Previous Prev Day Next DayNext

Beginning

Read the Bible from start to finish, from Genesis to Revelation.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Ufunua wa Yohana 13-16

Mnyama Kutoka Baharini

13 Kisha nikaona mnyama akitoka baharini. Alikuwa na pembe kumi na vichwa saba na taji kumi kwenye pembe zake. Na kila kichwa kiliandikwa jina la kufuru. Huyo mnyama alifanana kama chui lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kinywa chake kama cha simba. Lile joka lilimpa mnyama huyo nguvu zake, kiti chake cha enzi na uwezo mkuu. Kichwa kimoja cha huyo mnyama kilione kana kama kilikwisha kuwa na jeraha lisiloweza kupona, lakini jeraha hilo lilikuwa limepona na dunia nzima ilimstaajabia huyo mnyama na kumfuata. Watu waliliabudu lile joka kwa sababu lili kuwa limempa huyo mnyama uwezo wake. Pia walimwabudu huyo mnyama wakisema, “Ni nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana naye?”

Kisha huyo mnyama akaruhusiwa kusema maneno ya kujisifu na ya kufuru na akapewa haki ya kutawala kwa muda wa miezi arobaini na miwili. Alisema maneno ya kumkufuru Mungu, akilitukana jina lake na mahali aishipo, yaani, aliwatukana wale waishio mbinguni. Pia aliruhusiwa kuwapiga vita watu wa Mungu na kuwashinda. Alipewa uwezo juu ya watu wa kila kabila, kila ukoo, kila lugha na taifa. Na watu wote waishio duniani watamwabudu, yaani kila mmoja ambaye tangu kabla ya ulimwengu kuumbwa, jina lake haliku andikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa.

“Aliye na nia ya kusikia, asikilize kwa makini: 10 Ye yote aliyepangiwa kuchukuliwa mateka atatekwa. Mtu ye yote akiua kwa upanga atauawa kwa upanga. Na hii ndio nafasi ya watu wa

Mnyama Kutoka Ardhini

11 Kisha nikamwona mnyama mwingine akipanda juu kutoka katika ardhi. Alikuwa na pembe mbili kama za mwana kondoo lakini aliongea kama joka. 12 Naye alitumia uwezo wote wa yule mnyama wa kwanza aliyemtangulia. Akalazimisha dunia yote na wote waliomo duniani wamwabudu huyo mnyama wa kwanza aliyekuwa na jeraha la kifo lililokuwa limepona. 13 Huyu mnyama wa pili akafanya miu jiza ya ajabu hata kufanya moto utoke mbinguni na kushuka duniani mbele ya watu. 14 Kwa njia ya miujiza aliyowezeshwa kufanya kwa niaba ya yule mnyama wa kwanza, aliwadanganya watu waishio duniani. Aliwaamuru watengeneze sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi. 15 Kisha akawe zeshwa kuipatia pumzi ile sanamu ya mnyama wa kwanza hata ikaweza kuongea na kufanya wale wote ambao hawakuiabudu wauawe. 16 Pia aliwalazimisha watu wote, wakubwa kwa wadogo, matajiri na mas kini, watu huru na watumwa, watiwe alama kwenye mikono yao ya kulia au kwenye vipaji vya nyuso zao. 17 Hakuna mtu ye yote ambaye angeweza kununua au kuuza kitu kama hana alama ile, yaani jina la huyo mnyama au namba ya jina lake.

18 Jambo hili linahitaji hekima. Mwenye akili ya kutambua apige hesabu ya mnyama huyo kwa sababu ni namba ya mtu. Namba yake ni mia sita sitini na sita.

Mwana-Kondoo Na Waliokombolewa Wa Kwanza

14 Kisha nikatazama na mbele yangu nikamwona Mwana-Kondoo amesimama juu ya Mlima Sioni akiwa pamoja na watu 144,000 ambao kwenye vipaji vya nyuso zao waliandikwa jina la Mwana-Kondoo na jina la Baba yake. Basi nikasikia sauti kutoka mbinguni kama sauti ya maporomoko ya maji mengi na kama sauti ya ngurumo ya radi kubwa. Na sauti hiyo niliyoisikia, ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi wakipiga vinubi vyao. Walikuwa wanaimba wimbo mpya mbele ya kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe hai wanne na wale wazee. Hakuna mtu aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao watu 144,000 waliokombolewa kutoka duniani. Hao ndio wale ambao hawakujitia unajisi kwa kuhusiana na wanawake, kwa kuwa wao ni bikira. Hao ndio wanaomfuata Mwana-Kondoo kila aendako. Wame nunuliwa kutoka miongoni mwa wanadamu wakawa matunda ya kwanza kutolewa kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo. Hawajapata kusema uongo kamwe; hawana hatia yo yote.

Malaika Watatu

Kisha nikamwona malaika mwingine akiruka juu angani akiwa na Injili ya milele ya kuwatangazia watu wote waishio duniani: kwa mataifa yote, makabila yote, kwa watu wa lugha zote na watu wa aina zote. Akasema kwa sauti kuu, “Mcheni Mungu na kumtu kuza kwa maana saa ya kutoa hukumu yake imefika. Mwabuduni yeye aliyeumba mbingu, dunia, bahari na chemchemi za maji.”

Malaika wa pili akafuata akisema, “Babiloni umeanguka! Babiloni mkuu umeanguka, ule mji mkuu ambao uliwanywesha mataifa yote divai yake, divai kali ya uzinzi wake.”

Malaika wa tatu aliwafuata hao wawili akisema kwa sauti kuu, “Kama mtu ye yote anamwabudu yule mnyama na sanamu yake na kukubali kutiwa alama yake kwenye kipaji cha uso wake au kwenye mkono wake, 10 yeye naye atakunywa divai ya ghadhabu ya Mungu ambayo imemiminiwa katika kikombe cha ghadhabu yake bila kuchan ganywa na maji. Naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya mal aika watakatifu na mbele za Mwana-Kondoo. 11 Moshi wa mateso yao hupanda juu milele na milele; wala hakuna nafuu, mchana au usiku, kwa wale wamwabuduo huyo mnyama na sanamu yake au kwa ye yote anayepokea alama ya jina lake.” 12 Jambo hili linahitaji watu wa Mungu, wale ambao wanazishika amri zake, wawe wavumilivu na kumwamini Yesu.

13 Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika haya: Wamebarikiwa watu ambao tangu sasa wanakufa wakiwa ndani ya Bwana.” “Naam,” asema Roho, “watapumzika baada ya taabu zao, kwa kuwa matendo yao yatawafuata.”

Mavuno

14 Nikatazama, na mbele yangu nikaona wingu jeupe na mtu anayeonekana kama ‘mwana wa mtu’ akiwa ameketi juu yake. Alikuwa na taji ya dhahabu kichwani mwake na mundu mkali mkononi mwake. 15 Na malaika mwingine akaja kutoka Hekaluni na kwa sauti kubwa akamwita yule aliyekuwa ameketi juu ya wingu akasema, “Chukua mundu wako ukavune kwa kuwa saa ya kuvuna imefika, maana mavuno ya dunia yamekomaa.” 16 Basi yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu akauzungusha mundu wake duniani, na mavuno ya dunia yakavunwa.

17 Kisha malaika mwingine akatoka Hekaluni mbinguni, naye pia akiwa na mundu mkali.

18 Na malaika mwingine, ambaye alikuwa na mamlaka juu ya moto, akatoka kwenye madhabahu akamwita yule malaika mwenye mundu mkali kwa sauti kuu, akasema, “Chukua mundu wako mkali ukayakate matawi ya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva.”

19 Basi malaika huyo akauzungusha mundu wake duniani akakata zabibu za dunia, akazitia ndani ya mtambo mkubwa wa kusindika zabibu wa ghadhabu ya Mungu. 20 Zabibu zikakamuliwa ndani ya mtambo huo wa kusindika zabibu uliokuwa nje ya mji, na damu ika tiririka kama mafuriko kutoka katika mtambo huo na urefu wa mafu riko hayo ulikuwa kama kilometa mia tatu, na kina chake kiasi cha meta moja na nusu.

Wimbo Wa Musa Na Mwana-Kondoo

15 Ndipo nikaona ishara nyingine mbinguni, ishara kubwa na ya ajabu: malaika saba wenye maafa saba ya mwisho, kwa maana, maafa hayo yanakamilisha ghadhabu ya Mungu.

Na nikaona kitu kama bahari ya kioo imechanganyika na moto. Na kando ya hiyo bahari, walikuwa wamesimama wale watu waliom shinda yule mnyama na sanamu yake pamoja na namba ya jina lake. Walikuwa wameshika vinubi walivyopewa na Mungu. Nao waliimba wimbo wa Musa, mtumishi wa Mungu na wimbo wa Mwana-Kondoo wakisema, ‘ ‘Matendo yako Bwana Mungu Mwenyezi, ni makuu na ya ajabu! Njia zako wewe Mfalme wa Mataifa ni za haki na za kweli! Ni nani asiyekucha wewe Bwana na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako ni mtakatifu. Mataifa yote yatakuja na kukuabudu kwa kuwa matendo yako ya haki yamekwisha dhihirishwa.”

Baada ya hapo nikatazama, nikaona mbinguni Hekalu, yaani hema ya ushuhuda, imefunguliwa. Basi wale malaika saba wenye maafa saba wakatoka humo Hekaluni wakiwa wamevaa nguo za kitani safi zing’aazo na vifuani mwao walivaa mikanda ya dhahabu. Kisha mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai, akawapa wale mal aika saba mabakuli saba ya dhahabu yalizojaa ghadhabu ya Mungu aishiye milele na milele. Na Hekalu ilijaa moshi uliotokana na utukufu na uweza wake, wala hakuna mtu aliyeweza kuingia Hekaluni mpaka yale maafa saba ya wale malaika saba yakamilike.

Mabakuli Saba Ya Ghadhabu Ya Mungu

16 Kisha nikasikia sauti kuu kutoka Hekaluni ikiwaambia wale malaika saba, “Nendeni mkamwage duniani yale mabakuli saba ya ghadhabu ya Mungu.”

Malaika wa kwanza akaenda akalimimina bakuli lake ardhini na madonda mabaya yenye maumivu makali yakawapata wote waliokuwa na alama ya yule mnyama na walioabudu sanamu yake.

Malaika wa pili akamimina bakuli lake baharini , ikawa kama damu ya mtu aliyekufa na kila kiumbe hai kilichokuwa ndani ya bahari kikafa.

Malaika wa tatu akamimina bakuli lake katika mito na chemchemi za maji, nazo zikageuka kuwa damu. Nami nikamsikia malaika wa maji akisema, “Umefanya haki katika hukumu hizi uli zotoa, wewe uliyeko na uliyekuwako, Mtakatifu. Maana walimwaga damu ya watakatifu na manabii, na wewe umewapa damu wanywe, kama walivyostahili.” Nikasikia madhabahu ikiitikia, “Naam, Bwana Mungu Mwenyezi, hukumu zako ni za kweli na haki.!”

Mungu Mwenyezi, hukumu zako ni za kweli na haki.!”

Malaika wa nne akamimina bakuli lake kwenye jua nalo lika pewa nguvu za kuwachoma watu kwa moto wake mkali. Watu wakaun guzwa na moto huo nao wakalaani jina la Mungu aliyekuwa na uwezo juu ya maafa haya, wala hawakutubu na kumtukuza.

10 Malaika wa tano akamimina bakuli lake kwenye kiti cha enzi cha yule mnyama, na ufalme wake ukawa gizani. Watu wakauma ndimi zao kwa uchungu 11 wakamlaani Mungu wa mbinguni kwa mau mivu yao na madonda yao, wala hawakutubu kwa ajili ya matendo yao maovu.

12 Malaika wa sita akamimina bakuli lake kwenye mto mkubwa wa Efrati, maji yake yakakauka ili kuwatayarishia njia wafalme kutoka mashariki. 13 Nikaona roho wachafu waliofanana na chura wakitoka katika kinywa cha lile joka na katika kinywa cha yule mnyama, na katika kinywa cha yule nabii wa uongo. 14 Hizo ni roho za pepo zitendazo miujiza. Nazo huwaendea wafalme wa ulim wengu wote na kuwakusanya tayari kwa vita, siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi. 15 “Sikiliza! Ninakuja kama mwizi! Amebarikiwa aliye macho, akiziweka tayari nguo zake ili asiende bila nguo na watu wakam wona uchi!” 16 Kisha wakawakusanya wafalme pamoja mahali ambapo huitwa “Armageddoni” kwa Kiebrania.

17 Malaika wa saba akamimina bakuli lake angani na sauti kuu ikatoka Hekaluni katika kile kiti cha enzi ikisema, “Imekwisha timia!” 18 Kukawa na miali ya umeme, sauti, ngurumo za radi na tetemeko kuu la ardhi. Hapajawahi kuwa na tetemeko la ardhi kama hilo tangu mwanadamu kuwapo, kwani lilikuwa tetemeko kubwa ajabu.

19 Ule mji mkuu uligawanywa katika sehemu tatu na miji yote ya mataifa ikaanguka. Mungu akakumbuka Babiloni kuu akainywesha kikombe cha divai ya hasira na ghadhabu yake. 20 Kila kisiwa kikatoweka wala milima haikuonekana. 21 Mvua kubwa ya mawe, mawe mazito karibu kilo hamsini, ikanyesha kutoka mbinguni ikawaangu kia wanadamu. Wanadamu wakamlaani Mungu kwa ajili ya maafa ya mvua ya mawe. Kwa maana lilikuwa ni pigo kuu la kutisha.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica