Revised Common Lectionary (Complementary)
Malaika Wenye Mapigo ya Mwisho
15 Ndipo nikaona ajabu nyingine mbinguni, ilikuwa kubwa na ya kushangaza. Walikuwepo malaika saba wenye mapigo saba. Haya ni mapigo ya mwisho kwa sababu baada ya haya, ghadhabu ya Mungu itakuwa imekwisha.
2 Niliona kama bahari ya kioo iliyochanganyikana na moto. Wale wote waliomshinda mnyama na sanamu yake na namba ya jina lake walikuwa wamesimama kando ya bahari. Watu hawa walikuwa na vinubi walivyopewa na Mungu. 3 Waliuimba wimbo wa Musa, mtumishi wa Mungu na wimbo wa Mwanakondoo:
“Mambo unayotenda ni makuu na ya kushangaza,
Bwana Mungu Mwenye Nguvu.
Njia zako ni sahihi na za kweli,
mtawala wa mataifa.
4 Watu wote watakucha wewe, Ee Bwana.
Watu wote watalisifu jina lako.
Mtakatifu ni wewe peke yako.
Watu wote watakuja na kusujudu mbele yako,
kwa sababu ni dhahiri kuwa wewe hutenda yaliyo haki.”
© 2017 Bible League International