwaminifu katika nyumba ya Mungu. Lakini Yesu amehesabiwa kuwa anastahili utukufu zaidi kuliko Musa, kama vile mjenzi wa nyumba anavyopewa heshima zaidi kuliko nyumba aliyoijenga. Maana kila nyumba hujengwa na mtu fulani bali aliyejenga vitu vyote ni Mungu. Ni kweli kwamba Musa ali kuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu kama mtumishi, akishu hudia juu ya yale mambo ambayo Mungu angeyatamka baadaye, lakini Kristo alikuwa mwaminifu katika nyumba ya Mungu kama mwana. Na sisi ni nyumba yake, ikiwa tutashikilia ujasiri wetu na lile tumaini tunalojivunia.

Jihadharini Na Kutokuamini

Kwa hiyo, kama Roho Mtakatifu asemavyo, “Leo, mkiisikia sauti yake, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama mlivyofanya wakati wa uasi , siku ile ya majaribio jangwani, ambapo baba zenu walinijaribu wakaona kazi zangu kwa miaka arobaini. 10 Kwa hiyo kizazi kile kilinikasirisha, nikasema, ‘Mioyo ya watu hao imepotoka; hawajapata kujua njia zangu.’ 11 Katika hasira yangu nikaapa, ‘Hawataingia kwenye pumziko langu kamwe.’

12 Angalieni, ndugu zangu, asiwepo miongoni mwenu mtu ye yote mwenye moyo wa dhambi, usioamini, unaomfanya ajitenge na Mungu wa uzima. 13 Bali muonyane kila siku maadamu bado ni ‘ ‘leo” ili asiwepo mtu kati yenu anayefanywa mkaidi na udangany ifu wa dhambi. 14 Kwa maana sisi ni washiriki pamoja na Kristo iwapo tutashikilia tumaini letu la kwanza kwa uaminifu mpaka mwisho. 15 Kama Maandiko yalivyosema: “Leo mkiisikia sauti yake, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu. Kama mlivyofanya wakati wa uasi.” 16 Ni nani hao waliosikia lakini wakaasi? Si wale wote waliotoka Misri wakiongozwa na Musa? 17 Na ni nani waliom kasirisha Mungu kwa miaka arobaini? Si wale waliofanya dhambi wakafa jangwani? 18 Na ni nani ambao Mungu aliapa kuwa hawatain gia kwenye pumziko lake, isipokuwa wale waliokataa kutii? 19 Kwa hiyo tunaona kwamba walishindwa kuingia kwa sababu ya kutokuamini kwao. Pumziko La Sabato

Basi, maadamu ahadi ya Mungu ya kuingia katika pumziko lake bado ipo, tujihadhari asije mmoja wenu akakutwa ameshindwa kuin gia huko. Maana sisi tumehubiriwa Habari Njema kama vile wao walivyohubiriwa. Lakini ujumbe waliosikia haukuwasaidia kwa sababu hawakuupokea kwa imani. Kwa kuwa sisi tulioamini tunain gia katika pumziko hilo, kama Mungu alivyosema, “Na katika hasira yangu nikaapa, ‘Hawataingia kwenye pumziko langu kamwe.’ Mungu alisema hivyo ingawa kazi yake ilikamilika tangu ulimwengu ulipoumbwa. Maana mahali fulani akizungumza kuhusu siku ya saba, alisema: “Mungu alipumzika siku ya saba baada ya kazi zake zote.” Na tena mahali hapo alisema: “Hawataingia kwenye pum ziko langu kamwe.” Basi kwa kuwa wapo watakaoingia kwenye pum ziko hilo, na wale ambao walihubiriwa Habari Njema hapo mwanzo lakini wakashindwa kuingia kwa sababu ya kutokutii kwao, kwa hiyo Mungu aliweka tena siku nyingine akaiita “Leo”; akasema kwa maneno ya Daudi miaka mingi baadaye, kama yalivyokwisha kukaririwa: “Leo mkiisikia sauti yake, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu.”

Maana, kama Yoshua angalikuwa amekwisha kuwapatia pumziko, Mungu asingalizungumzia baadaye kuhusu siku nyingine. Kwa hiyo basi ipo bado sabato ya mapumziko waliyowekewa watu wa Mungu; 10 kwa maana, mtu anayeingia katika pumziko la Mungu, pia hupum zika kutoka katika kazi zake kama vile Mungu alivyopumzika baada ya kazi zake.

11 Basi tujitahidi kuingia kwenye pumziko hilo asije mtu akaanguka kwa kutokuamini kama hao. 12 Kwa maana neno la Mungu ni hai tena lina nguvu; ni kali kuliko upanga wenye makali kuwili, linachoma kabisa na kutenganisha nafsi na roho, viungo vya mwili na mafuta yaliyomo ndani yake; na kutambua nia na mawazo ya mioyo ya watu. 13 Hakuna kiumbe cho chote kilichofi chika machoni pa Mungu. Kila kitu kimefunuliwa na kuwekwa wazi machoni pake yeye ambaye hatuna budi kueleza habari zetu zote kwake.

Kuhani Mkuu Yesu Kristo

14 Hivyo basi, kwa kuwa tunaye kuhani mkuu aliyepitia mbingu, Yesu Mwana wa Mungu, tushikilie kwa uthabiti imani yetu tunayoikiri. 15 Kwa maana huyu kuhani wetu mkuu si kuhani ambaye hawezi kutuhurumia katika udhaifu wetu, bali ni kuhani ambaye kwa kila hali amejaribiwa kama sisi, lakini pasipo kutenda dhambi. 16 Kwa hiyo basi, tusogelee kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupokee rehema na kupata neema ya kutusaidia wakati wa shida.

Sifa Za Kuhani Mkuu

Kwa maana kila kuhani mkuu anayechaguliwa miongoni mwa watu huteuliwa kumtumikia Mungu kwa niaba yao, kutoa sadaka na dhabihu kwa ajili ya dhambi zao. Anaweza kuwaonea huruma wale wasioel ewa na wanaopotoka kwa sababu yeye mwenyewe anasumbuliwa na udhaifu kama wao . Kwa sababu hii, anawajibika kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe na kwa ajili ya dhambi za hao watu.

Hakuna mtu anayejichagulia heshima hii ya kuwa kuhani mkuu. Kila mmoja huitwa na Mungu kama vile Haruni alivyoitwa.

Kristo hakujichagulia mwenyewe utukufu wa kuwa kuhani mkuu. Bali aliteuliwa na Mungu ambaye alimwambia, “Wewe ni mwanangu, leo hii nimekuzaa;” na tena kama asemavyo mahali pengine, “Wewe ni kuhani milele, katika ngazi ile ya ukuhani ya Mel kizedeki. Yesu alipokuwa akiishi duniani, alitoa dua na maombi kwa kilio kikuu na machozi kwa Mungu ambaye angeweza kumwokoa na kumtoa katika kifo, naye Mungu alimsikia kwa sababu alikuwa mnyenyekevu na mtiifu. Ingawa alikuwa Mwana wa Mungu, aliji funza utii kutokana na mateso aliyopata; na baada ya kufanywa mkamilifu, akawa chanzo cha wokovu wa milele kwa wote wanaomtii, 10 akateuliwa na Mungu kuwa kuhani mkuu wa ngazi ile ile ya

Onyo Kuhusu Kuanguka

11 Kuhusu ukuhani huu, tunayo mengi ya kusema ambayo ni mag umu kuyaeleza, kwa maana ninyi si wepesi wa kuelewa. 12 Ingawa kwa wakati huu mngalipaswa kuwa walimu, lakini bado mnahitaji mtu wa kuwafundisha tena hatua za kwanza za neno la Mungu. Mnahitaji maziwa, wala si chakula kigumu. 13 Kwa maana anayeishi kwa maziwa peke yake bado ni mtoto mchanga, hana ujuzi katika mafund isho kuhusu neno la haki. 14 Bali chakula kigumu ni kwa ajili ya watu wazima, watu ambao wamekomaa akili kutokana na mafunzo ya mazoezi ya kupambanua kati ya mema na mabaya.

Basi sasa tutoke katika yale mafundisho ya msingi kuhusu Kristo, tupige hatua kufikia ukamilifu katika kuelewa kwetu. Hatupaswi tena kuwaeleza ninyi yale mafundisho ya msingi kuhusu kutubu na kuacha matendo yaletayo kifo, na kuhusu kumwamini Mungu pamoja na maagizo kuhusu ubatizo, kuwekea watu mikono, kufufuka kwa wafu na hukumu ya milele. Mungu akitujalia tutaendelea mbele.

Kwa maana haiwezekani tena kuwarejesha katika toba watu ambao waliwahi kuongoka, ambao wameonja uzuri wa mbinguni, wakashiriki Roho Mtakatifu, ambao wameonja wema wa neno la Mungu na nguvu za nyakati zijazo, kama wakikufuru. Kwa sababu wanamsulubisha tena Mwana wa Mungu mioyoni mwao na kumwaibisha hadharani. Ardhi ambayo baada ya kupata mvua ya mara kwa mara, hutoa mazao yanayowanufaisha wale ambao wanailima na kupokea bar aka kutoka kwa Mungu. Lakini kama ardhi hiyo itaotesha magugu na miiba, haina thamani, na inakaribia kulaaniwa. Mwisho wake ni kuchomwa moto.

Wanaopokea Ahadi Za Mungu

Ingawa tunasema hivi, ndugu zangu, kwa upande wenu tuna hakika ya mambo mazuri zaidi, yanayoandamana na wokovu. 10 Mungu si dhalimu hata asahau kazi yenu na upendo mliomwonyesha mlipowa saidia watu wake na mnavyoendelea kuwasaidia. 11 Tunapenda kila mmoja wenu aonyeshe bidii hiyo hiyo mpaka mwisho ili mpate kupo kea tumaini lenu. 12 Hatutaki muwe wavivu bali muige wale ambao kwa imani na subira hupokea yale yaliyoahidiwa na Mungu.

Uhakika Wa Ahadi Ya Mungu

13 Mungu alipompa Ibrahimu ahadi, aliapa kwa jina lake mwe nyewe kwa kuwa hapakuwa na mkuu kuliko yeye ambaye angeweza kuapa kwa jina lake. 14 Alisema, “Hakika nitakubariki na kukupatia watoto wengi.” 15 Na hivyo baada ya kungoja kwa subira, Abra hamu alipata ahadi hiyo.

16 Watu huapa kwa mtu aliye mkuu kuliko wao, na kiapo hicho huthibitisha kinachosemwa na humaliza ubishi wote. 17 Kwa hiyo Mungu alipotaka kuwahakikishia warithi wa ahadi yake kuhusu maku sudi yake yasiyobadilika, aliwathibitishia kwa kiapo. 18 Mungu alifanya hivyo ili, kwa kutumia mambo haya mawili yasiyobadilika, na ambayo Mungu hawezi kusema uongo, sisi tuliokimbilia usalama kwake tutiwe moyo, tushikilie kwa uthabiti tumaini lililowekwa mbele yetu.

19 Tunalo tumaini hili kama nanga ya roho zetu yenye nguvu na imara. Tumaini hili linaingia hadi ndani ya pazia 20 ambamo Yesu ameingia akitutangulia; ameingia huko kwa niaba yetu. Yeye amekuwa kuhani mkuu milele, kama Melkizedeki.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica