Previous Prev Day Next DayNext

Beginning

Read the Bible from start to finish, from Genesis to Revelation.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Ufunua wa Yohana 9-12

Tarumbeta Ya Tano

Kisha malaika wa tano akapiga tarumbeta yake, nikaona nyota iliyokuwa imeanguka kutoka angani hadi ardhini. Nyota hiyo ili pewa ufunguo wa shimo la kuzimu. Alipolifungua hilo shimo, moshi ulitoka ndani yake kama moshi wa tanuru kubwa sana. Jua na anga vilitiwa giza kwa ajili ya ule moshi uliotoka katika shimo hilo. Kisha, katika ule moshi wakatoka nzige wakatua ardhini. Nao wakapewa nguvu kama nguvu ya nge wa duniani. Waliambiwa wasidhuru nyasi za nchi, wala majani, wala mmea au mti wo wote. Bali wawadhuru wale watu wasiokuwa na muhuri wa Mungu kwenye vipaji vya nyuso zao. Waliruhusiwa kuwatesa kwa muda wa miezi mitano lakini wasiwaue. Na uchungu wa kuuma kwao ulikuwa kama uchungu wa mtu anapoumwa na nge. Katika siku hizo watu watata futa kifo lakini hawatakiona; watatamani kufa, lakini kifo kita wakimbia.

Wale nzige walionekana kama farasi waliotayarishwa kwa vita; vichwani mwao kulikuwa na kitu kama taji za dhahabu; na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu. Manyoya yao yalifanana kama nywele za wanawake; na meno yao yalikuwa kama meno ya simba. Walikuwa na magamba yaliyofanana na ngao za chuma; na kelele za mabawa yao zilikuwa kama kelele za magari ya farasi yenye farasi wanaokimbia kwenda vitani. 10 Walikuwa na mikia ya kuuma kama nge; nguvu yao ya kutesa watu kwa muda wa miezi mitano ilikuwa katika mikia yao. 11 Walikuwa na mfalme wa kuwatawala, naye ni malaika wa shimo la kuzimu ambaye jina lake kwa Kiebrania ni Aba doni na kwa Kigiriki ni Apolioni.

12 Maafa ya kwanza yamepita; bado mengine mawili yanakuja.

Tarumbeta Ya Sita

13 Malaika wa sita akapiga tarumbeta yake, nami nikasikia sauti ikitoka katika zile pembe nne za madhabahu iliyoko mbele ya Mungu. 14 Sauti hiyo ikamwambia yule malaika wa sita mwenye tar umbeta, “Wafungulie wale malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa wa Efrati.” 15 Basi wakafunguliwa wale malaika wanne waliokuwa wamewekwa tayari kwa ajili ya saa hiyo, na siku hiyo na mwezi huo na mwaka huo, wawaue theluthi moja ya wanadamu. 16 Idadi ya majeshi wapandao farasi ilikuwa milioni mia mbili. 17 Na hivi ndivyo nilivyowaona hao farasi na wapanda farasi katika maono yangu: wapanda farasi walivaa ngao vifuani zenye rangi ya moto na samawati na kiberiti. Na vichwa vya farasi hao vilikuwa kama vichwa vya simba; na moto, moshi na kiberiti vili kuwa vinatoka vinywani mwao. 18 Theluthi moja ya wanadamu waliu awa kwa maafa hayo matatu, yaani, moto, moshi na kiberiti, yaliy otoka vinywani mwa hao farasi. 19 Nguvu ya hao farasi ilikuwa vinywani mwao na mikiani mwao; kwa sababu mikia yao ilikuwa kama nyoka wenye vichwa ambavyo vilitumika kuwadhuru watu.

20 Wanadamu waliosalia, ambao hawakuuawa katika maafa hayo, bado walikataa kutubu na kuacha kuabudu vitu walivyotengeneza kwa mikono yao wenyewe. Waliendelea kuabudu pepo, sanamu za dhahabu na za fedha na za shaba na za mawe na za miti, sanamu zisizoweza kuona, kusikia wala kutembea. 21 Wala hawakutubu na kuacha matendo yao ya uuaji, uchawi, uasherati na wizi.

Malaika Mwenye Hati Ndogo

10 Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa amevaa wingu, na upinde wa mvua kich wani. Uso wake uling’aa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto. Mkononi mwake alikuwa ameshika hati ndogo iliyokuwa imefunguliwa. Mguu wake wa kulia aliuweka juu ya bahari na mguu wake wa kushoto aliuweka juu ya nchi kavu. Naye akaita kwa sauti kuu kama simba anayenguruma. Alipopaza sauti, ngurumo saba ziliitikia kwa kishindo. Na zile ngurumo saba zilipokwisha kuitikia, nilitaka kuanza kuandika, lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Funga hayo yaliyosemwa na ngurumo hizo saba, ni siri; usiyaandike.”

Kisha yule malaika aliyekuwa amesimama juu ya bahari na nchi kavu akainua mkono wake wa kulia juu mbinguni, akaapa kwa jina la Mungu aishiye milele na milele, aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote vilivyomo, na bahari na vyote vilivy omo, akasema, “Wakati wa kungoja umekwisha. Lakini katika siku ambazo yule malaika wa saba atakaribia kupiga tarumbeta yake, siri ya Mungu itatimizwa kama alivyowatangazia watumishi wake manabii.”

Ndipo ile sauti niliyokuwa nimeisikia pale mwanzoni ikasema nami tena, “Nenda, kachukue ile hati iliyoko mkononi mwa yule malaika aliyesimama juu ya bahari na nchi kavu.”

Basi nikaenda, nikamwomba yule malaika anipe ile hati ndogo. Akaniambia, “Ichukue uile. Itakuwa chungu tumboni mwako, lakini mdomoni mwako itakuwa tamu kama asali.” 10 Basi nikaichukua ile hati ndogo kutoka mkononi mwa yule malaika nikaila. Ilikuwa tamu kama asali mdomoni mwangu lakini nili poimeza, ikawa chungu tumboni mwangu. 11 Kisha nikaambiwa, “Inakubidi kutoa unabii tena kuhusu watu wengi, na mataifa, lugha na wafalme.”

Mashahidi Wawili

11 Ndipo nikapewa kipimo kama fimbo, nikaambiwa, “Nenda kapime Hekalu la Mungu pamoja na madhabahu na uwahesabu watu waabuduo humo. Lakini usipime uwanja wa nje ya Hekalu, uache, kwa sababu uwanja huo wamepewa mataifa wasiomjua Mungu. Wao wataukanyagakanyaga mji mtakatifu kwa muda wa miezi arobaini na miwili. Nami nitawapa uwezo mashahidi wangu wawili watoe unabii kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na sitini na mbili, wakiwa wamevaa magunia.”

Manabii hao wawili ni ile mizeituni miwili na vile vinara viwili visimamavyo mbele za Bwana na mbele ya nchi yote. Na mtu akitaka kuwadhuru, moto hutoka vinywani mwao na kuwateketeza adui zao. Na hivyo ndivyo atakavyokufa mtu ye yote atakayetaka kuwad huru. Watu hawa wanayo mamlaka ya kuyafunga mawingu ili mvua isinyeshe wakati wote watakapokuwa wanatoa unabii wao. Watakuwa na mamlaka juu ya maji kuyageuza kuwa damu, na kuleta maafa ya kila aina ulimwenguni, kama wapendavyo. Lakini wakishamaliza kutoa unabii huo, yule mnyama atokaye katika shimo la kuzimu ata wapiga vita na kuwashinda na kuwaua. Maiti zao zitabaki katika barabara ya mji mkuu ambao kwa fumbo unaitwa Sodoma na Misri, ambapo Bwana wao alisulubiwa. Kwa muda wa siku tatu na nusu, watu wa kila kabila, lugha, taifa na rangi wataziangalia maiti zao, na hawataruhusu wazikwe. 10 Watu waishio duniani watafura hia kifo cha manabii hao wawili na kushangilia kwa kupeana zawadi kwa sababu manabii hao waliwatesa watu waishio ulimwenguni.

11 Lakini baada ya zile siku tatu na nusu, pumzi ya uhai kutoka kwa Mungu iliwaingia, nao wakasimama; wote waliowaona wakaingiwa na hofu kuu. 12 Kisha wale manabii wawili wakasikia sauti kuu kutoka mbinguni ikiwaambia, “Njooni huku juu!” Nao wakapaa mbinguni katika wingu, wakati maadui zao wakiwatazama. 13 Wakati huo huo, kukatokea tetemeko kuu la nchi, na sehemu moja ya kumi ya mji ikaanguka. Watu elfu saba wakauawa katika tetemeko hilo na waliosalimika wakaogopa sana, wakamtukuza Mungu wa mbinguni.

14 Maafa ya pili yamekwisha kupita. Lakini maafa ya tatu yanakuja upesi.

Tarumbeta Ya Saba

15 Kisha malaika wa saba akapiga tarumbeta yake. Na sauti kuu zikasikika mbinguni zikisema, “Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana wetu na Kristo wake, naye atatawala milele na milele.” 16 Na wale wazee ishirini na wanne waketio mbele za Mungu katika viti vyao vya enzi wakaanguka kifudifudi wakamwabudu Mungu, 17 wakisema, “Tunakushukuru, Bwana Mungu Mwenyezi uli yeko na uliyekuwako; kwa kuwa umeuchukua uweza wako mkuu na ukaanza kutawala. 18 Watu wa mataifa walikasirika kwa kuwa wakati wa ghadhabu yako umefika. Wakati umefika wa kuwahukumu wafu na kuwapa tuzo watumishi wako manabii na watakatifu walioli tukuza jina lako, wakubwa kwa wadogo; na wakati umefika wa kuwaangamiza wale wanaoiangamiza dunia.”

19 Kisha Hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa na sanduku la agano lake likaonekana Hekaluni mwake. Kukatokea umeme, sauti, ngurumo na tetemeko la nchi na mvua kubwa ya mawe.

Mwanamke Na Joka

12 Ndipo ishara kuu ikaonekana mbinguni: palikuwa na mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na taji ya nyota kumi na mbili ilikuwa juu ya kichwa chake. Alikuwa mjam zito,akilia kwa uchungu kwa kuwa alikuwa anakaribia kujifungua. Kisha ishara nyingine ikaonekana mbinguni: likaonekana joka kubwa jekundu lenye vichwa saba na pembe kumi na taji saba katika vichwa vyake. Mkia wake ulifagia theluthi moja ya nyota zote angani na kuziangusha ardhini. Joka hili likasimama mbele ya yule mwanamke aliyekuwa karibu kujifungua, likiwa tayari kumla huyo mtoto mara tu atakapozaliwa. Mama huyo akajifungua mtoto wa kiume, ambaye atayatawala mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Lakini mtoto huyo akanyakuliwa na kupelekwa kwa Mungu, kwenye kiti chake cha enzi. Yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambako Mungu alik wisha kumtengenezea mahali pa kumtunza kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na sitini.

Vita Mbinguni

Kisha kukazuka vita mbinguni: Mikaeli na malaika wake waki pigana na hilo joka. Joka nalo pamoja na malaika wake likapigana nao. Lakini joka na malaika wake wakashindwa na hapakuwa tena na nafasi kwa ajili yao mbinguni. Basi joka hilo kuu likatupwa nje, yule nyoka wa kale aitwaye Ibilisi na Shetani, adanganyaye watu wote ulimwenguni. Alitupwa chini ardhini, yeye pamoja na malaika wake.

Ushindi Mbinguni Watangazwa

10 Kisha nikasikia sauti kuu mbinguni ikisema, “Sasa umeti mia wokovu na uweza na Ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake yamefika. Kwa kuwa mshtaki wa ndugu zetu anayewashtaki mbele za Mungu usiku na mchana ametupwa chini. 11 Nao wamemshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo na kwa neno la ushuhuda wao, kwa kuwa wao hawakuyapenda maisha yao kiasi cha kuogopa kifo. 12 Kwa hiyo furahini ninyi mbingu, na wote wakaao mbinguni! Bali ole wenu nchi na bahari maana shetani amekuja kwenu akiwa amejaa ghadhabu, kwa maana anajua kuwa muda wake ni mfupi!”

13 Lile joka lilipoona kuwa limetupwa chini duniani, lilim winda yule mwanamke aliyekuwa amejifungua mtoto wa kiume. 14 Lakini huyo mama akapewa mabawa mawili ya yule tai mkubwa kusudi aruke hadi mahali ambapo atatunzwa kwa muda na nyakati na nusu ya wakati. 15 Lile joka likamwaga maji kama mto kutoka kinywani mwake, mafuriko yakamfuata huyo mama ili yamchukue. 16 Lakini ardhi ikamsaidia huyo mama; ikafunua kinywa chake na kuumeza ule mto uliotoka kinywani mwa joka. 17 Kisha lile joka likashikwa na ghadhabu kwa ajili ya huyo mama, likaondoka kwenda kupigana vita na watoto wake waliobakia, wale wanaozitii amri za Mungu na kumshuhudia Yesu. Lile joka likasimama kwenye mchanga wa bahari.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica