Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Book of Common Prayer

Daily Old and New Testament readings based on the Book of Common Prayer.
Duration: 861 days
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Version
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Exod for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Wakolosai 3:18-4

Utu Wenu Mpya Mkiwa Nyumbani

18 Wake, muwe radhi kuwatumikia waume zetu. Ni jambo sahihi kufanya katika kumfuata Bwana.

19 Waume wapendeni wake zenu na msiwe na hasira nao.

20 Watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote. Hili humfurahisha Bwana.

21 Wababa, msiwakorofishe watoto wenu, mkiwa wagumu kupendezwa nao; wanaweza kukata tamaa.

22 Enyi watumwa, watiini mabwana zenu katika mambo yote. Mwe watii kila wakati, hata kama wao hawawezi kuwaona. Msijifanye kazi kwa bidii ili wawatendee mema. Mnapaswa kuwatumikia mabwana[a] zenu kwa moyo kwa sababu mna hofu ya Bwana. 23 Kila kazi mnayoifanya, ifanyeni kwa bidii. Fanyeni kama mnamfanyia Bwana wenu wa mbinguni, na si kama mnamfanyia bwana wa dunia hii. 24 Mnajua kwamba mtapokea kutoka kwa Bwana ujira aliowaahidi watu wake. Ndiyo, mnamtumikia Kristo aliye Bwana[b] wenu halisi. 25 Kumbukeni kuwa Mungu hana upendeleo; kila afanyaye uovu ataadhibiwa kwa sababu ya uovu wake.

Enyi mabwana, wapeni kilicho chema na chenye haki watumwa wenu. Kumbukeni kuwa Mkuu wenu yuko mbinguni.

Mambo ya Kufanya

Msiache kuomba kamwe. Iweni tayari kwa lolote kwa kuomba na kushukuru. Mtuombee na sisi pia, ili Mungu atupe fursa za kuwaeleza watu ujumbe wake. Nimefungwa kwa sababu ya hili. Lakini ombeni ili tuendelee kuwaeleza watu siri ya kweli ambayo Mungu ameiweka wazi kuhusu Kristo. Niombeeni ili niseme yanayonipasa kusema, ili niweze kuiweka wazi kweli hii kwa kila mtu.

Iweni na hekima kwa namna mnavyochukuliana pamoja na wale wasioamini. Tumieni muda wenu vizuri kadri mwezavyo. Kila mnapozungumza pamoja na walio nje ya kundi lenu, muwe wema na wenye hekima. Ndipo mtaweza kumjibu kila mtu ipasavyo.

Habari Kuhusu Wale Walio Pamoja na Paulo

Tikiko ni ndugu yangu mpendwa katika Kristo. Yeye ni msaidizi mwaminifu na anamtumikia Bwana pamoja nami. Atawaambia kila kitu kuhusu mimi. Hii ndiyo sababu ninamtuma, ninataka mfahamu hali yetu, na ninamtuma awatie moyo ninyi. Ninamtuma yeye pamoja na Onesimo, ndugu mpendwa na mwaminifu kutoka kwenye kundi lenu. Watawaeleza kila kitu kilichotokea hapa.

10 Aristarko, aliyefungwa pamoja nami humu gerezani anawasalimu. Marko, binamu yake Barnaba anawasalimu pia. (Nimekwisha kuwaambia kuhusu Marko. Ikiwa atakuja, mpokeeni.) 11 Pia pokeeni salamu toka kwa Yesu, aitwaye pia Yusto. Hawa ni Wayahudi waamini pekee wanaofanya kazi pamoja nami kwa ajili ya ufalme wa Mungu. Wamekuwa faraja kubwa sana kwangu.

12 Epafra, mtumishi mwingine wa Yesu Kristo, kutoka kwenu anawasalimu. Yeye anahangaika kwa ajili yenu kwa kuwaombea mara kwa mara, ili mkue kiroho na kupokea kila kitu ambacho Mungu anataka kwa ajili yangu. 13 Ninafahamu kwamba amefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu ninyi na kwa ajili ya watu wa Laodikia na Hierapoli. 14 Pokeeni pia salamu kutoka kwa Dema na kutoka kwa rafiki yetu mpendwa Luka ambaye ni tabibu.

15 Wasalimuni kaka na dada zetu walioko Laodikia. Msalimuni pia Nimfa na kanisa lililo katika nyumba yake. 16 Baada ya kusoma barua hii, ipelekeni katika kanisa la Laodikia, ili isomwe huko pia. Ninyi nanyi msome barua niliyowaandikia wao. 17 Mwambieni Arkipo hivi, “Hakikisha unaifanya kazi aliyokupa Bwana.”

18 Hii ni salamu yangu ambayo nimeiandika kwa mkono wangu mwenyewe: Paulo. Msiache kunikumbuka nikiwa hapa gerezani. Ninawaombea neema ya Mungu iwe pamoja nanyi nyote.

Mathayo 5:1-10

Mafundisho ya Yesu Mlimani

(Lk 6:20-23)

Yesu alipoyaona makundi ya watu, alipanda kwenye kilima na kukaa chini. Wanafunzi wake walimjia Yesu. Kisha Yesu akaanza kuwafundisha watu kwa akasema:

“Heri[a] kwa walio maskini na wenye kujua kwamba wanamhitaji Mungu.[b]
    Kwa kuwa ufalme wa Mungu ni wao.
Heri kwa wenye huzuni sasa.
    Kwa kuwa watafarijiwa na Mungu.
Heri kwa walio wapole.
    Kwa kuwa watairithi nchi.[c]
Heri kwa wenye kiu na njaa ya kutenda haki.[d]
    Kwa kuwa Mungu ataikidhi kiu na njaa yao.
Heri kwa wanaowahurumia wengine.
    Kwa kuwa watahurumiwa pia.
Heri kwa wenye moyo safi,[e]
    Kwa kuwa watamwona Mungu.
Heri kwa wanaotafuta amani.[f]
    Kwa kuwa wataitwa watoto wa Mungu.
10 Heri kwa wanaoteswa kwa sababu ya kutenda haki.
    Kwa kuwa ufalme wa Mungu ni wao.

Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)

© 2017 Bible League International