Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

M’Cheyne Bible Reading Plan

The classic M'Cheyne plan--read the Old Testament, New Testament, and Psalms or Gospels every day.
Duration: 365 days
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Version
Error: Book name not found: Gen for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Mathayo 20

Yesu Atumia Mfano wa Wakulima Katika Shamba la Mizabibu

20 Ufalme wa Mungu umefanana na mtu aliyemiliki shamba la mizabibu. Asubuhi mmoja akatoka kwenda kuajiri watu ili walime katika shamba lake la mizabibu. Alikubaliana nao kuwa atawalipa sarafu moja ya fedha ikiwa watafanya kazi siku ile. Kisha akawapeleka kwenye shamba la mizabibu kulima.

Ilipofika saa tatu asubuhi mtu huyo alitoka na kwenda sokoni ambako aliwaona baadhi ya watu wamesimama na hawafanyi kazi yo yote. Akawaambia, ‘Ikiwa mtakwenda kufanya kazi shambani kwangu, nitawalipa kutokana na kazi yenu.’ Hivyo walikwenda kufanya kazi kwenye shamba lake la mizabibu.

Ilipofika saa sita mchana na saa tisa alasiri alitoka tena. Na nyakati zote mbili aliwaajiri watu wengine waende kufanya kazi shambani mwake. Ilipofika saa kumi na moja alikwenda sokoni tena. Akawaona watu wengine wamesimama pale. Akawauliza, ‘Kwa nini mmesimama hapa siku nzima na hamfanyi kazi?’

Wakasema, ‘Hakuna aliyetupa kazi.’

Mwenye shamba akawaambia, ‘Basi mnaweza kwenda kufanya kazi katika shamba langu la mizabibu.’

Mwishoni mwa siku, mwenye shamba akamwambia msimamizi wa wafanyakazi wote, ‘Waite wafanyakazi na uwalipe wote. Anza kwa kulipa watu niliowaajiri mwishoni, na malizia kwa wale niliowaajiri mwanzoni.’

Wafanyakazi walioajiriwa saa kumi na moja jioni walipata malipo yao. Kila mfanyakazi alipata sarafu moja ya fedha. 10 Ndipo wafanyakazi walioajiriwa kwanza wakaja kupokea malipo yao. Walidhani wangelipwa zaidi ya wengine. Lakini kila mmoja wao alipokea sarafu moja ya fedha. 11 Walipopata sarafu ya fedha, walimlalamikia mmiliki wa shamba. 12 Walisema, ‘Watu hao walioajiriwa mwishoni wamefanya kazi saa moja tu. Lakini umewalipa sawa na sisi. Na tumefanya kazi siku nzima kwenye jua kali.’

13 Lakini mmiliki wa shamba akamwambia mmoja wao, ‘Rafiki, nimekulipa kama tulivyopatana, ulikubali kufanya kazi kwa malipo ya sarafu moja ya fedha. Sawa? 14 Hivyo chukua malipo yako na uende. Ninataka kumlipa mtu niliyemwajiri mwishoni sawa na kiasi nilichokulipa. 15 Ninaweza kufanya chochote ninachotaka na pesa yangu. Wewe unao wivu[a] na unataka kuwadhuru wengine kwa kuwa mimi ni mkarimu?’

16 Hivyo walio wa mwisho sasa watakuwa wa kwanza siku zijazo. Na walio wa kwanza sasa watakuwa wa mwisho siku zijazo.”

Yesu Azungumza Tena Kuhusu Kifo Chake

(Mk 10:32-34; Lk 18:31-34)

17 Yesu alikuwa anakwenda Yerusalemu akiwa na wafuasi wake kumi na wawili. Walipokuwa wakitembea, aliwakusanya pamoja wafuasi hao na kuzungumza nao kwa faragha. Akawaambia, 18 “Tunakwenda Yerusalemu. Mwana wa Adamu atatolewa kwa viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, nao watasema ni lazima auawe. 19 Watamkabidhi wa wageni, watakaomcheka na kumpiga kwa mijeledi, kisha watamwua kwenye msalaba. Lakini siku ya tatu baada ya kifo chake, atafufuliwa kutoka kwa wafu.”

Mama Ataka Upendeleo Maalum kwa Wanaye

(Mk 10:35-45)

20 Ndipo mke wa Zebedayo akamjia Yesu akiwa na wanaye. Akainama mbele ya Yesu na akamwomba amtendee kitu.

21 Yesu akasema, “Unataka nini?”

Akasema, “Niahidi kuwa mmoja wa wanangu atakaa upande wa kuume na mwingine wa kushoto katika ufalme wako.”

22 Hivyo Yesu akawaambia wana wa Zebedayo, “Hamwelewi mnachokiomba. Mnaweza kukinywea kikombe[b] ambacho ni lazima nikinywee?”

Wana wa Zebedayo wakajibu, “Ndiyo tunaweza!”

23 Yesu akawaambia, “Ni kweli kuwa mtakinywea kikombe nitakachokinywea. Lakini si mimi wa kuwaambia ni nani ataketi mkono wangu wa kuume au wa kushoto. Baba yangu amekwisha amua ni nani ataketi kuume au kushoto kwangu. Amekwisha andaa nafasi hizo kwa ajili yao.”

24 Wafuasi wengine kumi waliposikia hili walikasirika kwa ajili ya wale ndugu wawili. 25 Hivyo Yesu akawaita pamoja, akawaambia, “Mnajua kuwa watawala wa watu wasio Wayahudi[c] wanapenda kuonesha nguvu yao kwa watu. Na viongozi wao muhimu wanapenda kutumia mamlaka yao yote juu ya watu. 26 Lakini isiwe hivyo miongoni mwenu. Kila anayetaka kuwa kiongozi wenu lazima awe mtumishi wenu. 27 Kila anayetaka kuwa wa kwanza ni lazima awatumikie ninyi nyote kama mtumwa. 28 Fanyeni kama nilivyofanya: Mwana wa Adamu hakuja ili atumikiwe na watu. Alikuja ili awatumikie wengine na kutoa maisha yake ili kuwaokoa watu wengi.”

Yesu Awaponya Watu Wawili Wasiyeona

(Mk 10:46-52; Lk 18:35-43)

29 Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wanaondoka Yeriko, umati mkubwa wa watu ulimfuata. 30 Walikuwepo wasiyeona wawili wamekaa kando ya njia. Waliposikia kuwa Yesu anapita pale walipaza sauti wakasema, “Bwana, Mwana wa Daudi, tafadhali tusaidie!”

31 Watu waliwakemea wale wasiyeona, wakawaambia wanyamaze. Lakini waliendelea kupaza sauti zao zaidi na zaidi, “Bwana, Mwana wa Daudi, tafadhali tusaidie!”

32 Yesu alisimama na kuwaambia, “Mnataka niwafanyie nini?”

33 Wakajibu, “Bwana, tunataka tuweze kuona.”

34 Yesu aliwahurumia wale wasiyeona. Akayagusa macho yao, na mara hiyo hiyo wakaanza kuona. Wakawa wafuasi wa Yesu.

Error: Book name not found: Neh for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Matendo 20

Paulo Aenda Makedonia na Uyunani

20 Ghasia zilipokwisha, Paulo aliwaalika wafuasi wa Bwana kuja kumtembelea. Baada ya kuwatia moyo, aliwaaga na kuondoka kwenda Makedonia. Katika safari yake kupitia Makedonia alikuwa na maneno mengi ya kuwatia moyo wafuasi sehemu mbalimbali. Kisha alikwenda Uyunani na alikaa huko kwa miezi mitatu.

Alipokuwa tayari kutweka tanga kwenda Shamu, baadhi ya Wayahudi walikuwa wanapanga kitu kinyume naye. Hivyo aliamua kurudi nyuma kwenda Shamu kupitia Makedonia. Watu hawa walikuwa wanasafiri pamoja naye: Sopata, mwana wa Piro, kutoka mji wa Berea; Aristarko na Sekundo, kutoka mji wa Thesalonike; Gayo, kutoka mji wa Derbe; Timotheo; na watu wawili kutoka Asia, Tikiko na Trofimo. Watu hawa walimtangulia Paulo. Walitusubiri katika mji wa Troa. Baada ya Siku kuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu tulitweka tanga kutoka katika mji wa Filipi. Tuliwakuta watu hawa katika mji wa Troa siku tano baadaye na tulikaa pale kwa siku saba.

Paulo Atembelea Troa Mara ya Mwisho

Siku ya Jumapili[a] sote tulikusanyika pamoja kula Meza ya Bwana.[b] Paulo alizungumza na kundi. Kwa sababu alipanga kuondoka siku iliyofuata, aliendelea kuzungumza mpaka usiku wa manane. Tulikuwa wote kwenye chumba ghorofani na kulikuwa taa nyingi chumbani. Alikuwepo kijana mmoja aliyekuwa amekaa dirishani aliyeitwa Eutiko. Paulo aliendelea kuzungumza, na Eutiko alianza kuchoka na kusikia ungungizi. Mwishowe alisinzia na kuanguka. Alianguka chini, nje kutoka ghorofa ya tatu. Watu walipokwenda kumnyenyua alikuwa amekwisha kufa.

10 Paulo alishuka, akaenda mahali alipokuwa Eutiko, akapiga magoti, na akamkumbatia. Akawaambia waamini wengine, “Msiwe na hofu. Ni mzima yuko hai sasa.” 11 Kisha Paulo akapanda ghorofani, akamega baadhi ya mikate na kula. Alizungumza nao kwa muda mrefu. Alimaliza kuzungumza mapema asubuhi na akaondoka. 12 Wafuasi wa Bwana walimpeleka Eutiko nyumbani akiwa hai, walifarijika sana wote.

Safari Kutoka Troa kwenda Mileto

13 Tulimtangulia Paulo, tukatweka tanga kwenda Asso, tulipanga kumkuta huko. Alitwambia tufanye hivi kwa sababu alitaka kusafiri kwa nchi kavu. 14 Alipotukuta Asso, aliungana nasi na tulipanda meli pamoja naye, na sote tulitweka tanga kwenda Mitelene. 15 Siku iliyofuata, tulitweka tanga kutoka pale na kufika karibu na kisiwa cha Kio. Kisha siku iliyofuata tulitweka tanga kwenda kwenye kisiwa Samosi. Baada ya siku moja tukafika kwenye mji wa Mileto. 16 Paulo alikwisha amua kutosimama Efeso. Hakutaka kukaa Asia kwa muda mrefu. Alikuwa anaharakisha kwa sababu alitaka ikiwezekana awe Yerusalemu siku ya Pentekoste.

Paulo Azungumza na Wazee kutoka Efeso

17 Tukiwa Mileto Paulo alitume ujumbe kwenda Efeso, akiwaambia wazee wa kanisa la Efeso waje kwake.

18 Walipofika, Paulo akawaambia, “Mnafahamu kuhusu maisha yangu tangu siku ya kwanza nilipofika Asia. Mnafahamu namna nilivyoishi wakati wote nilipokuwa pamoja nanyi. 19 Wayahudi walipanga hila kinyume nami, na hila zao zilinisababishia matatizo mengi. Lakini mnafahamu kwamba daima nilimtumikia Bwana, nyakati zingine kwa machozi. Sikujipendelea mimi mwenyewe kwanza. 20 Daima niliwatendea mema. Niliwahubiri Habari Njema kuhusu Yesu sehemu za wazi mbele ya watu na pia nilifundisha katika nyumba zenu. 21 Nilimwambia kila mtu, Myahudi na Myunani, kubadilika na wakamgeukia Mungu. Niliwaambia wote wamwamini Bwana wetu Yesu.

22 Lakini sasa ni lazima nimtii Roho na kwenda Yerusalemu. Sifahamu nini kitanipata huko. 23 Ninafahamu kitu kimoja kwamba katika kila mji Roho Mtakatifu huniambia kwamba matatizo na hata kufungwa gerezani kunanisubiri. 24 Siujali uhai wangu mwenyewe. Jambo la muhimu zaidi ni mimi kuimaliza kazi yangu. Ninataka niimalize huduma ambayo Bwana Yesu alinipa niifanye, nayo ni kuwahubiri watu Habari Njema kuhusu neema ya Mungu.

25 Na sasa nisikilizeni. Ninafahamu kwamba hakuna mmoja wenu atakayeniona tena. Wakati wote nilipokuwa pamoja nanyi, niliwahubiri Habari Njema kuhusu ufalme wa Mungu. 26 Hivyo leo ninaweza kuwaambia kitu kimoja ambacho nina uhakika nacho: Mungu hatanilaumu ikiwa baadhi yenu hamtaokoka. 27 Ninaweza kusema hivi kwa sababu ninajua niliwaambia yote ambayo Mungu anataka mfahamu. 28 Jilindeni ninyi wenyewe pamoja na watu wote mliopewa na Mungu. Naye Roho Mtakatifu amewapa ninyi kazi ya kuwachunga[c] kondoo hawa.[d] Ni lazima muwe wachungaji wa kanisa la Mungu,[e] watu ambao Mungu aliwanunua kwa damu ya Mwanaye wa pekee.[f] 29 Ninafahamu ya kwamba nikishaondoka, baadhi ya watu watakuja kwenye kundi letu. Watakuwa kama mbwa mwitu na watajaribu kuwaangamiza kondoo. 30 Pia, watu kutoka kwenye kundi lenu wenyewe wataanza kufundisha mambo yasiyo sahihi. Watawaongoza baadhi ya wafuasi wa Bwana mbali na kweli ili wawafuate katika upotovu wao. 31 Hivyo iweni waangalifu! Na daima kumbukeni mambo niliyofanya kwa miaka mitatu nilipokuwa pamoja nanyi. Sikuacha kumkumbusha kila mmoja wenu jinsi anavyopaswa kuishi, nikiwashauri usiku na mchana na kulia kwa ajili yenu.

32 Sasa ninawaweka katika uangalizi wa Mungu. Ninategemea ujumbe wa neema yake kuwaimarisha ninyi. Ujumbe huo unaweza kuwapa ninyi baraka ambazo Mungu huwapa watakatifu wake wote. 33 Nilipokuwa pamoja nanyi, sikutamani pesa ya mtu yeyote au nguo nzuri. 34 Mnafahamu kwamba daima nilifanya kazi kwa mikono yangu mwenyewe ili nimudu mahitaji yangu mwenyewe na mahitaji ya watu waliokuwa pamoja nami. 35 Daima niliwaonesha kwamba mnapaswa kufanya kazi nilivyofanya na kuwasaidia wadhaifu. Niliwafundisha kukumbuka maneno ya Bwana Yesu aliyosema, ‘Ni baraka kuu kutoa kuliko kupokea.’”

36 Paulo alipomaliza kuzungumza, alipiga magoti chini, na wote waliomba pamoja. 37-38 Walilia sana. Kilichowahuzunisha sana ilikuwa kauli ya Paulo alipowaambia kuwa hawatamwona tena. Walimkumbatia na kumbusu. Kisha walikwenda pamoja naye mpaka kwenye meli na wakaagana naye.

Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)

© 2017 Bible League International