Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Old/New Testament

Each day includes a passage from both the Old Testament and New Testament.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Error: Book name not found: Ps for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Matendo Ya Mitume 21:18-40

18 Kesho yake Paulo alikwenda nasi kwa Yakobo, na wazee wote wa kanisa walikuwepo. 19 Baada ya kuwasalimu, Paulo alitoa taarifa kamili ya mambo yote ambayo Mungu alifanya kati ya watu wa mataifa kwa kumtumia yeye. 20 Baada ya maelezo yake wote walimtukuza Mungu. Ndipo wakamwambia, “Unavyoona ndugu, kuna maelfu ya Wayahudi walioamini; nao wote wanaishika sheria kwa bidii. 21 Lakini wamekuwa wakiambiwa habari zako kuwa wewe umew afundisha Wayahudi wanaoishi na watu wa mataifa waache kushika sheria za Musa; na kuwaambia wasitahiri watoto wao, au kufuata mila za Kiyahudi. 22 Sasa tufanyeje? Kwa maana watasikia kwamba umefika Yerusalemu. 23 Kwa hiyo fanya kama tunavyokushauri. Tunao watu wanne hapa ambao wameweka nadhiri. 24 Wachukue hawa ukajitakase pamoja nao na ulipe gharama zao ili wanyoe nywele zao. Kwa njia hii kila mtu atafahamu ya kuwa mambo waliyosikia si ya kweli na kwamba wewe unashika sheria. 25 Lakini wale watu wa mataifa walioamini tumewapelekea barua tukiwaambia kuwa tumeamua wajitenge na kitu cho chote ambacho kimetolewa kwanza kama sadaka kwa miungu ya sanamu na wasinywe damu au kula nyama ya mnyama aliyeuawa kwa kunyongwa. Tena ni lazima wajitenge na uasherati.” 26 Kwa hiyo Paulo akawachukua wale watu na kesho yake akajita kasa pamoja nao. Akaingia ndani ya Hekalu ili akatoe taarifa ya tarehe ambayo siku zao za utakaso zitamalizika na sadaka kutolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.

Paulo Akamatwa

27 Zile siku saba zilipokaribia kumalizika, Wayahudi kutoka jimbo la Asia waliokuwa wamemwona Paulo ndani ya hekalu, waka chochea umati mkubwa wa watu wakamkamata Paulo. 28 Wakapiga kelele wakasema, “Ndugu Waisraeli, tusaidieni! Huyu ni yule mtu ambaye anafundisha watu kila mahali wawadharau watu wetu, wazid harau sheria zetu na hata hili Hekalu. Zaidi ya hayo amewaleta Wagiriki katika Hekalu na kuchafua hapa mahali patakatifu!” 29 Walisema hivi kwa sababu walimwona Trofimo, mwenyeji wa Efeso, akiwa mjini na Paulo wakadhani kuwa Paulo alikuwa amemleta Hekaluni . 30 Habari hizi zikawachochea watu wa mji mzima nao wakakimbia pamoja kwa hasira wakamkamata Paulo wakamtoa nje ya Hekalu. Milango ya Hekalu ikafungwa. 31 Walipokuwa wakitaka kum wua, habari zikamfikia Jemadari wa jeshi la askari wa Kirumi kwamba Yerusalemu yote ilikuwa katika hali ya machafuko. 32 Na mara yule jemadari akachukua maofisa wengine wa jeshi pamoja na maaskari wakakimbilia kwenye ile ghasia. Watu walipomwona jema dari na askari wakija, waliacha kumpiga Paulo. 33 Kisha yule jemadari akamkamata Paulo akaamuru afungwe kwa minyororo miwili. Akauliza yeye ni nani na alikuwa amefanya nini. 34 Baadhi ya watu wakapiga kelele wakieleza jambo moja na wengine wakieleza jingine. Yule jemadari alipoona kuwa hawezi kupata ukweli kamili kwa sababu ya zile kelele, akaamuru Paulo apelekwe katika ngome ya jeshi. 35 Basi walipofika penye ngazi, ilibidi askari wambebe Paulo juu juu kwa sababu ya fujo za ule umati wa watu 36 ambao walikuwa wakiwafuata wakipiga kelele, “Mwueni!”

Paulo Anajitetea

37 Walipokuwa wanakaribia kuingia katika ngome ya jeshi, Paulo alimwuliza yule jemadari, “Je, naweza kusema jambo moja?” Yule jemadari akajibu, “Kumbe unajua Kigiriki? 38 Wewe si yule Mmisri ambaye siku za karibuni alianzisha uasi akaongoza majam bazi elfu nne wenye silaha jangwani?” 39 Paulo akajibu, “Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso, jimbo la Kilikia na raia wa mji wenye sifa. Tafadhali niruhusu nizungumze na hawa watu.” 40 Yule jemadari alipomruhusu azungumze, Paulo akasimama penye ngazi akawapungia watu mkono ili wanyamaze. Watu walipokuwa kimya kabisa, Paulo akazungumza nao kwa lugha ya Kiebrania, akasema;

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica