Print Page Options Listen to Acts 18-20
Previous Prev Day Next DayNext

Beginning

Read the Bible from start to finish, from Genesis to Revelation.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Matendo Ya Mitume 18-20

Paulo Aenda Korintho

18 Baada ya haya, Paulo aliondoka Athene akaenda Korintho. Huko alimpata Myahudi mmoja jina lake Akila, mzaliwa wa Ponto, ambaye alikuwa amewasili karibuni kutoka Italia pamoja na mkewe Prisila, kwa sababu mfalme Klaudio alikuwa ameamuru Wayahudi wote waondoke Rumi. Paulo akaenda kuwaona. Akakaa nao na kufanya kazi na Akila kwa sababu wote wawili walikuwa mafundi wa kutengeneza mahema. Kila siku ya sabato Paulo alikwenda katika sinagogi akajaribu kuwavuta Wayahudi na Wagiriki waamini. Sila na Timotheo walipofika kutoka Makedonia walimkuta akihubiri na kuwashuhudia Wayahudi na Wagiriki, kuwa Yesu ndiye Kristo. Wal ipombishia na kumtukana alikung’uta mavazi yake akawaambia, “Mimi sina lawama, mkipotea , lawama iko juu yenu wenyewe. Tangu sasa nitawahubiria mataifa neno la Mungu.” Kwa hiyo Paulo akaondoka akaenda kwenye nyumba ya mtu anayeitwa Titio Yusto ali yekuwa mcha Mungu. Nyumba yake ilikuwa karibu sana na sinagogi. Kiongozi wa hilo sinagogi aliyeitwa Krispo akamwamini Bwana pamoja na jamaa yake; na Wakorintho wengi waliomsikia Paulo wakaamini na kubatizwa. Usiku mmoja Bwana akazungumza na Paulo katika ndoto akamwambia, “Usiogope, endelea kuhubiri wala usi kate tamaa. 10 Kwa maana mimi niko pamoja nawe, wala hakuna mtu atakayeweza kukushambulia na kukudhuru; kwa kuwa kuna watu wengi walio wangu katika mji huu.” 11 Kwa hiyo Paulo akakaa Korintho kwa muda wa mwaka mmoja na nusu, akiwafundisha waamini neno la Mungu. 12 Lakini wakati Galio alipofanywa kuwa Liwali wa Akaya, Wayahudi waliungana kumshambulia Paulo, Wakamkamata na kumpeleka Mahakamani. 13 Wakamshitaki wakisema, “Mtu huyu anawashawishi watu wamwabudu Mungu kinyume cha sheria zetu.” 14 Paulo alipo taka kujitetea Galio akawaambia Wayahudi, “Kama mashtaka yenu yalihusu makosa ambayo mtu huyu amefanya au kama yangehusu ujam bazi, ningewasikiliza. 15 Lakini kwa kuwa kesi hii inahusu maneno na majina yaliyo katika sheria zenu, itawabidi muiamue wenyewe. Nakataa kabisa kujihusisha na jambo hili.” 16 Akawafu kuza kutoka mahakamani. 17 Wakamkamata Sosthene, kiongozi wa sinagogi, wakampiga mbele ya mahakama. Wala Galio hakuingilia kati.

Paulo Arudi Antiokia

18 Baada ya haya Paulo alikaa huko Korintho kwa siku nyingi zaidi kisha akaagana na wale ndugu waamini akasafiri kwa meli kuelekea Siria akiongozana na Prisila na Akila. Walipofika Kenk rea Paulo alinyoa nywele zake kwa maana alikuwa ameweka nadhiri. 19 Walipofika Efeso Paulo aliwaacha Prisila na Akila, akaenda katika sinagogi akawa akijadiliana na Wayahudi. 20 Walipomwambia akae nao kwa muda mrefu zaidi alikataa, 21 lakini alipokuwa aki waaga aliwaambia, “Nitarudi kama Mungu akipenda.” Akasafiri kwa meli kutoka Efeso. 22 Alipofika Kaisaria alikwenda kuwasalimu ndugu katika kanisa kisha akaelekea Antiokia. 23 Alikaa Antiokia kwa muda, na baadaye aliondoka akatembelea makanisa huko Galatia na Frigia, akiwaimarisha waamini wote.

Apolo Ahubiri Efeso Na Korintho

24 Basi Myahudi mmoja jina lake Apolo, mwenyeji wa Aleksan dria alikuja Efeso. Yeye alikuwa mtu mwenye uwezo mkubwa wa kuhu biri na pia aliyajua Maandiko barabara. 25 Alikuwa amefundishwa njia ya Bwana naye akiwa amejaa moto wa kiroho alifundisha kwa usahihi juu ya Yesu. Lakini ujuzi wake uliishia kwenye ubatizo wa Yohana. 26 Apolo alihubiri kwa ujasiri mkubwa katika sinagogi. Lakini Prisila na Akila walipomsikiliza walimchukua nyumbani kwao wakamfundisha njia ya Mungu kwa ukamilifu zaidi. 27 Na alipoamua kwenda Akaya, ndugu wa Efeso walimtia moyo wakampa na barua ya kumtambulisha kwa ndugu wa huko. Alipofika aliwasaidia sana watu wengi ambao kwa neema ya Mungu walikuwa wameamini; 28 maana kwa uwezo mkubwa aliwakanusha hadharani Wayahudi waliokuwa wakipinga Habari Njema kwa kuwaonyesha kutoka katika Maandiko kuwa Yesu ndiye Kristo.

Waamini Wa Efeso Wapokea Roho Mtakatifu

19 Wakati Apolo alikuwa Korintho, Paulo alipitia sehemu za kaskazini akafika Efeso. Huko aliwakuta wanafunzi kadhaa, aka wauliza, “Mlipoamini mlipokea Roho Mtakatifu?” Wakajibu, “Hapana. Hatujawahi hata kusikia kuwa kuna Roho Mtakatifu.” Ndipo Paulo akawauliza, “Mlibatizwa ubatizo gani?” Wakajibu, “Ubatizo wa Yohana.” Paulo akasema, “Yohana alipobatiza, aliwaambia watu watubu dhambi na kumwamini atakayekuja baada yake, yaani, Yesu.” Waliposikia haya, wakabatizwa katika jina la Yesu. Na Paulo alipoweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akawashukia , wakasema kwa lugha mpya na kutabiri. Walikuwepo kama watu kumi na wawili.

Paulo akaingia katika sinagogi na kwa muda wa miezi mitatu akafundisha kwa ujasiri akitumia kila njia kueleza juu ya Ufalme wa Mungu. Lakini baadhi yao walipokataa kuamini na kuanza kukashifu ujumbe wake mbele ya ushirika wote, aliachana nao, akawachukua wale wanafunzi akaendelea kujadiliana nao katika ukumbi wa Tirano. 10 Aliendelea na kazi hii kwa muda wa miaka miwili mpaka wenyeji wote wa Asia wakawa wamesikia neno la Bwana,

Wana Wa Skeva Wajaribu Kutoa Pepo

11 Na Mungu alifanya miujiza mingi ya ajabu kwa mkono wa Paulo. 12 Watu wakachukua vitambaa na taulo ambazo zilikuwa zimegusa mwili wa Paulo wakawawekea wagonjwa, nao wakapona magonjwa yao na pepo wachafu wakawatoka. 13 Baadhi ya Wayahudi waliokuwa wakienda huku na huko wakiwatoa watu pepo wachafu wali jaribu nao kutumia jina la Yesu kutoa pepo, wakisema, “Nakuamuru kwa jina la Yesu, anayehubiriwa na Paulo.” 14 Palikuwa na wana saba wa kuhani mkuu aliyeitwa Skeva ambao walikuwa wakifanya hivi. 15 Lakini pepo mchafu akawajibu, “Yesu namfahamu na Paulo pia namfahamu; lakini ninyi ni nani?” 16 Yule mtu aliyekuwa na pepo mchafu akawarukia akawashambulia vikali, wakatoka ndani ya ile nyumba mbio wakiwa uchi na wenye majeraha. 17 Jambo hili likajulikana kwa wenyeji wote wa Efeso, Wayahudi kwa Wagiriki; hofu ikawajaa watu wote; na jina la Bwana likaheshimiwa. 18 Waamini wengi wakatubu matendo yao maovu hadharani. 19 Na wale waliokuwa wakishiriki uchawi na kupiga ramli wakaleta vitabu vyao na kuvichoma moto hadharani. Walipopiga hesabu ya vitabu walivyochoma walikuta kwamba thamani yake ilikuwa vipande elfu hamsini vya fedha. 20 Neno la Bwana likaenea sana na kuwa na nguvu.

Ghasia Huko Efeso

21 Baada ya mambo haya kutokea, Paulo aliongozwa na Roho kupitia Makedonia na Akaya akiwa njiani kwenda Yerusalemu. Paulo alisema, “Nikishafika Yerusalemu, ni lazima niende Rumi pia.” 22 Akatuma wasaidizi wake wawili, Timotheo na Erasto, waende Makedonia, naye akakaa Asia kwa muda kidogo zaidi. 23 Wakati huo huo pakatokea ghasia kubwa kwa sababu ya Njia ya Bwana. 24 Mtu mmoja aitwaye Demetrio mhunzi wa vinyago vya fedha alikuwa akitengeneza vihekalu vya fedha vya Artemi na kuwa patia mafundi wake biashara kubwa. 25 Yeye aliwakutanisha watu hawa pamoja na watu wengine wanaofanya kazi za kutengeneza viny ago vya miungu kama wao akawaambia, “Jamani, mnajua ya kuwa uta jiri wetu unatokana na kazi zetu. 26 Lakini mmeona na kusikia jinsi ambavyo huko Efeso na karibu Asia yote huyu Paulo amewash awishi watu na kutuharibia biashara kwa kusema kuwa miungu iliy otengenezwa na watu si miungu ya kweli. 27 Kwa hiyo kuna hatari kuwa kazi yetu itaanza kudharauliwa. Na si hivyo tu, bali hata hekalu la mungu wetu Artemi, aliye mkuu na anayeabudiwa Asia yote na ulimwengu wote, litakuwa halina maana tena na utukufu wake utaondolewa.”

28 Waliposikia maneno haya walighadhabika wakapiga kelele, “Artemi wa Waefeso ni mkuu!” 29 Mji mzima ukajaa vurugu, waka kimbilia katika ukumbi wa michezo kwa pamoja wakawakamata Gayo na Aristarko, Wamakedonia waliokuwa wakisafiri na Paulo. 30 Paulo alitaka kuingilia kati lakini wanafunzi wengine wakam zuia; 31 hata baadhi ya viongozi waliokuwa marafiki wa Paulo walituma watu wamsihi asiingie katika ule ukumbi. 32 Pakawa na kutokuelewana katika ule ukumbi kwa sababu baadhi ya watu wali kuwa wakisema jambo moja na wengine lingine. Ikawa ni fujo; wengi wa watu waliofika hawakujua ni kwa nini walikuwa wamekusanyika huko. 33 Wayahudi wakamchagua Aleksanda azungumze kwa niaba yao naye akawaashiria watu wanyamaze apate kuzungumza. 34 Lakini umati ulipogundua yakuwa yeye ni Myahudi, walipiga kelele kwa kiasi cha saa mbili wakisema, “Artemi wa Waefeso ni mkuu!” 35 Baadaye karani wa mji alipofanikiwa kuwanyamazisha, aliwahu tubia akasema, “Ndugu Waefeso, kila mtu ulimwenguni anajua ya kuwa mji wa Efeso ndio unaotunza hekalu la Artemi aliye mkuu na ile sanamu iliyoanguka kutoka angani. 36 Kwa hiyo, kwa kuwa hakuna anayeweza kukanusha mambo haya, sioni sababu ya ninyi kufanya fujo au kuchukua hatua ambazo baadaye huenda mkazijutia. 37 Kwa maana mmewaleta hawa watu wawili hapa ingawa wao hawaja fanya uharibifu wo wote kwa hekalu la Artemi au kusema maneno ya kufuru juu ya huyu mungu wetu mwanamke. 38 Kama Demetrio na mafundi wenzake wana mashtaka juu ya mtu ye yote, mahakama ziko wazi na mahakimu wapo; wachukue hatua za kisheria. 39 Lakini kama kuna mashauri mengine, itabidi mtumie baraza halali. 40 Hivi sasa tuko katika hatari ya kushtakiwa kwa kufanya fujo kwa maana hatuna sababu ya kuridhisha kuhusu mambo yaliyotokea leo.” 41 Baada ya kusema haya akavunja mkutano.

Paulo Aenda Makedonia na Ugiriki

20 Fujo zilipokwisha, Paulo aliwaita wanafunzi pamoja akawa tia moyo halafu akawaaga. Akaanza safari yake ya kwenda Makedo nia. Alipokuwa akisafiri, aliwapa waamini katika sehemu zote alizopita maneno ya kuwatia moyo, ndipo akaenda Ugiriki ambako alikaa kwa muda wa miezi mitatu. Alipokuwa akijiandaa kwenda Siria kwa meli, iligundulika kwamba Wayahudi walikuwa na mpango wa kumwua, kwa hiyo akaamua kurudi akipitia Makedonia. Watu waliofuatana naye safarini ni Sopatro Piro mwenyeji wa Beroya , Aristako na Sekundo kutoka Thesalonike, Gayo mwenyeji wa Derbe; Timotheo, Tikiko na Trofimo wenyeji wa Asia. Hawa walitutangu lia wakaenda kutungojea Troa. Sisi tuliondoka baada ya sikukuu ya mikate isiyotiwa hamira tukasafiri kwa meli na kuungana nao siku tano baadaye huko Troa ambako tulikaa kwa siku saba.

Paulo Akutana Na Waamini Wa Troa

Jioni siku ya kwanza ya Juma tulikuwa tumekutana pamoja kwa chakula na Paulo akaongea nao akiwa na mpango wa kuondoka kesho yake; akaendelea na mazungumzo mpaka usiku wa manane. Chumba cha ghorofani walipokuwa wakikutania kilikuwa na taa nyingi na kijana mmoja jina lake Eutiko alikuwa amekaa dirishani. Paulo alivyoendelea kuongea kijana huyu alizidi kusinzia. Hatimaye alishikwa na usingizi kabisa, akaanguka chini kutoka ghorofa ya tatu, akadhaniwa kuwa amekufa. 10 Lakini Paulo alishuka chini akainama, akamkumbatia yule kijana akasema, “Msiwe na hofu, yun gali hai.” 11 Paulo akarudi ghorofani na alipokwisha kula, akaongea nao tena mpaka alfajiri ndipo akaondoka. 12 Yule kijana alichukuliwa nyumbani akiwa hai na wote waliokuwepo walifarijika.

Paulo Atoka Troa Kwenda Mileto

13 Tuliingia katika meli tukasafiri mpaka Aso ambako tuli tarajia kumchukua Paulo kwa maana alikuwa amepanga kusafiri nchi kavu mpaka huko. 14 Alipotukuta huko Aso, tulimchukua melini tukasafiri wote mpaka Mitilene. 15 Kutoka Mitilene tuliendelea kwa meli na kesho yake tukafika pwani ya upande wa pili wa Kio. Siku iliyofuata tukafika Samo na kesho yake tukawasili Mileto. 16 Paulo alikuwa ameamua tusipitie Efeso ili asitumie muda mwingi katika jimbo la Asia; kwa sababu alitaka kama ikiwezekana afike Yerusalemu kabla ya siku ya Pentekoste.

Paulo Anawaaga Wazee Wa Kanisa La Efeso

17 Paulo akiwa Mileto, alituma ujumbe kwenda Efeso kuwaita wazee wa kanisa wakutane naye. 18 Walipofika aliwaambia, “Ninyi mnajua jinsi nilivyoishi nanyi tangu siku ya kwanza nilipofika Asia. 19 Nilimtumikia Bwana kwa unyenyekevu na machozi na kwa mateso yaliyotokana na njama za Wayahudi. 20 Mnajua jinsi ambavyo sikusita kuwaambia cho chote ambacho kingekuwa cha faida kwenu, na jinsi nilivyofundisha hadharani na nyumba kwa nyumba 21 nikiwashuhudia Wayahudi na Wagiriki juu ya kutubu dhambi kwa Mungu na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo. 22 Na sasa nimevutwa na Roho niende Yerusalemu na sijui mambo yatakayonipata huko. 23 Ila katika kila mji niliopitia, Roho Mtakatifu amenifunulia kwamba mbele yangu kifungo na mateso vinaningoja. 24 Lakini nay ahesabu maisha yangu kuwa si kitu cha thamani kwangu, ili mradi niweze kukamilisha wito na kazi niliyopewa na Bwana Yesu; kazi ya kuwashuhudia watu kuhusu Habari Njema ya neema ya Mungu. 25 Na sasa najua ya kuwa hakuna hata mmoja wenu, ninyi ambao kati yenu nimekuwa nikihubiri juu ya Ufalme wa Mungu, atakayeniona tena. 26 Kwa hiyo nawashuhudia wazi leo hii kwamba sina lawama juu ya mtu ye yote kati yenu, 27 kwa sababu sikuacha kuwatangazia mpango kamili wa Mungu. 28 Jilindeni nafsi zenu, na mlinde kundi lote la kondoo ambalo Roho Mtakatifu ameliweka chini ya uongozi wenu; mtunze kanisa la Mungu ambalo amelinunua kwa damu ya Mwa nae. 29 Najua kwamba nikishaondoka, mbwa mwitu wakali watakuja kati yenu nao hawatakuwa na huruma yo yote juu ya kundi lenu. 30 Na hata kati yenu ninyi patatokea watu watakaosema maneno ya kupotosha ili wawavute baadhi ya wanafunzi wawafuate. 31 Kwa hiyo muwe macho; mkumbuke jinsi nilivyomwonya kila mmoja kwa machozi usiku na mchana kwa muda wa miaka mitatu. 32 Na sasa nawakabidhi kwa Mungu na kwa neno la neema yake ambalo linaweza kuwajenga na kuwapa ninyi urithi pamoja na wote ambao wameta kaswa. 33 Sikutamani fedha au dhahabu au nguo za mtu ye yote. 34 Ninyi wenyewe mnajua kwamba kwa mikono yangu nimefanya kazi nikapata mahitaji yangu na ya wenzangu. 35 Katika kila jambo nimewaonyesha kwamba kwa kufanya kazi kwa bidii mtaweza kuwa saidia walio dhaifu, mkikumbuka maneno aliyosema Bwana Yesu kwamba, ‘Kuna baraka kubwa zaidi katika kutoa kuliko kupokea.”’

36 Paulo alipomaliza kusema haya alipiga magoti akaomba pamoja nao wote. 37 Na wote wakalia, wakamkumbatia Paulo na kum busu, 38 wakihuzunika kwa sababu ya maneno aliyowaambia kwamba hawatamwona tena. Wakamsindikiza wakamfikisha kwenye meli.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica