Revised Common Lectionary (Complementary)
14 Neno akafanyika kuwa mwanadamu
na akaishi pamoja nasi.
Tuliouna ukuu wa uungu wake;
utukufu alionao Mwana pekee wa Baba.
15 Yohana alizungumza kuhusu yeye alipopaza sauti na kusema, “Huyu ndiye niliyemzungumzia habari zake niliposema, ‘Anayekuja baada yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa sababu alikuwepo mwanzoni, zamani kabla sijazaliwa.’”
16 Alikuwa amejaa neema na kweli ya Mungu,
tulipokea kutoka baraka moja
baada ya nyingine[a] kutoka kwake.
17 Hiyo ni kusema kuwa,
sheria ililetwa kwetu kupitia Musa.
Lakini neema na kweli imekuja
kupitia Yesu Kristo.
18 Hakuna aliyewahi kumwona Mungu
isipokuwa Mwana peke yake,
ambaye yeye mwenyewe ni Mungu,
ametuonesha jinsi Mungu alivyo.
Yuko karibu sana na Baba
kiasi kwamba tunapomwona,
tumemwona Mungu.
© 2017 Bible League International