Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Revised Common Lectionary (Semicontinuous)

Daily Bible readings that follow the church liturgical year, with sequential stories told across multiple weeks.
Duration: 1245 days
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Version
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Josh for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
1 Wakorintho 11:27-34

27 Hivyo, ukiula mkate na kukinywea kikombe cha Bwana isivyostahili, unautendea dhambi mwili na damu ya Bwana. 28 Unapaswa kujichunguza mwenendo wako kabla ya kula mkate na kunywa kikombe. 29 Ukila na kunywa bila kuwajali wale ambao ndiyo mwili wa Bwana, kula na kunywa kwako kutasababisha uhukumiwe kuwa mwenye hatia. 30 Ndiyo sababu watu wengi katika kanisa lenu ni wagonjwa na dhaifu, na wengi wameshakufa. 31 Lakini ikiwa tungejichunguza kwa usahihi, Mungu asingetuhukumu. 32 Lakini Bwana anapotuhukumu, anatuadhibu ili kutuonesha njia sahihi. Hufanya hivi ili tusishutumiwe kuwa wakosa na tukahukumiwa pamoja na ulimwengu.

33 Hivyo ndugu zangu, mnapokusanyika pamoja ili mle, subirianeni na mkaribishane kwa moyo wa upendo. 34 Ikiwa mtu yeyote anawaza kuhusu njaa yake mwenyewe, basi akae nyumbani kwake na ale huko! Fanyeni hivi ili kukutanika kwenu kusilete hukumu ya Mungu juu yenu. Nitakapokuja nitawaambia nini cha kufanya kuhusu masuala mengine.

Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)

© 2017 Bible League International