Revised Common Lectionary (Semicontinuous)
Ujumbe Wangu: Yesu Kristo Msalabani
2 Wapendwa kaka na dada zangu katika Kristo, nilipokuja kwenu, niliwaambia siri ya kweli iliyofunuliwa na Mungu. Lakini sikuja kama mtu mwenye uwezo mkubwa wa kuongea au mwenye hekima ya juu. 2 Nilipokuwa pamoja nanyi, niliamua kusahau kila kitu isipokuwa Yesu Kristo na kifo chake msalabani. 3 Nilipokuja kwenu nilikuwa mdhaifu na mwenye hofu. 4 Mafundisho na kuzungumza kwangu hakukuwa kwa maneno yenye hila. Lakini uthibitisho wa mafundisho yangu ilikuwa nguvu inayotolewa na Roho. 5 Nilifanya hivi ili imani yenu iwe katika nguvu ya Mungu siyo katika hekima ya kibinadamu.
Hekima ya Mungu
6 Tunafundisha hekima kwa watu ambao macho yao yamefunguliwa ili waione hekima ya siri ya Mungu. Si hekima ya watawala wa ulimwengu huu wanaobatilika. 7 Tunaisema hekima ya Mungu katika namna ambayo baadhi wanaweza kuiona na wengine hawawezi. Ni hekima iliyofichwa mpaka wakati huu na Mungu aliipanga hekima hii kabla ya kuumba ulimwengu, kwa ajili ya utukufu wetu. 8 Hakuna mtawala yeyote wa ulimwengu huu aliyeielewa hekima hii. Ikiwa wangeielewa, wasingemwua Bwana wetu mkuu na mwenye utukufu mwingi msalabani. 9 Lakini kama Maandiko yanavyosema,
“Hakuna aliyewahi kuona,
hakuna aliyewahi kusikia,
hakuna aliyewahi kufikiri
kuhusu kile ambacho Mungu amewaandalia wanaompenda.”(A)
10 Lakini Mungu ametuonesha mambo haya kupitia Roho.
Roho anaweza kuchunguza mambo yote. Anajua hata siri za ndani kabisa za Mungu.
© 2017 Bible League International