Print Page Options Listen to Acts 4-6
Previous Prev Day Next DayNext

Beginning

Read the Bible from start to finish, from Genesis to Revelation.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Matendo Ya Mitume 4-6

Petro Na Yohana Wakamatwa

Walipokuwa bado wanasema na watu, makuhani, mkuu wa walinzi wa Hekalu na Masadukayo waliwajia wakiwa wamekasirika kwa sababu Petro na Yohana walikuwa wakiwafundisha watu kwamba kufu fuka kwa Yesu kunadhihirisha kwamba wafu watafufuka. Wakawaka mata wakawaweka jela mpaka kesho yake kwa maana ilikuwa jioni. Lakini wengi wa wale waliosikia mahubiri yao waliamini; idadi ya wanaume walioamini ilikuwa kama elfu tano.

Siku ya pili yake viongozi wa Kiyahudi, wazee na waandishi wa sheria walikusanyika Yerusalemu. Walikuwepo Kuhani Mkuu Anasi, Kayafa , Yohana, Aleksanda na ndugu zake Kuhani Mkuu. Wakawaleta wale mitume wawili katikati yao wakawauliza, “Ni kwa uwezo gani au mmetumia jina la nani kufanya jambo hili?” Petro, akiwa amejawa na Roho Mtakatifu akajibu, “Waheshimiwa viongozi na wazee wa watu, kama mnatuhoji kuhusu mambo mema aliyotendewa kilema, na jinsi alivyoponywa, tungependa ninyi na watu wote wa 10 Israeli mfahamu kwamba, ni kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulubisha lakini Mungu akam fufua kutoka kwa wafu, kwa uwezo wa Yesu, huyu mtu anasimama mbele yenu akiwa mzima kabisa. 11 Huyu Yesu ndiye ‘lile jiwe ambalo ninyi wajenzi mlilikataa, ambalo limekuwa jiwe kuu la pembeni.’ 12 Wokovu unapatikana kwake tu; kwa maana hakuna jina jingine duniani ambalo wamepewa wanadamu kuwaokoa ila jina la Yesu, na ni kwa jina hilo peke yake tunaweza kuokolewa!”

Ujasiri Wa Petro Na Yohana Washangaza Watu

13 Wale viongozi na wazee walipoona ujasiri wa Petro na Yohana na kufahamu ya kuwa walikuwa watu wa kawaida wasio na elimu walishangaa sana. Wakatambua kwamba hawa watu walikuwa na Yesu. 14 Lakini kwa kuwa walimwona yule kilema aliyeponywa ame simama nao hawakuweza kusema lo lote kupinga maneno yao. 15 Wakawaamuru watoke nje ya ule ukumbi. 16 Kisha wakaanza kuulizana, “Tuwafanye nini watu hawa? Hatuwezi kukanusha muujiza huu mkubwa walioufanya ambao ni dhahiri kwa kila mtu Yerusalemu. 17 Lakini tunaweza kuzuia jambo hili lisiendelee kuenezwa kwa watu kama tukiwakanya wasiseme tena na mtu ye yote kwa jina la Yesu.” 18 Kwa hiyo wakawaita tena ndani wakawaamuru wasiseme au kufundisha watu tena kwa jina la Yesu.

Bora Kumtii Mungu Kuliko Wanadamu

19 Ndipo Petro na Yohana wakawajibu, “Ninyi amueni wenyewe lililo bora kutenda mbele za Mungu: kuwatii ninyi au kumtii Mungu. 20 Lakini sisi hatuwezi kuacha kusema yale tuliyoyaona na kuyasikia.”

21 Wale viongozi wakawaonya tena kwa vitisho, kisha waka waacha waende. Hawakuona njia ya kuwaadhibu kwa kuwa waliwaogopa wale watu ambao walishuhudia ule muujiza uliotendeka, nao wali kuwa wakimsifu Mungu. 22 Na yule mtu aliyeponywa alikuwa na umri wa zaidi ya miaka arobaini.

23 Mara Petro na Yohana walipoachiliwa, walirudi kwa waamini wenzao wakawaeleza waliyoambiwa na makuhani wakuu na wazee. 24 Waamini wote waliposikia maneno yao walimwomba Mungu kwa pamoja wakasema, “Wewe Bwana Mtukufu, uliyeumba mbingu na nchi na bahari na kila kiumbe kilichopo, 25 wewe ulitamka kwa njia ya Roho wako mtakatifu kupitia kwa baba yetu Daudi mtumishi wako, aliposema, ‘Mbona mataifa wanaghadhabika, na watu wanawaza mambo yasiyo na maana? 26 Wafalme wa dunia wamejiandaa na watawala wamekusanyika wampinge Bwana na Masihi wake.’ 27 Ndiyo sababu katika mji huu Herode na Pontio Pilato walikutana na Waisraeli wote na watu wa mataifa juu ya mtumishi wako mtakatifu Yesu, 28 wakaamua kumfanyia yale yote ambayo wewe ulikuwa umekusudia tangu awali na kupanga kwa uweza wako yatendeke.

29 “Sasa Bwana, sikia vitisho vyao na utuwezeshe sisi wat umishi wako kuhubiri neno lako kwa ujasiri mkuu; 30 na unyooshe mkono wako ili tuweze kuponya wagonjwa na kutenda ishara na miu jiza kwa jina la mtumishi wako mtakatifu Yesu.” 31 Walipokwisha kusali, nyumba waliyokuwa wamekutania ikatikisika na wote wakaja zwa na Roho Mtakatifu, wakahubiri neno la Mungu kwa ujasiri. 32 Waamini wote walikuwa na nia moja na moyo mmoja, wala hakuna aliyeona mali aliyokuwa nayo kuwa yake, bali walishirikiana vitu vyote kwa pamoja. 33 Na kwa uwezo mkubwa mitume wakashuhudia kwa ujasiri habari za kufufuka kwa Bwana Yesu. Mungu akawapa wote neema kuu. 34 Wala hakuwepo mtu ye yote miongoni mwa waamini aliyepungukiwa na kitu kwa sababu wale waliokuwa na mashamba na nyumba waliuza vyote wakaleta fedha waliyopata 35 kwa wale mitume; kila mtu akagawiwa kadiri ya mahitaji yake.

36 Ndivyo ilivyokuwa kwamba Yusufu ambaye mitume walimwita Barnaba, maana yake Mwana wa Faraja, wa ukoo wa Lawi kutoka kisiwa cha Kipro 37 aliuza shamba alilokuwa nalo akaleta fedha alizopata kwa wale mitume.

Anania Na Safira

Pia mtu mmoja jina lake Anania na mkewe Safira waliuza mali yao. Lakini Anania, kwa makubaliano na mkewe akaficha sehemu ya fedha alizopata, akaleta kiasi kilichobakia kwa mitume.

Petro akamwambia, “Anania, mbona shetani ametawala moyo wako kiasi cha kukubali kumdanganya Roho Mtakatifu, ukaficha sehemu ya fedha ulizopata? Kabla hujauza hilo shamba lilikuwa mali yako. Na hata baada ya kuliuza , fedha ulizopata zilikuwa zako. Kwa nini basi umeamua moyoni mwako kufanya jambo kama hili? Ujue hukumdanganya mtu ila umemdanganya Mungu.”

Ujue hukumdanganya mtu ila umemdanganya Mungu.”

Anania aliposikia maneno haya akaanguka chini akafa. Na wote waliosikia maneno haya wakajawa na hofu. Vijana wakaingia wakaufunga mwili wake wakamchukua nje kumzika.

Na baada ya muda wa saa tatu mkewe Anania akaingia, naye hakuwa na habari ya mambo yaliyotokea. Petro akamwuliza, “Niambie, je? Mliuza shamba lenu kwa kiasi hiki?” Akajibu, “Ndio, tuliuza kwa kiasi hicho.”

Ndipo Petro akamwambia, “Imekuwaje wewe na mumeo mkaamua kumjaribu Roho Mtakatifu wa Bwana? Tazama, vijana waliomzika mumeo wako mlangoni nao watakuchukua nje.”

10 Na mara akaanguka chini akafa. Wale vijana walipoingia wakamwona kuwa amekufa, wakamchukua wakamzika karibu na mumewe. 11 Waamini wote na watu wote waliosikia habari hizi wakajawa na hofu kuu.

Mitume Wafanya Miujiza Mingi Na Maajabu

12 Mitume walifanya miujiza mingi na ishara za ajabu. Na waamini wote walikuwa wakikusanyika katika ukumbi wa Sulemani. 13 Hakuna mtu mwingine aliyethubutu kujiunga nao lakini watu wote waliwaheshimu sana. 14 Hata hivyo watu wengi zaidi, wanaume kwa wanawake walikuwa wakiongezeka katika kundi la waliomwamini Bwana. 15 Hata walikuwa wakiwabeba wagonjwa wakawalaza kwenye mikeka barabarani ili Petro alipokuwa akipita kivuli chake kiwa guse angalau baadhi yao, wapone. 16 Pia watu walikusanyika kutoka katika miji iliyokuwa karibu na Yerusalemu wakileta wagonjwa na watu waliopagawa na pepo wachafu, hao wote wakapo nywa.

Mitume Washitakiwa

17 Kuhani mkuu na wale waliomuunga mkono, yaani Masadukayo, walijawa na wivu, 18 wakawakamata mitume na kuwatia gerezani.

19 Lakini usiku ule malaika wa Bwana akaja akawafungulia milango ya gereza akawatoa nje akawaambia, 20 “Nendeni mkasi mame Hekaluni mkawaambie watu habari za maisha haya mapya!”

21 Waliposikia haya wakaenda Hekaluni alfajiri wakaanza kufundisha watu. Kuhani Mkuu alipowasili pamoja na wenzake wakaitisha mkutano wa baraza na wazee wote wa Israeli wakatuma wale mitume waletwe kutoka gerezani. 22 Lakini wale maafisa wal iotumwa walipoingia gerezani hawakuwakuta wale mitume mle. Kwa hiyo wakarudi kutoa ripoti kwa baraza. 23 Wakasema, “Tumekuta milango ya jela imefungwa sawasawa, na maaskari wa gereza wamesi mama nje ya milango, lakini tulipofungua milango hakuwepo mtu ye yote ndani.”

24 Mkuu wa kikosi cha Walinzi wa Hekalu na makuhani wakuu waliposikia ripoti hiyo wakashangaa sana wasijue mambo haya yan geishia wapi. 25 Ndipo mtu mmoja akaja akawaambia, “Wale watu mliowatia gerezani wako Hekaluni wakiwafundisha watu.”

26 Ndipo yule mkuu wa kikosi cha walinzi wa Hekalu na wale maofisa wakaenda wakawaleta mitume lakini hawakuwadhuru kwa sababu waliogopa wangelipigwa mawe na watu. 27 Baada ya kuwaleta wakawaweka mbele ya baraza. Kuhani mkuu akaanza kuwahoji,

28 “Tuliwakanya msifundishe kwa jina la huyu mtu, lakini ninyi mmeeneza mafundisho yenu Yerusalemu yote, na tena mmeamua kuwa sisi tuna hatia juu ya kifo chake.”

29 Petro na wale mitume wengine wakajibu, “Imetupasa kumtii Mungu na sio wanadamu. 30 Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu ambaye ninyi mlimwua kwa kumtundika kwenye msalaba. 31 Mungu alimwinua, akamweka mkono wake wa kuume awe Mtawala na Mwokozi ili awape wana wa Israeli toba na msamaha wa dhambi. 32 Nasi tu mashahidi wa mambo haya pamoja na Roho Mtakatifu aliyetolewa na Mungu kwa watu wanaomtii.”

Mungu kwa watu wanaomtii.”

33 Wajumbe wa baraza la wazee waliposikia haya walijawa na ghadhabu, wakataka kuwaua wale mitume. 34 Lakini mmoja wao, Far isayo aitwaye Gamalieli ambaye alikuwa mwalimu wa sheria aliyeh eshimiwa na watu wote, akasimama akaamuru wale mitume watolewe nje kwa muda.

35 Ndipo alipowaambia wajumbe wa baraza, “Wazee wa Israeli, fikirini kwa uangalifu mtakalowatendea watu hawa! 36 Kumbukeni kuwa sio zamani sana tangu alipotokea mtu aliyeitwa Theuda ambaye alijidai kuwa yeye ni mtu maarufu, akapata wafuasi mia nne wal ioambatana naye. Lakini aliuawa na wafuasi wake wote wakatawany ika, kazi yake ikawa bure. 37 “Baada yake alitokea Yuda Mgali laya wakati ule wa sensa, akapata wafuasi wengi; lakini naye akauawa nalo kundi lake likatawanyika.

38 “Kwa hiyo, kwa kesi hii nawashauri waacheni watu hawa wala msiwatendee lo lote, kwa maana kama mpango wao na kazi yao ni mambo ya wanadamu hayatafika po pote; 39 lakini ikiwa ni kazi ya Mungu hamtaweza kuwazuia. Badala yake huenda mkajikuta mnam pinga Mungu!”

40 Wakapokea ushauri wa Gamalieli; wakawaita mitume ndani na baada ya kuwachapa viboko wakawaamuru wasifundishe kwa jina la Yesu. Wakawaachia waende zao. 41 Wale mitume walitoka barazani wamejaa furaha kwa sababu Mungu aliwapa heshima ya kupata aibu ya kuchapwa viboko kwa ajili ya jina la Yesu. 42 Na kila siku Hek aluni na nyumbani walizidi kuhubiri na kufundisha bila kukoma, juu ya Habari Njema kwamba Yesu ndiye Kristo.

Uchaguzi Wa Wahudumu

Siku hizo, wakati idadi ya waamini ilipokuwa ikiongezeka sana palitokea manung’uniko. Wayahudi walioongea lugha ya Kigi riki walilalamika kuwa wakati wa kugawa chakula, wajane walioon gea Kiebrania walipendelewa na wajane wao walibaguliwa. Wale mitume kumi na wawili waliitisha kikao cha wanafunzi wote, wakasema, “Si sawa sisi tuache kazi ya kuhubiri neno la Mungu tuanze kugawa chakula. Kwa hiyo ndugu, chagueni watu saba mion goni mwenu; watu wenye sifa njema, waliojawa na Roho Mtakatifu na hekima, ili tuwakabidhi kazi hii. Na sisi tutatumia wakati wetu kwa kuomba na kufundisha neno la Bwana.”

Uamuzi huu ukawaridhisha wote nao wakawachagua Stefano, mtu aliyejawa na imani na Roho Mtakatifu; na Filipo, Prokoro, Nika nori, na Timoni, Parmena na Nikolao mwongofu wa kutoka Antiokia. Wakawaleta watu hawa mbele ya mitume, nao wakawaombea na kuwawekea mikono juu yao.

Na neno la Mungu likazidi kuenea; idadi ya wanafunzi ika zidi kuongezeka sana katika Yerusalemu, na hata makuhani wengi wakamwamini Yesu.

Stefano Akamatwa

Na Stefano akiwa amejawa na neema na nguvu za Mungu alifa nya maajabu makubwa na ishara kati ya watu.

Lakini baadhi ya watu wa sinagogi lililoitwa la ‘Watu Huru,’ na wengine kutoka masinagogi ya Kirene na Aleksandria, pamoja na baadhi kutoka Kilikia na Asia, wakajaribu kubishana na Stefano. 10 Lakini hawakuweza kushindana naye kwa sababu ya hekima yake na Roho aliyemwezesha kusema.

11 Ndipo wakawashawishi watu fulani ambao walisema, “Tulim sikia akisema maneno ya kufuru juu ya Musa na Mungu.”

Stefano Afikishwa Mbele Ya Baraza

12 Wakawachochea watu, wazee na waandishi wa sheria nao wakamkamata Stefano wakamfikisha mbele ya baraza. 13 Wakaweka mashahidi wa uongo ambao walisema, “Mtu huyu siku zote anasema maneno ya kashfa juu ya Hekalu hili takatifu na juu ya sheria za Musa. 14 Kwa maana tumemsikia akisema kwamba eti huyu Yesu wa Nazareti ataharibu hili Hekalu takatifu na atabadilisha mila zote tulizopewa na Musa.” 15 Watu wote waliokuwa katika baraza hilo walimtazama Stefano kwa makini wakaona uso wake unang’aa kama uso wa malaika! Hotuba Ya Stefano

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica