Previous Prev Day Next DayNext

Beginning

Read the Bible from start to finish, from Genesis to Revelation.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
1 Wakorintho 5-8

Mwasherati Atengwe

Kuna habari thabiti kwamba miongoni mwenu kuna uasherati unaotendeka; tena ni uasherati wa aina ambayo hata watu wasiomjua Mungu hawafanyi. Nimesikia kwamba kuna mtu anazini na mama yake wa kambo! Mnawezaje basi kujivuna! Badala yake mngepaswa kuom boleza. Huyo aliyefanya tendo hili afukuzwe na kutengwa nanyi. Japokuwa sipo nanyi katika mwili, lakini nipo nanyi katika roho. Na nimekwisha toa hukumu kuhusu huyo mtu aliyetenda jambo hili, kama vile ningekuwapo. Mnapokutana katika jina la Bwana wetu Yesu nami nikiwepo katika roho, na nguvu ya Bwana wetu Yesu ikiwepo, mtoeni mtu huyu kwa shetani, ili asili yake ya dhambi iangamizwe lakini roho yake iokolewe siku ile ya Bwana.

Kiburi chenu hakifai. Hamjui kwamba hamira kidogo tu huumua donge lote la unga? Ondoeni chachu ya zamani ili mpate kuwa donge lisilo na chachu, kama mnavyotakiwa kuwa. Kwa maana Kristo ambaye ndiye Mwana-kondoo wetu wa Pasaka amekwisha tolewa kama dhabihu. Kwa hiyo, tusherehekee sikukuu hii, sio kwa chachu ya zamani, chachu ya nia mbaya na uovu bali kwa mkate usiotiwa hamira, wa moyo safi na kweli.

Niliwaandikia katika barua yangu kuwa msishirikiane na waasherati. 10 Sikuwa na maana kwamba msishirikiane na watu wa dunia walio waasherati, au wenye tamaa mbaya, wanyang’anyi au waabudu sanamu. Kufanya hivyo ingewabidi mtoke duniani. 11 Lakini nilikuwa namaanisha kwamba msishirikiane na mtu ye yote anayejiita ndugu lakini ni mwasherati, mwenye tamaa mbaya, mwabudu sanamu, mtukanaji, mlevi na laghai. Wala msile na mtu kama huyo.

12 Si kazi yangu kuhukumu watu walio nje ya kanisa. Je, si hao walio ndani ya kanisa mnaopaswa kuwahukumu? 13 Mungu anawa hukumu walio nje ya kanisa. “Mfukuzeni mtu mwovu atoke kutoka katika ushirika wenu.”

Kushtakiana Kati Ya Ndugu

Kama mmoja wenu ana mashtaka kumhusu ndugu, anathubutuje kupeleka mashtaka yake mbele ya mahakimu wasio mcha Mungu, badala ya kuyapeleka mbele ya watu wa Mungu? Hamjui kwamba watu wa Mungu watahukumu ulimwengu? Na kama ninyi mtahukumu ulimwengu, hamwezi kuhukumu mambo madogo madogo? Hamjui kwamba tutawahu kumu malaika? Je, si zaidi mambo ya maisha haya? Kwa hiyo kwa nini kama kuna kutokuelewana kati yenu kuhusu mambo kama haya, mnachagua kama mahakimu watu ambao hata hawaheshimiwi na kanisa? Nasema hivi ili muone aibu. Je, inawezekana kuwa hakuna mtu kati yenu mwenye hekima ya kutosha kuamua mashtaka kati ya ndugu mmoja na mwenzake? Badala yake ndugu mmoja anampeleka ndugu mwingine mahakamani, tena mbele ya watu wasioamini!

Kwamba mnashtakiana kati yenu ni dalili kuwa mmeanguka. Badala ya kushtakiana, kwa nini msikubali kutendewa ubaya? Kwa nini msikubali kudanganywa? Lakini ninyi wenyewe mnakoseana na kudhulumiana, na mnafanya hivyo hata kwa ndugu zenu!

Je, hamjui kwamba wasio na haki hawataurithi Ufalme wa Mungu? Msidanganyike, waasherati hawataurithi Ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wapotoshaji; 10 wala wezi, wala wenye tamaa mbaya, wala walevi, wala wanaodhihaki, wala wanyang’anyi. 11 Na baadhi yenu mlikuwa kama hao. Lakini mlioshwa, mlitakaswa, mlihesabiwa haki kwa jina la Bwana Yesu Kristo na katika Roho wa Mungu wetu.

Dhambi Za Zinaa

12 “Kila kitu ni halali kwangu,”lakini si kila kitu kina faida. “Kila kitu ni halali kwangu,”lakini sitatawaliwa na cho chote. 13 “Chakula ni kwa ajili ya tumbo, na tumbo ni kwa ajili ya chakula,” lakini Mungu ataviharibu vyote viwili. Mwili wa mwanadamu haukuumbwa kwa ajili ya zinaa bali kwa ajili ya Bwana, na Bwana kwa ajili ya mwili.

14 Mungu alimfufua Bwana na atatufufua na sisi pia kwa uwezo wake. 15 Je, hamjui ya kwamba miili yenu ni sehemu ya Kristo? Je, naweza kuchukua sehemu ya mwili wa Kristo na kuiunganisha na mwili wa kahaba? Hata kidogo! 16 Hamjui kwamba mtu aushirikishaye mwili wake na kahaba ana kuwa mmoja naye kimwili? Maandiko yanasema, “Hao wawili watakuwa mwili mmoja.” 17 Lakini mtu anayejiunga na Bwana ana kuwa mmoja naye kiroho.

18 Kimbieni dhambi ya zinaa. Dhambi nyingine zote anazotenda mwanadamu hufanyika nje ya mwili wake, lakini anayezini, ana tenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe. 19 Hamjui kwamba miili yenu ni Hekalu la Roho Mtakatifu anayekaa ndani yenu, ambaye mme pewa na Mungu? Ninyi si mali yenu wenyewe; 20 mmenunuliwa kwa bei kubwa. Kwa hiyo mtukuzeni Mungu katika miili yenu.

Kuhusu Ndoa

Na sasa kuhusu mambo mliyoniandikia. Ni vizuri mtu asioe. Lakini kwa kuwa dhambi ya zinaa imeenea, kila mwanamume awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe.

Mume atimize wajibu wake wa ndoa kwa mkewe; na hali kadhal ika mke kwa mumewe. Kwa maana mke hatawali mwili wake mwe nyewe, bali mume wake ndiye autawalaye. Vivyo hivyo, mume hata wali mwili wake mwenyewe, bali mkewe ndiye anayeutawala. Msiny imane, isipokuwa kama mmekubaliana kufanya hivyo kwa muda mfupi ili muwe na nafasi nzuri ya maombi. Lakini baada ya muda huo rudianeni tena shetani asije akapata nafasi ya kuwajaribu kwa sababu ya kushindwa kujizuia. Nasema haya kama ushauri, na si sheria. Ningalipenda wote wawe kama mimi nilivyo. Lakini kila mtu amepewa karama yake kutoka kwa Mungu, mmoja ana karama hii na mwingine ana karama ile.

Na sasa nasema kwa wale wasioolewa na kwa wajane. Ingekuwa vizuri kama wangeendelea kuishi bila kuoa au kuolewa kama mimi. Lakini kama hawawezi kujizuia, basi waoe. Ni afadhali kuoa kuliko kuwaka kwa tamaa.

10 Kwa wale waliooana ninayo amri, si amri yangu ila ni ya Bwana. Mke asimwache mumewe. 11 Lakini kama akimwacha, ni lazima akae bila kuolewa, ama sivyo apatane tena na mumewe. Na mume asimpe mkewe talaka.

12 Lakini kwa wengine nasema, si Bwana ila ni mimi: kama ndugu ana mke asiyeamini, na huyo mke amekubali kuishi pamoja naye, basi asimpe talaka. 13 Na kama mwanamke mwamini ameolewa na mwanaume asiyeamini, na huyo mwanaume amekubali kuishi naye, basi huyo mwanamke asimpe talaka. 14 Kwa maana huyo mwanaume asiyeamini anatakaswa kwa ajili ya mkewe naye mwanamke asiyeamini anatakaswa kwa ajili ya mumewe anayeamini. Kama isingalikuwa hivyo watoto wao wangalikuwa si safi, lakini ilivyo sasa wao ni watakatifu. 15 Lakini kama yule asiyeamini akitaka kuachana na mwenzake anayeamini, basi na iwe hivyo. Katika hali hiyo mke au mume ambaye ni mwamini hafungwi. Kwa sababu Mungu ametuita tuishi kwa amani. 16 Wewe mke, unajuaje kama hutamwokoa mumeo? Wewe mume unajuaje kama hutamwokoa mkeo?

Kuishi Kama Mlivyoitwa

17 Kila mtu aishi maisha aliyopangiwa na Bwana, na ambayo ameitiwa na Mungu. Hii ndio amri ninayotoa kwa makanisa yote.

18 Kama mtu alikuwa ametahiriwa alipoitwa, basi asijaribu kuondoa alama za kutahiriwa kwake. Na kama mtu alikuwa hajatahi riwa alipoitwa, basi, asitafute kutahiriwa. 19 Kwa kuwa kutahi riwa au kutotahiriwa si kitu. Jambo lililo muhimu ni kutii amri za Mungu . 20 Kila mtu abaki katika nafasi ambayo alikuwa nayo alipoitwa kuamini. 21 Je, wewe ulipoitwa ulikuwa mtumwa? Jambo hilo lisikusumbue. Lakini kama unaweza kuwa huru, utumie nafasi hiyo. 22 Kwa maana aliyeitwa kwa Bwana akiwa mtumwa ni mtu huru wa Bwana. Hali kadhalika mtu aliyekuwa huru alipoitwa ni mtumwa wa Kristo. 23 Mmenunuliwa kwa gharama; msikubali kuwa watumwa wa watu. 24 Kwa hiyo ndugu zangu, kila mmoja wenu akae na Mungu katika nafasi aliyokuwa nayo alipoitwa.

Kwa Hali Ya Sasa, Afadhali Kutokuoa

25 Sasa, kuhusu wale walio bikira. Sina amri yo yote kutoka kwa Bwana, lakini mimi natoa ushauri kama mtu aliyemwaminifu kwa rehema ya Bwana.

26 Kwa sababu ya dhiki iliyopo, nadhani itakuwa vyema mki baki kama mlivyo. 27 Je, umeoa? Basi usitake talaka. Kama hujaoa usitafute mke. 28 Lakini kama ukioa, hujatenda dhambi; na kama bikira akiolewa hajatenda dhambi. Lakini wanaooa watakabil iana na matatizo mengi katika maisha haya, nami ningependa myaep uke kwa kubaki mlivyo.

29 Nikisema hivyo ndugu zangu, nina maana kwamba muda uliobaki ni mfupi. Tangu sasa waliooa waishi kama hawakuoa; 30 na wana oomboleza kama hawaoombolezi; wenye furaha kama hawana furaha; wanaonunua kama walivyonunua si mali yao; 31 na wanaoshughulika na vitu vya dunia hii, kama hawahusiki navyo. Kwa maana dunia hii kama tunavyoiona sasa inatoweka.

32 Ningependa msiwe na wasiwasi. Mwanamume ambaye hajaoa anajishughulisha na mambo ya Bwana, jinsi ya kumpendeza. 33 Lakini mwanamume aliyeoa anajishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi ya kumfurahisha mke wake. 34 Kwa sababu hiyo, ana vutwa huku na huko. Mwanamke asiyeolewa au msichana bikira anaj ishughulisha na kazi ya Bwana, jinsi ya kuwa mtakatifu kimwili na kiroho. Lakini mwanamke aliyeolewa anajishughulisha na mambo ya dunia, jinsi ya kumfurahisha mume wake. 35 Ninasema haya kwa faida yenu na sio kuwawekea vikwazo. Napenda muishi sawa na kumpa Bwana maisha yenu yote. 36 Kama mtu anafikiri kwamba mwenendo wake kwa mchumba wake si sawa, na hasa kama mchumba wake anaanza kuzeeka, na anaona anawajibika kumuoa, basi afanye anavyoona vyema; waoane, si dhambi. 37 Lakini kama mwanamume ameshaamua moyoni mwake kuto kuoa bila kulazimishwa na mtu; kama anaweza kujitawala kabisa, basi anafanya vyema kutokumuoa mchumba wake. 38 Kwa hiyo mwana mume anayeamua kumuoa mchumba wake anafanya vizuri, lakini yule anayeamua kutokumuoa anafanya vizuri zaidi.

39 Mwanamke aliyeolewa amefungwa kwa mume wake maadamu anaishi. Kama mumewe akifa, basi mwanamke huyo yuko huru kuolewa na mume mwingine ampendaye, ila iwe katika Bwana. 40 Lakini kwa upande wangu naona kuwa angekuwa na furaha zaidi akibaki alivyo.

Chakula Kilichotolewa Sadaka Kwa Sanamu

Sasa kuhusu chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu. Tuna jua kwamba ‘sisi sote tuna ujuzi.’ Lakini ‘ujuzi’ huleta maji vuno, ila upendo hujenga. Mtu anayedhania kwamba anajua kitu, basi hajafahamu kama inavyompasa kujua. Lakini kama mtu anam penda Mungu, mtu huyo anajulikana na Mungu.

Kwa hiyo basi, kuhusu kula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu: tunajua kwamba ‘sanamu haina uhai wa kweli’ na kwamba ‘kuna Mungu mmoja tu.’ Kwa maana hata kama wapo hao wanaoitwa ‘miungu,’ kama ni mbinguni au duniani; na kwa kweli wapo ‘miungu’ wengi na ‘mabwana’ wengi; sisi tunajua kwamba kuna Mungu mmoja, aliye Baba, ambaye vitu vyote vinatoka kwake, na sisi tunaishi kwa ajili yake; na kuna Bwana mmoja, Yesu Kristo, ambaye vitu vyote vimekuwepo kupitia kwake na tunaishi kutokana naye.

Lakini si wote wanajua mambo haya. Watu wengine mpaka leo bado wamezoea miungu ya sanamu kiasi ambacho wanapokula chakula hicho wanadhani ni chakula kilichotolewa kwa sanamu, na kwa kuwa dhamiri yao ni dhaifu, inadhurika. Lakini chakula hakitusaidii kuwa karibu zaidi na Mungu. Hatupotezi cho chote tusipokula, wala hatupati faida yo yote kama tukila.

Lakini hata hivyo tuwe waangalifu jinsi tunavyotumia uhuru wetu tusije tukawakwaza walio dhaifu katika imani. 10 Kwa maana kama mtu mwenye dhamiri dhaifu akiwaona ninyi wenye ujuzi mkila katika hekalu la sanamu, je, si atavutwa kula chakula kilichoto lewa kwa sanamu? 11 Kwa njia hiyo, huyo ndugu mwenye dhamiri dhaifu, ambaye Kristo alimfia, atateketea kwa sababu ya ujuzi wako. 12 Mnapowatenda dhambi ndugu zenu kwa njia hii na kuharibu dhamiri zao dhaifu, mnamkosea Kristo. 13 Kwa hiyo kama chakula kitamfanya ndugu yangu aanguke katika dhambi, sitakula nyama kamwe, nisije nikamfanya ndugu yangu aanguke.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica