Previous Prev Day Next DayNext

Beginning

Read the Bible from start to finish, from Genesis to Revelation.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
2 Timotheo 1-4

Kutoka kwa Paulo mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, kulingana na ahadi ya uzima uliomo ndani ya Kristo Yesu. Kwa Timotheo, mwanangu mpendwa. Ninakutakia neema, rehema na amani kutoka kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.

Paulo Amtia Moyo Timotheo

Ninamshukuru Mungu ninayemtumikia kwa dhamiri safi, kama walivyomtumikia baba zangu, ninapokukumbuka usiku na mchana katika sala zangu. Nikiyakumbuka machozi yako, ninatamani sana kukuona ili nijazwe furaha. Nakumbushwa kuhusu imani yako ya kweli, imani ambayo walikuwa nayo bibi yako Loisi na mama yako Eunike na ambayo nina hakika, unayo. Kwa sababu hii nakukum busha ukichochee kile kipawa ulichopewa na Mungu wakati nilipo kuwekea mikono. Maana Mungu hakutupatia roho ya woga bali roho ya nguvu, ujasiri na kiasi.

Basi usione haya kumshuhudia Bwana wetu, wala usinionee haya mimi niliye mfungwa kwa ajili yake, bali uishiriki taabu kwa ajili ya Habari Njema kwa kadiri ya nguvu upewayo na Mungu. Yeye ametuokoa na kutuita tupokee maisha ya utakatifu; si kwa sababu ya matendo yetu mema bali kwa sababu ya makusudio yake na neema yake. Tulipewa neema hii katika Kristo Yesu tangu milele 10 na sasa imedhihirishwa kwa kuja kwake Mwokozi wetu Kristo Yesu ambaye ameondoa kifo kabisa na kuleta uzima na kutokufa kwa njia ya Injili. 11 Nami nimechaguliwa kuwa mhubiri, mtume na mwalimu wa Injili hii. 12 Ndio sababu ninateseka hivi. Lakini sioni aibu kwa maana ninamjua huyo niliyemwamini na nina hakika ya kuwa anaweza kutunza kile nilichomkabidhi, mpaka siku ile.

13 Tumia kama kielelezo cha mafundisho sahihi maneno ya kweli ambayo umeyasikia kutoka kwangu pamoja na imani na upendo katika Kristo Yesu. 14 Linda ile kweli ambayo umekabidhiwa na Roho Mtakatifu aishiye ndani yetu. 15 Bila shaka unafahamu kuwa watu wote katika jimbo la Asia wameniacha, wakiwemo Filego na Hermogene. 16 Bwana aonyeshe huruma yake kwa jamaa ya Onesiforo kwa sababu alinitia moyo mara nyingi na hakuonea aibu minyororo yangu. 17 Bali alipofika Roma alinitafuta kwa bidii mpaka akanipata. 18 Bwana amwezeshe kupata rehema kutoka kwa Bwana siku ile. Unafahamu pia jinsi alivyoni saidia huko Efeso.

Askari Mwaminifu Wa Kristo Yesu

Basi, wewe mwanangu, uwe imara katika neema iliyomo ndani ya Kristo Yesu. Na mambo ambayo ulinisikia nikiyasema mbele ya mashahidi wengi, uwakabidhi watu waaminifu ambao wataweza kuwa fundisha watu wengine pia. Vumilia mateso pamoja nasi kama askari mwema wa Kristo Yesu. Hakuna askari ambaye akiwa vitani hujishughulisha na mambo ya kiraia kwa sababu nia yake ni kumrid hisha yule aliyemwandika kuwa askari. Hali kadhalika mwanar iadha hawezi kupewa tuzo kama hakufuata masharti. Mkulima mwe nye bidii ndiye anayestahili kupata fungu la kwanza la mavuno. Yatafakari haya ninayokuambia, kwa maana Mungu atakupa ufahamu katika mambo yote.

Mkumbuke Yesu Kristo aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, aliyez aliwa katika ukoo wa Daudi. Hii ndio Injili yangu ninayoihubiri. Nami ninateseka kwa sababu ya Injili hii nikivaa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu halikufungwa minyororo. 10 Kwa hiyo ninavumilia taabu zote kwa ajili ya wateule wa Mungu, kusudi na wao pia wapokee wokovu uliomo ndani ya Kristo Yesu pamoja na utukufu wake wa milele.

11 Neno hili ni kweli kabisa: kwamba kama tumekufa pamoja naye, tutaishi pamoja naye pia. 12 Kama tukivumilia, tutatawala pamoja naye pia; kama tukimkana, naye pia atatukana. 13 Tusipo kuwa waaminifu, yeye huendelea kuwa mwaminifu kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.

Mfanyakazi Mwenye Kibali Mbele Za Mungu

14 Wakumbushe mambo haya na uwaamuru mbele za Bwana waache kubishana juu ya maneno. Hii haiwasaidii cho chote bali huwaanga miza wanaowasikiliza. 15 Jitahidi kujidhihirisha mbele za Mungu kama mtu aliyepata kibali chake, mfanyakazi asiyekuwa na sababu yo yote ya kuona aibu, ambaye hulitumia neno la kweli kwa usa hihi. 16 Jiepushe na maneno ya kipuuzi, yasiyo ya kimungu, kwa maana hayo huwavuta watu mbali na Mungu zaidi na zaidi. 17 Mafundisho yao yataendelea kuenea kama donda ndugu. Kati yao wamo Himenayo na Fileto 18 ambao wametanga tanga na kuiacha kweli wakisema kwamba ufufuo umekwishapita. Wanapotosha imani ya baadhi ya watu. 19 Lakini msingi thabiti wa Mungu umesimama imara ukiwa na muhuri wenye maneno haya: “Bwana anawajua walio wake,” na tena, “Kila anayelitaja jina la Bwana aache uovu.”

20 Katika nyumba ya kifahari kuna vyombo vya dhahabu na fedha na pia vimo vyombo vya mbao na vya udongo. Baadhi ya vyombo ni vya heshima lakini vingine sio. 21 Kama mtu akijitakasa na kujitenga na visivyo vya heshima atakuwa chombo cha kutumika kwa shughuli za kifahari; chombo kilichotakaswa kimfaacho Bwana wa nyumba, ambacho ni tayari kwa matumizi yote yaliyo mema. 22 Basi, kimbia tamaa za ujana, na utafute kupata haki, imani, upendo na amani pamoja na wote wamwitao Bwana kwa moyo safi.

23 Usijishughulishe na mabishano yasiyo na maana na ya kipumbavu kwa kuwa unajua ya kwamba hayo huleta ugomvi. 24 Na tena mtumishi wa Bwana hapaswi kuwa mgomvi. Anapaswa kuwa mpole kwa kila mtu na mwalimu mwenye uwezo, na mvumilivu. 25 Anapaswa kuwaonya wale wanaompinga kwa upole, kwa matumaini kwamba Mungu anaweza kuwajalia watubu na kuifahamu kweli; 26 fahamu zao ziwarudie tena, watoke katika mtego wa shetani ambaye amewafunga wafanye kama apendavyo.

Hatari Za Siku Za Mwisho

Lakini fahamu jambo hili: kwamba siku za mwisho kutakuwa na nyakati za taabu. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, watukanaji, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio na utakatifu; wasio na ubinadamu, wasiopenda kusuluhishwa, wachonganishi, walafi, wakatili, wasiopenda mema; wasaliti, wasiojali kitu, waliojaa majivuno, wapendao anasa badala ya kumpenda Mungu. Hao ni watu ambao kwa nje wataonekana kuwa wana dini, huku wakikana nguvu ya imani yao. Jiepushe na watu wa jinsi hiyo.

Maana miongoni mwao wamo wale waendao katika nyumba za watu na kuwateka wanawake dhaifu waliolemewa na dhambi na kuyumbishwa na tamaa za kila namna. Wao humsikiliza kila mtu lakini hawawezi kutambua kweli. Kama vile Yane na Yambre walivyopin gana na Musa, kadhalika watu hawa nao wanapingana na ile kweli. Ni watu wenye akili potofu, wenye imani ya bandia. Lakini hawa tafika mbali, kwa sababu ujinga wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama ulivyokuwa dhahiri ujinga wa hao watu wawili.

Maagizo Ya Paulo Kwa Timotheo

10 Bali wewe umeyafahamu mafundisho yangu, mwenendo wangu, makusudio yangu, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu, ustahimilivu wangu, 11 mateso yangu, taabu zangu. Umefahamu yote yaliyonipata huko Antiokia, Ikonia na Listra, mateso yote niliyostahimili; lakini Bwana aliniokoa katika hayo yote. 12 Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya kumcha Mungu ndani ya Kristo Yesu watateswa. 13 Lakini watu waovu na wadanganyifu watazidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika. 14 Bali wewe, udumu katika yale uliyojifunza na kuyaamini kwa uthabiti, ukitam bua umejifunza hayo kutoka kwa nani; 15 na jinsi ambavyo tangu utoto wako umeyafahamu Maandiko matakatifu ambayo yanaweza kukuelekeza kupokea wokovu kwa kumwamini Kristo Yesu. 16 Andiko zima lina pumzi ya Mungu nalo lafaa kwa mafundisho, kwa kuwaonya watu makosa yao, kuwaongoza na kuwafundisha katika haki 17 ili mtu wa Mungu awe kamili akiwa na nyenzo zote za kutenda kila jambo jema.

Maagizo Ya Mwisho

Ninakuamuru mbele za Mungu na mbele za Kristo Yesu ambaye atawahukumu walio hai na wafu; na kwa kuja kwake na ufalme wake: hubiri Neno; lisisitize wakati ufaao na wakati usiofaa; sadik isha, kemea, na kuonya kwa uvumilivu mkuu na mafundisho thabiti. Maana wakati unakuja ambapo watu hawatavumilia kusikia mafund isho yenye uzima; bali kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajilundi kia walimu tele watakaowaambia yale ambayo masikio yao yanatamani sana kuyasikia. Watakataa kabisa kusikia kweli na watageukia hadithi za uongo. Bali wewe uwe imara, katika mambo yote, vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiza wajibu wote wa huduma yako.

Maana mimi sasa ni tayari kutolewa kama sadaka, saa ya kuondoka kwangu imefika. Nimepigana ile vita njema, nimemaliza shindano, nimeitunza imani. Na sasa nimewekewa taji ya haki ambayo Bwana, mwamuzi wa haki, atanituza Siku ile; wala si mimi tu, bali na wote ambao wamengojea kwa hamu kuja kwake.

Maombi Ya Binafsi

Jitahidi kuja kuniona upesi 10 kwa sababu Dema, kwa kuu penda ulimwengu huu wa sasa, ameniacha akaenda Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia na Tito amekwenda Dalmatia.

11 Ni Luka peke yake ambaye yupo hapa pamoja nami. Mchukue Marko uje pamoja naye kwa sababu ananisaidia katika huduma yangu. 12 Nimemtuma Tikiko Efeso. 13 Utakapokuja, niletee lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa na vile vitabu, hasa vile vya ngozi.

14 Aleksanda mfua chuma alinitendea ubaya mkubwa. Mungu atamlipa kwa yale aliyonitendea. 15 Wewe pia ujihadhari naye kwa sababu alipinga vikali ujumbe wetu.

16 Nilipojitetea mara ya kwanza hakuna hata mmoja aliyekuwa upande wangu, kila mmoja alinikimbia. Naomba wasihesabiwe hatia kwa jambo hilo. 17 Lakini Bwana alisimama nami akanitia nguvu kutangaza Habari Njema kwa ukamilifu ili watu wote wa mataifa wapate kusikia. Na niliokolewa kutoka katika kinywa cha simba. 18 Bwana ataniokoa katika kila uovu na kunihifadhi mpaka niu fikie ufalme wake wa mbinguni. Atukuzwe Yeye milele na milele.

Salamu Za Mwisho

19 Nisalimie Prisila na Akila na wote waliomo nyumbani kwa Onesiforo. 20 Erasto alibaki Korintho. Trofimo nilimwacha akiwa mgonjwa huko Mileto.

21 Jitahidi kufika huku kabla ya majira ya baridi kali. Sal amu zako kutoka kwa Eubulo, Pude, Lino, Klaudia na ndugu wote.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica