Previous Prev Day Next DayNext

Beginning

Read the Bible from start to finish, from Genesis to Revelation.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
2 Wakorintho 5-9

Makao Ya Mbinguni

Kwa maana twajua kwamba kama hema hii tunamoishi tukiwa ulimwenguni itaharibiwa, tunalo jengo kutoka kwa Mungu, nyumba ya milele mbinguni, ambayo haikujengwa kwa mikono ya wanadamu. Maana sasa twaugua, tukitamani kuvikwa makao yetu ya mbinguni, kwa kuwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tena tukiwa uchi. Tukiwa bado tunaishi katika hema hii tunaugua na kulemewa, kwa maana hatutaki kukaa bila nguo bali tunatamani kuvikwa makao yetu ya mbinguni ili ile hali ya kufa imezwe na uhai. Mungu ndiye aliyetuandaa kwa shabaha hii, naye ametupa Roho wake kama mdha mana, kutuhakikishia mambo yajayo baadaye. Kwa hiyo wakati wote tuna ujasiri mkuu. Tunajua kwamba wakati tukiwa katika mwili huu, tuko mbali na nyumbani kwa Bwana. Tunaishi kwa imani na si kwa kuona. Nasema tuna ujasiri na ingekuwa afadhali kuuacha mwili huu tukaishi nyumbani na Bwana. Kwa hiyo, kama tuko nyumbani katika mwili huu au tuko mbali nao, lengo letu ni kumpendeza Bwana. 10 Kwa kuwa sisi sote inatubidi kusimama mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo. Na kila mmoja atapokea mema au mabaya, kulingana na matendo yake alipokuwa katika mwili.

Huduma Ya Upatanisho

11 Kwa hiyo tukijua umuhimu wa kumcha Bwana tunajaribu kuwa vuta watu. Mungu anatufahamu fika. Tunaamini kwamba dhamiri zenu pia zinatufahamu tulivyo. 12 Hatujaribu kujipendekeza kwenu tena, lakini tunataka kuwapeni nafasi mjisifu juu yetu ili muweze kuwajibu hao wanaojisifia mambo yanayoonekana badala ya mambo yaliyo moyoni. 13 Kama tumeehuka, ni kwa ajili ya Mungu; lakini kama tuna akili timamu ni kwa faida yenu. 14 Kwa kuwa upendo wa Kristo unatusukuma, tunaamini ya kuwa mmoja alikufa kwa ajili ya wote kwa hiyo wote walikufa. 15 Naye alikufa kwa ajili ya watu wote ili wote wanaoishi, wasiishi tena kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa na kufufuka tena kwa ajili yao.

16 Tangu sasa hatumtazami mtu ye yote namna ya kibinadamu, ingawaje hapo mwanzo tulimtazama Kristo kwa namna ya kibinadamu. Hatumtazami hivyo tena. 17 Kwa hiyo mtu akiwa ndani ya Kristo, amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita, tazama, mapya yamekuja. 18 Haya yote yanatoka kwa Mungu, ambaye kwa njia ya Yesu Kristo ametupatanisha na mwenyewe, na akatupa huduma ya upatanisho. 19 Ndani ya Kristo Mungu aliupatanisha ulimwengu na yeye mwe nyewe, asiwahesabie watu dhambi zao. Naye ametukabidhi ujumbe huu wa upatanisho.

20 Kwa hiyo sisi ni mabalozi wa Kristo, Mungu anatutumia sisi kuwasihi ninyi. Na sisi tunawasihi ninyi kwa niaba ya Kristo: mpatanishwe na Mungu. 21 Mungu alimfanya yeye ambaye hakujua dhambi, awe dhambi kwa ajili yetu ili ndani yake tupate kuwa haki ya Mungu.

Kama wafanyakazi pamoja na Mungu, tunawasihi msipokee neema ya Mungu bure . Kwa maana Mungu anasema: “Wakati ufaao niliku sikiliza, na siku ya wokovu nilikusaidia. Tazameni, huu ndio wakati ufaao; leo ndio siku ya wokovu.”

Matatizo Ya Paulo

Hatutaki kumwekea mtu ye yote kikwazo ili huduma yetu isionekane kuwa na kasoro. Badala yake, kwa kila njia tunaon yesha ya kuwa sisi ni watumishi wa Mungu kwa kuvumilia: katika taabu, katika misiba, katika shida katika kupigwa, kufungwa gerezani na katika fujo; katika kazi ngumu, kukosa usingizi usiku na katika njaa; katika usafi wa moyo, katika ufahamu, subira na wema; katika Roho Mtakatifu na upendo wa kweli; katika maneno ya kweli na katika uwezo wa Mungu; kwa silaha za haki mkono wa kulia na mkono wa kushoto; katika utukufu na katika aibu, katika sifa na katika lawama; tukiwa wa kweli lakini tukionekana kuwa walaghai; tukiwa maarufu lakini tukihesabiwa kama tusioju likana; tukiwa kama wanaokufa lakini tunaishi; tukiadhibiwa lakini hatuuawi; 10 tukiwa wenye huzuni lakini siku zote tukish angilia; tukionekana maskini lakini tukiwafanya wengi kuwa mata jiri; tukiwa kama wasio na kitu lakini tukiwa na vitu vyote.

11 Tumesema wazi nanyi, ninyi ndugu wa Korintho, na kuweka mioyo yetu wazi kabisa kwenu. 12 Sisi hatujizuii kuwapenda, bali ninyi mmeuzuia upendo wenu usitufikie . 13 Na sasa nasema kama na watoto wangu: ninyi pia fungueni mioyo yenu kabisa kwetu.

Msiambatane Na Wasioamini

14 Msiambatane pamoja na watu wasioamini. Kwa maana kuna uhusiano gani kati ya haki na uovu? Au kuna ushirika gani kati ya nuru na giza? 15 Kuna kuelewana gani kati ya Kristo na shetani? Mwamini ana uhusiano gani na asiyeamini? 16 Kuna uelewano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa kuwa sisi ni hekalu la Mungu aliye hai. Kama Mungu alivyosema, “Nitaishi ndani yao na kutembea kati yao, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. 17 Kwa hiyo, tokeni kati yao, mkajitenge nao, asema Bwana. Msiguse cho chote kisicho safi; ndipo nitawakaribisha kwangu. 18 Nami nitakuwa baba kwenu, nanyi mtakuwa vijana wangu na binti zangu, asema Bwana Mwenyezi.”

Kwa kuwa tumepewa ahadi hizi wapendwa, basi tujitakase kutokana na kila aina ya uchafu wa mwili na roho, na tufanye bidii kufikia ukamilifu kwa kuwa tunamcha Mungu.

Furaha Ya Paulo

Tupokeeni kwa moyo mweupe. Hatujamkosea mtu ye yote, hatu jampotosha mtu ye yote, wala hatujamdhulumu mtu ye yote. Sisemi haya ili kuwahukumu; kwa kuwa, kama nilivyosema mwanzo, tunawath amini kiasi ambacho mpo mioyoni mwetu wakati wote, ikiwa ni kufa pamoja au kuishi pamoja. Ninayo imani kubwa kwenu; ninawaonea fahari kubwa. Nimefarijika sana. Pamoja na taabu zetu zote, furaha yangu haina mfano.

Kwa maana hata tulipofika Makedonia, miili yetu haikuwa na amani. Tulitaabishwa kila upande, kwa nje kulikuwa na upinzani na mioyoni mwetu tulikuwa na hofu. Bali Mungu, ambaye hufariji wenye huzuni, alitufariji kwa kumleta Tito; na si kwa kuwa Tito alifika tu, bali pia kwa kuwa ninyi mlimfariji. Alitueleza juu ya upendo wenu, huzuni yenu na jinsi mlivyonihurumia, kwa hiyo furaha yangu iliongezeka sana.

