Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Book of Common Prayer

Daily Old and New Testament readings based on the Book of Common Prayer.
Duration: 861 days
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Version
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Deut for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
2 Wakorintho 7:2-16

Furaha ya Paulo

Fungueni mioyo yenu kwetu. Hatujamtendea vibaya wala kumwumiza mtu yeyote. Na hatujamdanganya mtu yeyote. Sisemi haya kuwalaumu. Nimekwishawaeleza kuwa tunawapenda sana kiasi kwamba hakuna chochote katika maisha ama katika kifo kitakachotutenganisha na ninyi. Ninajisikia kwamba ninaweza kuwaambia lolote. Ninajivunia sana ninyi. Licha ya matatizo yote tuliyoyapata, nimetiwa moyo sana na ninajisikia kuwa mwenye furaha sana.

Tulipokuja Makedonia, hatukupumzika. Tulisumbuliwa kwa kila namna. Tulikuwa na vita kwa nje na hofu ndani yetu. Lakini Mungu huwapa moyo wale wanaosumbuliwa, na kwa hakika na sisi alitupa moyo kwa kumleta Tito kwetu. Ilikuwa furaha kumwona, lakini tulitiwa moyo zaidi tuliposikia jinsi nanyi mlivyomtia moyo yeye pia. Naye alitueleza kuwa mlikuwa na shauku ya kuniona mimi na kwamba mnayajutia yale mlivyofanya. Na akatueleza jinsi mlivyokuwa na shauku ya kusimama upande wangu. Niliposikia hili, nilifurahishwa sana.

Hata kama barua nilyowaandikieni iliwahuzunisha, sijutii kuiandika. Nafahamu kuwa barua ile iliwatia huzuni, ninasikitika kwa hilo. Lakini iliwapa huzuni kwa muda mfupi. Sasa ninafurahi, si kwa sababu mlipata huzuni, bali kwa sababu huzuni yenu iliwasababisha mkaamua kubadilika. Hilo ndilo ambalo Mungu alilitaka, hivyo hatukuwaumiza kwa namna yo yote. 10 Aina ya huzuni ambayo Mungu anaitaka inawafanya watu waamue kubadili maisha yao. Hili linawaelekeza kwenye wokovu, nasi hatuwezi kulijutia hilo. Lakini huzuni dunia huleta mauti. 11 Mlikuwa na huzuni ambayo Mungu alitaka muwe nayo. Sasa mmetambua kile ambacho huzuni hiyo imewaletea: Imewafanya muwe makini sana. Imewafanya mtafute kuthibitisha kuwa hamkufanya makosa. Iliwafanya mkasirike na mwogope. Imewafanya muwe na shauku ya kuniona. Imewafanya muwe na azma ya kufanya kile nilichowaagiza. Imewafanya muwe na shauku ya kuona kuwa haki inatendeka. Mlithibitisha kuwa hamkuwa na hatia katika sehemu yoyote ya tatizo hilo. 12 Sababu kubwa ya kuandika barua ile haikuwa kwa sababu ya yule aliyefanya kosa au aliyeumia. Niliandika ili mtambue, mbele za Mungu, jinsi mnavyotujali sana sisi. 13 Na hili ndilo lililokuwa faraja kwetu sisi.

Tulitiwa moyo sana, lakini hasa tulifurahishwa kuona jinsi Tito alivyokuwa mwenye furaha. Ninyi nyote mlimfanya apate utulivu moyoni. 14 Nilijisifu juu yenu kwake Tito, na ninyi hamkuniaibisha. Siku zote tumewaambia ninyi kweli, na sasa yale tuliyomwambia Tito kwa habari zenu yamedhihirika kuwa ni kweli. 15 Na upendo wake kwenu una nguvu anapokumbuka kuwa mlikuwa tayari kutii. Mlimpokea kwa heshima na hofu. 16 Ninafuraha sana kwa kuwa ninaweza kuwaamini kikamilifu.

Luka 17:20-37

Kuja Kwa Ufalme Wa Mungu

(Mt 24:23-28,37-41)

20 Baadhi ya Mafarisayo walimuuliza Yesu, “Ufalme wa Mungu utakuja lini?” Yesu akajibu, “Kuja kwa ufalme wa Mungu si kitu unachoweza kuona. 21 Watu hawatasema, ‘Tazama ufalme wa Mungu uko hapa’ au ‘Ule pale!’ Hapana, Ufalme wa Mungu upo hapa pamoja nanyi.”[a]

22 Kisha Yesu akawaambia wafuasi wake, “Wakati utakuja, ambapo mtatamani angalau kuwa na Mwana wa Adamu hata kwa siku moja, lakini hamtaweza. 23 Watu watawaambia, ‘Tazameni, yuko kule!’ au ‘Tazameni, yuko hapa!’ Kaeni pale mlipo; msitoke kwenda kumtafuta. 24 Iweni na subira kwa sababu Mwana wa Adamu atakaporudi, mtatambua. Siku hiyo atang'aa kama mwanga wa radi umulikavyo angani kutoka upande mmoja hadi mwingine. 25 Lakini kwanza, ni lazima Mwana wa Adamu ateseke kwa mambo mengi na watu wa leo watamkataa.

26 Mwana wa Adamu atakaporudi, itakuwa kama ilivyokuwa Nuhu alipoishi. 27 Watu walikuwa wakila, wakinywa, wakioa na kuolewa hata siku Nuhu alipoingia katika safina. Ndipo gharika ilikuja na kuwaangamiza wote.

28 Ilikuwa vivyo hivyo katika wakati wa Lutu, Mungu alipoteketeza Sodoma. Watu wa Sodoma walikuwa wakila, wakinywa, wakinunua, wakiuza, wakipanda na kujijengea nyumba. 29 Lakini siku ambayo Lutu alitoka Sodoma, moto na baruti vilinyesha kutoka mbinguni na kuwaua wote. 30 Hivi ndivyo itakavyokuwa siku ambayo Mwana wa Adamu atarudi.

31 Siku hiyo, ikiwa mtu atakuwa juu ya paa ya nyumba yake, hatakuwa na muda wa kushuka kwenda ndani ya nyumba kuchukua vitu vyake. Ikiwa atakuwa shambani, hataweza kurudi nyumbani. 32 Kumbukeni yaliyompata mke wa Lutu![b]

33 Kila atakayejaribu kutunza maisha aliyonayo atayaangamiza. Lakini yeyote atakayeyasalimisha maisha yake atayaokoa. 34 Usiku ule watu wawili wataweza kuwa wamelala katika chumba kimoja, mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa. 35 Wanawake wawili watakuwa wanasaga nafaka pamoja, mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.” 36 [c]

37 Wafuasi wake wakamuuliza, “Hii itakuwa wapi Bwana?”

Yesu akajibu, “Ni kama kuutafuta mzoga, utaupata pale ambapo tai wamekusanyika.”

Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)

© 2017 Bible League International