Previous Prev Day Next DayNext

Beginning

Read the Bible from start to finish, from Genesis to Revelation.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Warumi 11-13

Huruma Ya Mungu Kwa Waisraeli

11 Kwa hiyo nauliza, je, Mungu amewakataa watu wake? La, sivyo. Mimi mwenyewe ni Mwisraeli, wa uzao wa Ibrahimu na wa kabila la Benjamini. Mungu hajawakataa watu wake ambao aliwajua tokea mwanzo. Hamfahamu Maandiko yanavyosema kuhusu Eliya, jinsi alivyomlalamikia Mungu kuhusu Waisraeli akisema, “Bwana, wamewaua manabii wako na kuziharibu madhabahu zako, nimebaki mimi peke yangu, nao wanataka kuniua? Na Mungu alimjibuje? “Nime bakiza kwa ajili yangu watu elfu saba ambao hawajapiga magoti kumwabudu Baali.” Ndivyo ilivyo hata sasa; wapo wachache wal iosalia ambao Mungu amewachagua kwa neema yake. Lakini ikiwa wamechaguliwa kwa neema, haiwezekani tena wakachaguliwa kwa msingi wa matendo. Kama ingekuwa hivyo, neema isingekuwa neema tena.

Tusemeje basi? Waisraeli walishindwa kupata kile ambacho walikitafutakwa bidii. Lakini waliochaguliwa walikipata. Wa liobaki walifanywa wagumu, kama Maandiko yasemavyo, “Mungu ali wapa mioyo mizito, na macho ambayo hayawezi kuona, na masikio ambayo hayawezi kusikia, hata mpaka leo.” Naye Daudi anasema: “Karamu zao na ziwe mtego wa kuwanasa, na kitu cha kuwakwaza waanguke na kuadhibiwa, 10 Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona, na migongo yao ipinde kwa taabu daima.”

Kurejeshwa Kwa Waisraeli

11 Nauliza tena, je, Waisraeli walipojikwaa walianguka na kuangamia kabisa? La sivyo! Lakini kwa sababu ya uhalifu wao, wokovu umewafikia watu wa mataifa mengine, ili Waisraeli waone wivu. 12 Ikiwa uhalifu wao umeleta utajiri mkubwa kwa ulimwe ngu, na kama kuanguka kwao kumeleta utajiri kwa watu wasiomjua Mungu, basi Waisraeli wote watakapoongoka itakuwa ni baraka kub wa zaidi.

13 Sasa ninasema nanyi watu wa mataifa mengine. Mimi ni mtume kwa watu wa mataifa na ninajivunia huduma hiyo 14 ili kuwafanya Wayahudi wenzangu waone wivu, na hivyo niwaokoe baadhi yao. 15 Kwa kuwa ikiwa kukataliwa kwao kumefanya ulimwengu wote upatanishwe na Mungu, kuokolewa kwao je, si kutakuwa ni uhai kutoka kwa wafu? 16 Na kama sehemu ya kwanza ya unga ulioumuliwa ni wakfu, basi unga wote ni wakfu; na kama shina ni wakfu, matawi nayo yatakuwa wakfu.

17 Lakini kama baadhi ya matawi yamekatwa, na ninyi kama mizeituni mwitu mkapandwa katika shina, mkashiriki pamoja na matawi mengine chakula kutoka katika shina la mzeituni, 18 msi jivune mbele ya hayo matawi. Kama mkijisifu mkumbuke kuwa si ninyi mnaoshikilia shina, bali ni shina linalowashikilia ninyi. 19 Pengine mtasema, “Matawi yalikatwa ili nipate nafasi ya kupandikizwa katika shina.” 20 Hii ni kweli. Lakini kumbuka kuwa matawi hayo yalikatwa kwa sababu ya kutokuamini; na wewe umesimama imara kwa sababu ya imani. Kwa hiyo usijisifu, bali ujinyenyekeze na kuogopa. 21 Kwa maana kama Mungu hakuyahurumia matawi ya asili, hatakuacha wewe, atakuondoa. 22 Tafakari basi kuhusu wema na ukali wa Mungu. Yeye ni mkali kwa wale walio anguka, bali amekuonyesha wewe wema wake, kama utadumu katika wema wake. Vinginevyo, na wewe utakatiliwa mbali. 23 Na hata hao Waisraeli, kama wakiacha kudumu katika kutokuamini kwao, atawar udisha kwenye shina, kwa maana Mungu anao uwezo wa kuwarejesha. 24 Ikiwa ninyi mmekatwa kutoka katika mizeituni mwitu, na ki nyume cha asilia mkapandikizwa kwenye mzeituni uliopandwa, ita kuwa ni rahisi kiasi gani matawi haya ya asili kurejeshwa kwenye shina lake?

Huruma Ya Mungu Ni Kwa Wote

25 Ndugu zangu, napenda mfahamu siri hii, msije mkaanza kujiona. Waisraeli wamekuwa na mioyo migumu kwa kiasi fulani mpaka idadi kamili ya watu wa mataifa mengine watakapoamini. 26 Na ndipo Waisrael wote wataokoka kama ilivyoandikwa, “Mko mbozi atakuja kutoka Sayuni, na kuuondoa uasi wote kutoka katika uzao wa Yakobo. 27 Na hii itakuwa ni agano langu nao, nitakapoondoa dhambi zao.”

28 Basi Waisraeli ni maadui wa Mungu kwa sababu ya Injili. Hii ni kwa faida yenu. Lakini kuhusu uchaguzi, Waisraeli bado ni wapendwa wa Mungu kwa sababu ya ahadi yake kwa Abrahmu, Isaki na Yakobo. 29 Kwa maana karama za Mungu na wito wake hazifutiki. 30 Kama ninyi zamani mlivyokuwa mmemwasi Mungu na sasa mmepokea rehema kwa sababu ya kutokutii kwao, 31 hivyo nao Waisraeli wamekuwa waasi kwa ajili ya rehema mliyopata kutoka kwa Mungu, ili wao pia wapate rehema. 32 Kwa maana Mungu amewaachia wana damu wote wawe katika uasi, ili aweze kuwahurumia wote.

Wimbo Wa Shukrani

33 Jinsi utajiri wa Mungu ulivyo mkuu! Hekima yake na maarifa yake hayana mwisho. Njia zake na maamuzi yake hayachu nguziki! 34 Kwa maana ni nani amepata kufahamu mawazo ya Mungu au kuwa mshauri wake? 35 Au ni nani amewahi kumpa cho chote ili arudishiwe? 36 Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake na vipo kwa ajili yake na vyote vinadumu kwake. Utukufu ni wake milele. Amina.

Ibada Ya Kiroho

12 Kwa hiyo ndugu zangu nawasihi kwa sababu ya huruma zake Mungu, jitoeni kwake muwe sadaka hai, takatifu na inayompendeza Mungu, ambayo ndio ibada yenu ya kiroho. Msiige tabia na mien endo ya dunia hii bali mbadilishwe, nia zenu zikifanywa kuwa mpya, ili mpate kuwa na hakika ni nini mapenzi ya Mungu: yaliyo mema, yanayopendeza machoni pake na makamilifu.

Kwa sababu ya neema niliyopewa nawaambia kila mmoja wenu: Msijifikirie kuwa watu wa juu kuliko mlivyo. Badala yake, muwe na kiasi katika mawazo yenu, kila mmoja wenu ajipime kutokana na kiasi cha imani aliyopewa na Mungu. Kama vile ambavyo kila mmoja wenu ana mwili mmoja wenye viungo vingi, na kila kiungo kina kazi yake, hali kadhalika, ndani ya Kristo sisi tulio wengi tunakuwa mwili mmoja na kila mmoja wetu ni sehemu ya we ngine wote. Tumepewa vipawa tofauti kulingana na neema tuliy opokea kutoka kwa Mungu. Kama mtu ana kipawa cha kutoa unabii basi akitumie kulingana na imani yake. Kama kipawa chake ni kuwahudumia wengine, basi awahudumie. Kama ni kufundisha, basi na afundishe. Kama kipawa chake ni kuwatia moyo wengine, na afanye hivyo. Kama ni ukarimu, basi na atoe kwa moyo. Mwenye kipawa cha uongozi na afanye hivyo kwa bidii. Mwenye kipawa cha huruma na aonyeshe huruma yake kwa furaha.

Upendo Wa Kweli

Upendo wenu uwe wa kweli. Chukieni uovu, mshikilie yaliyo mema. 10 Pendaneni ninyi kwa ninyi kwa upendo wa kindugu. Waheshimuni wengine kuliko mnavyojiheshimu wenyewe. 11 Juhudi yenu isipungue, moto wenu wa kiroho uendelee kuwaka mkimtumikia Mungu. 12 Muwe na furaha katika tumaini lenu, na katika dhiki muwe na subira. Ombeni wakati wote. 13 Wasaidieni watu wa Mungu walio na shida. Muwe wakarimu kwa matendo.

14 Waombeeni baraka za Mungu wanaowatesa. Wabarikini wala msiwalaani. 15 Furahini pamoja na wenye furaha; huzunikeni pamoja na wenye huzuni. 16 Muishi kwa amani ninyi kwa ninyi. Msitake makuu bali muwe tayari kushirikiana na wanyonge. Kamwe msiwe watu wenye majivuno.

17 Msimlipe mtu uovu kwa uovu. Jitahidini kutenda yaliyo mema machoni pa watu wote. 18 Kama ikiwezekana, kaeni kwa amani na watu wote. 19 Wapendwa, msijilipizie kisasi, bali mtoe nafasi kwa ghadhabu ya Mungu, maana imeandikwa:“Kisasi ni juu yangu; Mimi nitalipa, asema Bwana. 20 Badala yake, adui yakoakiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe kitu anywe. Maana ukifanya hivyo, utampalia mkaa wa moto kichwani pake. 21 Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.

Kutii Mamlaka

13 Kila mtu hana budi kutii serikali inayotawala. Kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na serikali zote zilizopo zimewekwa na Mungu. Kwa hiyo anayepinga mamlaka inayotawala ana pinga chombo kilichowekwa na Mungu; na watu wanaoasi watajiletea hukumu. Kwa maana watawala hawatishi watu wanaotenda mema bali wale wanaotenda maovu. Kama hupendi kuishi kwa kumwogopa mwenye mamlaka, basi tenda mema naye atakusifu. Maana mwenye mamlaka ni mtumishi wa Mungu kwa manufaa yako. Lakini kama ukitenda maovu, basi ogopa kwa maana hatembei na silaha bure. Yeye ni mtumishi wa Mungu anayetekeleza adhabu ya Mungu juu ya watenda maovu. Kwa hiyo ni lazima kutii wenye mamlaka, si kwa sababu ya kuogopa adhabu tu bali pia kwa ajili ya dhamiri.

Kwa sababu hiyo hiyo mnalipa kodi, kwa maana watawala ni watumishi wa Mungu ambao hutumia muda wao wote kutawala. Wal ipeni wote haki zao; mtu wakodi mlipe kodi; na mtoza ushuru mli pe ushuru; astahilie kunyenyekewa, mnyenyekee; astahiliye hesh ima, mheshimu.

Upendo Na Sheria

Msiwe na deni la mtu ye yote; isipokuwa deni la kupendana; kwa maana ampendaye mwenzake, ameitimiza sheria. Kwa maana amri zisemazo: Usizini, Usiue, Usiibe, Usitamani na amri nyingine zote, zinajumlishwa katika amri hii moja: “Mpende jirani yako kama nafsi yako.” 10 Upendo haumfanyii jirani jambo baya, kwa hiyo upendo unakamilisha sheria zote.

11 Fanyeni hivi mkitambua kuwa sasa tumo katika wakati gani. Huu ni wakati wa kuamka kutoka usingizini, kwa maana wokovu wetu umekaribia zaidi sasa kuliko wakati tulipoamini kwa mara ya kwanza. 12 Usiku unakwisha na mchana unakaribia. Kwa hiyo tutupe kando matendo ya giza, tuvae silaha za nuru. 13 Tuishi maisha ya heshima kama inavyopasa wakati wamchana: si kwa ulafi na ulevi; si kwa ufisadi na uasherati; si kwa ugomvi na wivu. 14 Bali jivikeni Bwana Yesu Kristo, na msitoe nafasi kwa miili yenu yenye asili ya dhambi, kutimiza tamaa zake.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica