Beginning
1 Kutoka kwa Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu aliye tumaini letu. 2 Kwa
Walimu Wa Uongo
3 Kama nilivyokusihi wakati nikienda Makedonia, napenda ukae hapo Efeso uwaamuru watu fulani wasiendelee kufundisha mafund isho ya uongo. 4 Pia wasiendelee kupoteza wakati wao kwa hadithi na orodha ndefu zisizo na mwisho za majina ya vizazi ambazo huchochea mabishano badala ya kuwajenga katika maarifa ya kimungu yatokanayo na imani. 5 Shabaha ya maagizo haya ni upendo utokao katika moyo safi, dhamiri njema na imani ya kweli. 6 Watu wengine wamepotoka na kuingia katika majadiliano yasiyo na maana kwa kuwa hawakuzingatia mambo haya. 7 Wanataka kuwa walimu wa sheria ingawa hawaelewi mambo wanayosema wala hayo wanayotilia mkazo.
8 Tunajua kwamba sheria ni njema iwapo inatumika ipasavyo. 9 Lakini tuelewe kwamba sheria haikuwekwa kwa ajili ya wenye haki, bali kwa ajili ya waasi na wasiotii: wasiomcha Mungu na wenye dhambi; wale wasio watakatifu, walio wachafu; wale wanaow aua baba zao na mama zao; wale wanaoua binadamu; 10 wale wal iowazinzi, wafiraji; wale wanaoteka watu nyara, na waongo, na wanaoapa kwa uwongo; na mengine mengi ambayo ni kinyume cha mafundisho ya kweli, 11 ambayo yanaambatana na Injili tukufu ya Mungu Mbarikiwa, ambayo nimekabidhiwa. 12 Nami namshukuru Kristo Yesu Bwana wetu, aliyenitia nguvu na kunihesabu kuwa ni mwaminifu kwa kunichagua nimtumikie. 13 Ingawa hapo mwanzo nilimkufuru na kumtesa na kumtukana, nili hurumiwa kwa sababu nilitenda hayo katika ujinga wangu na kutoku amini kwangu. 14 Na neema ya Bwana wetu ilimiminika tele kwa ajili yangu pamoja na imani na upendo uliomo ndani ya Kristo Yesu. 15 Neno hili ni la hakika tena linastahili kukubalika kabisa, kwamba Kristo Yesu alikuja duniani kuokoa wenye dhambi, ambao kati yao, mimi ni mwenye dhambi kuliko wote. 16 Lakini nilihurumiwa kwa sababu hii kwamba, kwa kunitumia mimi niliyekuwa mwenye dhambi kuliko wote, Kristo aonyeshe uvumilivu wake, niwe mfano kwa wote watakaomwamini na kupata uzima wa milele. 17 Basi, heshima na utukufu ni wake yeye Mfalme wa milele, asi yekufa wala asiyeonekana, aliye peke yake Mungu, milele na milele. Amina.
18 Mwanangu Timotheo, ninakukabidhi agizo hili, kufuatana na maneno ya unabii yaliyosemwa juu yako, ili kwa kuyafuata uweze kupigana ile vita njema, 19 ukishikilia imani na dhamiri njema. Watu wengine, kwa kukataa kuisikiliza dhamiri yao, wameangamiza imani yao. 20 Miongoni mwa watu hao wamo Himenayo na Aleksanda ambao nimewakabidhi kwa shetani, ili wajifunze wasimtukane Mungu.
Maagizo Kuhusu Ibada
2 Basi, kwanza kabisa, naagiza kwamba dua, sala, maombezi na shukrani zitolewe kwa ajili ya watu wote: 2 kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani, tukimcha Mungu na kuwa wenye heshima kwa kila njia. 3 Jambo hili ni jema na linampendeza Mungu Mwokozi wetu 4 ambaye anapenda watu wote waokolewe na wapate kuijua kweli. 5 Maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, yaani mwanadamu Kristo Yesu, 6 aliyejitoa mwenyewe kuwa fidia kwa ajili ya wote. Yeye ni uthibitisho wa mambo haya, uliotolewa kwa wakati wake. 7 Na hii ndio sababu nilichaguliwa niwe mhubiri na mtume, nasema kweli sisemi uwongo; nilichaguliwa niwe mwalimu wa watu wa mataifa katika imani na kweli.
8 Kwa hiyo, nataka kila mahali wanaume wasali wakiinua mikono iliyotakaswa pasipo hasira wala mabishano. 9 Kadhalika, nataka wanawake wajipambe kwa heshima na kwa busara. Mavazi yao yawe nadhifu, si kwa kusuka nywele, kujipamba kwa dhahabu, lulu na mavazi ya gharama kubwa, 10 bali kwa matendo mema kama iwapa savyo wanawake wanaokiri kuwa wanamcha Mungu. 11 Mwanamke na ajifunze katika utulivu na unyenyekevu.
12 Simruhusu mwanamke ye yote kufundisha au kuwa na mamlaka juu ya wanaume. Mwanamke anapaswa kukaa kimya. 13 Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza kisha Hawa; 14 na Adamu hakudanganywa bali mwanamke alidanganywa akawa mkosaji. 15 Lakini mwanamke ataoko lewa kwa kuzaa, kama ataendelea kudumu katika imani, upendo na utakatifu, pamoja na kujiheshimu.
Viongozi Katika Kanisa
3 Neno hili ni kweli, kwamba mtu akitaka kuwa askofu, anata mani kazi njema. 2 Basi, askofu awe mtu asiye na lawama. Awe mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtaratibu, mkarimu na aju aye kufundisha. 3 Asiwe mlevi, wala mgomvi bali awe mpole; asiwe mbishi wala mtu apendaye fedha. 4 Aweze kuisimamia nyumba yake vizuri akiwafanya watoto wake kuwa wanyenyekevu na wenye heshima katika hali zote. 5 Kwa maana kama mtu hawezi kuitawala nyumba yake mwenyewe atawezaje kuliangalia kanisa la Mungu? 6 Asiwe mtu aliyeongoka karibuni asije akajiona na kuhukumiwa kama shetani alivyohukumiwa. 7 Kadhalika, awe mwenye sifa njema kati ya watu wa nje ya kanisa, asije akalaumiwa na kuanguka katika mtego wa shetani.
Wasaidizi Katika Kanisa
8 Vivyo hivyo mashemasi wawe wenye kuheshimika, si wenye kauli mbili au wanywaji mno wa divai au wenye tamaa ya fedha. 9 Wanapaswa kuizingatia ile siri ya imani kwa dhamiri safi. 10 Ni lazima wapimwe kwanza na wakionekana kuwa wanafaa basi waruhusiwe kutoa huduma ya ushemasi. 11 Hali kadhalika, wake zao wawe wenye kuheshimika, si wasengenyaji bali wenye kiasi na waaminifu katika mambo yote. 12 Shemasi awe mume wa mke mmoja; na aweze kuwatawala watoto wake na jamaa yake vema. 13 Watu wanaotoa huduma njema ya ushemasi hujipatia heshima kubwa na uha kika mkubwa katika imani yao kwa Kristo Yesu.
14 Ninakuandikia mambo haya sasa ingawa natarajia kuwepo pamoja nawe karibuni, 15 ili kama nikicheleweshwa, upate kujua jinsi watu wanavyopaswa kuenenda katika nyumba ya Mungu, ambayo ni kanisa la Mungu aliye hai, nguzo na msingi wa kweli. 16 Bila shaka yo yote, siri ya dini yetu ni kuu: Alidhihirishwa katika mwili wa kibinadamu, alithibitishwa katika Roho, alionwa na mal aika, alihubiriwa kati ya mataifa, akaaminiwa ulimwenguni, aka chukuliwa juu katika utukufu.
Maagizo Kwa Timotheo
4 Roho anasema wazi wazi kwamba katika siku za mwisho watu wengine wataiacha imani yao na kusikiliza roho za udanganyifu na mafundisho ya mashetani. 2 Mafundisho hayo yanaletwa na wanafiki waongo ambao dhamiri zao zimekufa kama vile zimechomwa kwa chuma cha moto. 3 Wao wanawazuia watu kuoa; na wanawaamrisha watu wasile vyakula vya aina fulani - ambavyo Mungu aliviumba vipoke lewe kwa shukrani na wale wanaoamini na waliopata kuijua kweli. 4 Kwa maana kila kitu alichokiumba Mungu ni chema wala kitu cho chote kisikataliwe kama kinapokelewa kwa shukrani, 5 maana kina takaswa kwa neno la Mungu na kwa sala.
Mtumishi Mwema Wa Kristo
6 Ukiwapa ndugu mafundisho haya, utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu ambaye amelishwa vema kwa maneno ya imani na yale mafundisho mema uliyoyafuata. 7 Usijishughulishe kabisa na hadithi zisizo za kidini ambazo hazina maana. Jizoeze kuishi kwa kumcha Mungu. 8 Maana japokuwa mazoezi ya mwili yana faida kiasi, kumcha Mungu kuna faida kwa kila hali, kwa sababu kumcha Mungu kuna faida kwa maisha ya sasa na maisha yajayo.
9 Neno hili ni la kweli na linastahili kupokelewa, 10 na kwa ajili yake sisi tunajitahidi na kutaabika, kwamba tumeweka tumaini letu kwa Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa watu wote, hasa wale waaminio.
11 Agiza na kufundisha mambo haya. 12 Mtu asikudharau kwa kuwa wewe ni kijana, bali uwe mfano mwema kwa waamini wote kwa maneno yako, kwa mwenendo wako, katika upendo, imani na usafi.
13 Mpaka hapo nitakapokuja, tumia wakati wako katika kusoma Maandiko hadharani, kuhubiri, na kufundisha. 14 Usiache kutumia kipawa ulichonacho, ambacho ulipewa kwa neno la unabii wakati wazee wa kanisa walipokuwekea mikono. 15 Tekeleza mambo haya. Tumia nguvu zako na wakati wako kuyatimiza ili watu wote waone maendeleo yako.
16 Jilinde sana, na utunze mafundisho yako. Yashikilie, maana kwa kufanya hivyo utajiokoa wewe mwenyewe na wale wanaoku sikiliza.
Maagizo Kuhusu Wajane, Wazee Na Watumwa
5 Usimkemee mzee bali umwonye kama baba yako. Vijana uwaten dee kama ndugu zako. 2 Uwaheshimu mama wazee kama mama zako na akina mama vijana kama dada zako , kwa usafi wote.
3 Waheshimu Wajane walioachwa pekee, ipasavyo. 4 Kama mjane ana watoto ama wajukuu, hao watimize wajibu wao wa kidini kwa familia, kwa kuwahudumia wazazi na hivyo wawarudishie wema wal iowatendea. Kwa kufanya hivyo watampendeza Mungu. 5 Mwanamke ambaye kweli ni mjane na ameachwa peke yake, anamwekea Mungu tumaini lake naye huendelea kusali na kuomba usiku na mchana. 6 Lakini mwanamke aishie kwa anasa, amekufa, ingawa anaishi. 7 Wape maagizo haya, ili wasiwe na lawama. 8 Kama mtu hatunzi jamaa yake, hasa wale waliomo nyumbani mwake, ameikana imani yake, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.
9 Mjane ye yote ambaye hajafikia umri wa miaka sitini na ambaye alikuwa mwaminifu kwa mumewe, asiwekwe kwenye orodha ya wajane. Mjane anayestahili kuwekwa kwenye orodha hiyo lazima pia 10 awe mwenye sifa ya matendo mema, aliyewalea watoto wake vizuri, aliyekuwa mkarimu, aliyewaosha miguu watu wa Mungu, ali yewasaidia watu wenye taabu na aliyejitolea kufanya mema kwa kila njia. 11 Lakini wajane vijana usiwaweke kwenye orodha hiyo, maana tamaa zao za kimaumbile zikizidi kule kujitoa kwao kwa Kristo, watataka kuolewa tena. 12 Na kwa njia hiyo watajiletea hukumu kwa kuivunja ahadi yao ya mwanzo. 13 Isitoshe, wajane kama hao wana tabia ya uvivu wakizurura nyumba kwa nyumba. Tena hawawi wavivu tu, bali pia huwa wasengenyaji, wajiingizao katika mambo yasiyowahusu na kusema mambo wasiyopaswa kusema.
4 Kwa hiyo napenda wajane vijana waolewe, wazae watoto na watunze nyumba zao, ili yule adui asipate nafasi ya kusema uovu juu yetu. 15 Kwa maana wajane wengine wamekwisha kupotoka na kumfuata she tani.
16 Lakini kama mama mwamini anao ndugu ambao ni wajane, basi awatunze mwenyewe, kanisa lisibebe mzigo huo, ili liweze kuwat unza wale wajane ambao hawana msaada.
Wazee
17 Wazee wa kanisa wanaoongoza shughuli za kanisa vema wanastahili heshima mara mbili, hasa wale ambao kazi yao ni kuhu biri na kufundisha. 18 Maana Maandiko husema, “Ng’ombe apurapo nafaka usimfunge kinywa,” na tena, “Mfanyakazi anastahili msha hara wake.” 19 Usikubali kusikiliza mashtaka juu ya mzee wa kanisa kama hayakuletwa na mashahidi wawili au watatu. 20 Wale wanaoendelea kutenda dhambi uwaonye hadharani kusudi wengine wapate kuogopa.
21 Ninakuamuru mbele ya Mungu, na mbele ya Kristo Yesu na mbele ya malaika wateule, tekeleza maagizo haya pasipo kubagua wala upendeleo. 22 Usiwe na haraka kumwekea mtu mikono wala usishiriki katika dhambi za mtu mwingine, jiweke katika hali ya usafi.
23 Usiendelee kunywa maji tu bali tumia divai kidogo kwa ajili ya tumbo lako na maumivu yako ya mara kwa mara.
24 Dhambi za watu wengine ni dhahiri nazo zinatangulia huku muni mbele yao. Lakini dhambi za watu wengine huonekana baadaye. 25 Hali kadhalika matendo mema ni dhahiri na hata kama si dha hiri hayawezi kuendelea kufichika.
Watumwa
6 Watumwa wote wawahesabu mabwana zao kuwa wanastahili hesh ima zote, ili watu wasije wakalitukana jina la Mungu pamoja na mafundisho yetu. 2 Watumwa ambao mabwana zao ni waamini, wasikose kuwaheshimu kwa kuwa ni ndugu; bali watumike kwa ubora zaidi kwa sababu wale wanaonufaika kwa huduma yao ni waamini na ni wapendwa.
3 Fundisha na kuhimiza mambo haya. Mtu ye yote akifundisha kinyume cha haya na asikubaliane na maneno ya kweli ya Bwana wetu Yesu Kristo, na mafundisho yanayo ambatana na kumcha Mungu, 4 huyo amejaa majivuno na wala hafahamu cho chote. Mtu kama huyo ana uchu wa ubishi na mashindano ya maneno ambayo huleta wivu, ugomvi, matukano, shuku mbaya, 5 na ugomvi wa mara kwa mara kati ya watu wenye mawazo maovu, ambao hawanayo ile kweli, na ambao hudhani kwamba kumcha Mungu ni njia ya kuchuma fedha.
6 Bali kumcha Mungu na kuridhika ni faida kubwa. 7 Kwa maana hatukuja na kitu cho chote hapa duniani, wala hatuwezi kutoka na kitu. 8 Lakini kama tuna chakula na mavazi, basi tutaridhika. 9 Watu wanaotamani kuwa matajiri huanguka katika majaribu na mtego na katika tamaa nyingi mbaya na za kijinga, ambazo huwato komeza wanadamu katika upotevu na maangamizi. 10 Maana kupenda fedha ni chanzo cha uovu wote. Tamaa ya fedha imewafanya wengine watangetange mbali na imani na kuteseka kwa huzuni nyingi.
Mawaidha Ya Paulo Kwa Timotheo
11 Lakini wewe mtu wa Mungu, epuka haya yote. Tafuta kupata haki, utauwa, imani, upendo, subira na upole. 12 Pigana ile vita njema ya imani. Shikilia uzima wa milele ulioitiwa ulipokiri lile ungamo lako jema mbele ya mashahidi wengi.
13 Mbele ya Mungu ambaye amevipa vitu vyote uhai, na mbele ya Kristo Yesu ambaye kwa ushuhuda wake mbele ya Pontio Pilato alikiri lile ungamo jema, 14 ninakuamuru utunze amri hii bila doa wala lawama mpaka Bwana wetu Yesu Kristo atakapokuja. 15 Jambo hili Mungu atalitimiza kwa wakati wake mwenyewe, Mungu Mbarikiwa ambaye peke yake ndiye Atawalaye, Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. 16 Yeye peke yake ndiye asiyekufa, na ndiye aishiye katika nuru isiyoweza kukaribiwa; hakuna mwanadamu ali yepata kumwona wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye hata milele. Amina.
17 Uwaagize matajiri wa ulimwengu huu waache kujivuna, wala wasiweke matumaini yao katika mali ambayo haina hakika. Bali wam tumaini Mungu ambaye hutupatia vitu vyote kwa wingi ili tuvifu rahie. 18 Waambie watende wema, wawe matajiri katika matendo mema, wawe wakarimu na tayari kushiriki mali zao na wengine. 19 Kwa njia hii watajiwekea msingi imara kwa wakati ujao na hivyo watajipatia uzima ambao ni uzima kweli.
20 Timotheo, tunza vema yote uliyokabidhiwa. Epuka majadil iano yasiyo ya Mungu na mabishano ambayo kwa makosa huitwa elimu.
Copyright © 1989 by Biblica