Revised Common Lectionary (Semicontinuous)
Kristo Akawa Kama Watu Ili Awaokoe
5 Mungu hakuwachagua malaika wawe watawala juu ya ulimwengu mpya unaokuja. Ulimwengu huo ujao ni ndiyo ambao tumekuwa tukiuzungumzia. 6 Imeandikwa mahali fulani katika Maandiko:
“Kwa nini watu ni muhimu sana kwako?
Kwa nini hata unafikiri juu yao?
Kwa nini unamjali mwana wa mwanadamu?[a]
Je, yeye ni muhimu kiasi hicho?
7 Kwa muda mfupi ulimfanya awe chini kuliko malaika.
Ukamvisha taji yenye utukufu na heshima.
8 Ukaweka kila kitu chini ya udhibiti wake.”[b](A)
Kama Mungu aliweka vitu vyote chini ya udhibiti wake, basi hakikuwepo chochote kilichoachwa ambacho hakukitawala. Lakini bado hatujamwona akitawala juu ya vyote. 9 Kwa kipindi kifupi Yesu aliwekwa chini kuliko malaika, lakini sasa tunamwona akiwa amevaa taji ya utukufu na heshima kwa sababu aliteseka na kufa. Kwa sababu ya neema ya Mungu, Yesu alikufa kwa ajili ya kila mmoja.
© 2017 Bible League International