Hata kama barua yangu iliwasikitisha, sasa sijuti kwamba niliiandika ingawa nilikuwa nimejuta. Naona barua yangu iliwahu zunisha, lakini kwa muda mfupi. Lakini sasa ninafurahi, si kwa kuwa mlihuzunika, bali kwa kuwa huzuni hiyo iliwafanya mtubu. Kwa maana mlihuzunika kama Mungu anavyopenda watu wahuzunike na hivyo hatukuwadhuru kwa njia yo yote. 10 Kwa maana huzuni ikitumiwa na Mungu huwafanya watu watubu dhambi zao wapate kuokolewa; nao wanakuwa hawana majuto. Lakini huzuni ya kidunia husababisha kifo. 11 Tazameni faida mlizopata kutokana na huzuni hii: bidii mliyo nayo; juhudi mliyofanya kujitetea, uchungu wenu, hofu yenu, upendo wenu, shauku yenu, na jinsi mlivyokuwa tayari kutoa adhabu inayostahili. Kwa kila njia mmethibitisha kuwa hamna hatia katika jambo hilo. 12 Kwa hiyo ingawa niliwaandikia, haikuwa kwa sababu ya huyo aliyekosa au huyo aliyekosewa. Lakini nilitaka ninyi wenyewe muone, mbele za Mungu, jinsi mnavyotupenda kwa moyo wote. 13 Kwa hiyo tumefarijika. Pamoja na faraja tuliyopata, tumefu rahi zaidi kwa kuona jinsi Tito alivyofurahi kwa kuwa mlimwondo lea wasi wasi aliokuwa nao. 14 Nilikuwa nimejisifu kwake juu yenu nanyi hamkuniaibisha. Kama jinsi yale niliyowaambia yalivy okuwa ya kweli, hali kadhalika kujisifu kwetu kwa Tito kuwahusu ninyi kumeonekana kuwa kweli pia. 15 Upendo wake kwenu unaongezeka sana anapokumbuka jinsi mlivyokuwa watii na jinsi mlivyompokea kwa hofu na kutetemeka. 16 Nafurahi kwa sababu nina imani nanyi kabisa.

Kutoa Kwa Ukarimu

Tunapenda mfahamu ndugu zetu, kuhusu neema ambayo Mungu amewapa makanisa ya Makedonia. Pamoja na majaribu makali na taabu walizopata, furaha yao na umaskini wao mkuu zimezaa utajiri wa ukarimu. Ninashuhudia kwamba walitoa kwa kadiri ya uwezo wao hata na zaidi ya uwezo wao. Kwa hiari yao wenyewe, walitusihi wapewe nafasi ya kushiriki katika huduma hii ya kuwasaidia watu wa Mungu. Na hawakufanya tulivyotazamia bali walijitoa wao wenyewe kwa Bwana kwanza na ndipo wakajitoa kwetu, kufuatana na mapenzi ya Mungu. Kwa hiyo tulimwagiza Tito, kwa kuwa ndiye aliyeanzisha jambo hili, akamilishe kazi hii ya neema pia kwa upande wenu. Basi, kama mlivyo mbele sana katika yote: katika imani, katika kutamka, katika juhudi na katika kutupenda, hakik isheni kuwa mnakuwa wa kwanza pia katika neema hii ya kutoa.

Siwapi amri, lakini nawaonyesha jinsi wengine walivyo tay ari kutoa ili kupima ukweli wa upendo wenu. Kwa maana mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye ingawa alikuwa tajiri, alikubali kuwa maskini kwa ajili yenu, ili kwa umaskini wake ninyi mpate kuwa matajiri. 10 Ushauri wangu kuhusu jambo hili ni huu. Ni vyema mkamilishe sasa jambo ambalo mlinia na mkaanza kulifanya tangu mwaka jana 11 ili wepesi wenu katika kunia ulin gane na kumaliza kwenu kutoa kwa kadiri ya mlicho nacho. 12 Kwa kuwa kama nia ya kutoa ipo, kitolewacho kinakubalika kufuatana na kile mtu alicho nacho, si kufuatana na kile ambacho mtu hana. 13 Nia yetu si kwamba wengine wasaidike wakati ninyi mnateseka bali pawe na uwiano. 14 Kwa wakati huu wingi wa vitu mlivyonavyo usaidie kutosheleza mahitaji yao, ili wakati wao wakiwa na wingi wa vitu, nao wapate kutosheleza mahitaji yenu. 15 Ndipo patakuwa na usawa, kama maandiko yanavyosema, “Aliyekusanya kwa wingi, hakubakiza kitu, na aliyekusanya kidogo hakupungukiwa.”

Tito Anatumwa Korintho

16 Tunamshukuru Mungu ambaye amempa Tito moyo wa kuwajali ninyi kama mimi ninavyowajali. 17 Si kwamba amekubali ombi letu tu, bali anakuja kwenu akiwa na ari na kwa hiari yake mwenyewe. 18 Pamoja naye tunamtuma ndugu ambaye anasifiwa na makanisa yote kwa huduma yake ya kuhubiri Injili. 19 Zaidi ya hayo, amechagu liwa na makanisa asafiri nasi kupeleka matoleo haya. Hii ni huduma ambayo tunafanya kwa utukufu wa Bwana na pia kuonyesha nia yetu ya kuwasaidia wengine. 20 Tumenuia kwamba mtu ye yote asiwe na sababu ya kutulaumu kuhusu jinsi tunavyosima mia matoleo haya ya ukarimu. 21 Tunajitahidi kuhakikisha kuwa tunafanya haki machoni pa Bwana na machoni penu, na wala si kama sisi tuonavyo vyema. 22 Pamoja na hawa, tunamtuma ndugu yetu ambaye tumempima mara nyingi tukamwona kuwa wa kweli na mwenye juhudi, hasa zaidi sana kwa kuwa ana imani kubwa kwenu. 23 Kumhusu Tito, yeye ni mwenzangu na mfanyakazi pamoja nami kwa ajili yenu. Kuhusu hawa ndugu wengine, wao ni wawakilishi wa makanisa, nao wanamletea Kristo utukufu. 24 Kwa hiyo, waonyesheni hawa ndugu upendo wenu na sababu inayotufanya tujivune kwa ajili yenu, ili makanisa yote yapate kuona.

Wasaidieni Wakristo Wenzenu

Hakuna sababu ya kuwaandikia kuhusu msaada unaotolewa kwa ajili ya watu wa Mungu, kwa kuwa ninajua mlivyo tayari kutoa, nami nimekuwa nikijivuna kwa ajili yenu kwa watu wa Makedonia, nikiwaambia kuwa ninyi wa Akaya mmekuwa tayari kutoa tangu mwaka jana. Ari yenu imewachochea wengi wao kuanza kutoa. Lakini sasa nawatuma hawa ndugu ili kujivuna kwetu kuhusu mchango wenu kusije kukawa ni maneno matupu, bali muwe tayari kama nilivyosema mko tayari. Isije ikawa nitakapokuja na watu wa Makedonia nikute hamko tayari niaibike, na ninyi zaidi, kwa kuwa nilishasema mko tayari. Kwa hivyo niliona ni muhimu niwahimize hawa ndugu watangulie kuja huko kabla yangu, wafanye mipango yote ya matoleo ya zawadi mliyoahidi ili iwe tayari, si kama mchango wa kulazim ishwa bali kama zawadi ya hiari.

Kumbukeni kwamba, mtu anayepanda mbegu chache, atavuna mazao machache; na mtu anayepanda mbegu nyingi atavuna mazao mengi. Kila mtu atoe kama anavyokusudia moyoni mwake, si kwa kusita au kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu anapenda mtu anayetoa kwa moyo. Na Mungu anaweza kuwapa kila baraka kwa wingi, ili kila wakati muwe na kila kitu kwa kiasi cha kutosha na ziada kwa ajili ya kila kazi njema. Kama Maandiko yanavyosema, “Yeye hutapanya kila mahali kuwapa maskini, haki yake hudumu milele.” 10 Na Mungu ambaye ndiye humpa mkulima mbegu za kupanda, na mkate kwa chakula, atawapa na kuzidisha mbegu mnazohitaji na kuziwezesha kukua zitoe mazao ya matendo mema ya haki. 11 Atawa fanya kuwa matajiri kwa kila hali ili mpate kuwa wakarimu kila wakati na kwa mchango wenu wa hiari kupitia kwetu, wengi wapate kumshukuru Mungu. 12 Huduma hii mnayofanya si kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya watu wa Mungu, bali utaleta mbubujiko wa shukrani nyingi kwa Mungu tu. 13 Kwa kutoa kwenu, mtakuwa mnatoa uthibitisho wa uhakika wa imani yenu. Ndipo watu watamtukuza Mungu kwa ajili ya utii wenu unaoambatana na kukiri kwenu kwa Injili ya Kristo, na kwa ukarimu wa mchango wenu kwao na kwa wen gine wote. 14 Nao watawaombea kwa upendo mwingi kwa ajili ya neema kuu mliyopewa na Mungu. 15 Tumshukuru Mungu kwa ajili ya zawadi hii isiyoelezeka.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica