Book of Common Prayer
Kristo Akawa Kama Watu Ili Awaokoe
5 Mungu hakuwachagua malaika wawe watawala juu ya ulimwengu mpya unaokuja. Ulimwengu huo ujao ni ndiyo ambao tumekuwa tukiuzungumzia. 6 Imeandikwa mahali fulani katika Maandiko:
“Kwa nini watu ni muhimu sana kwako?
Kwa nini hata unafikiri juu yao?
Kwa nini unamjali mwana wa mwanadamu?[a]
Je, yeye ni muhimu kiasi hicho?
7 Kwa muda mfupi ulimfanya awe chini kuliko malaika.
Ukamvisha taji yenye utukufu na heshima.
8 Ukaweka kila kitu chini ya udhibiti wake.”[b](A)
Kama Mungu aliweka vitu vyote chini ya udhibiti wake, basi hakikuwepo chochote kilichoachwa ambacho hakukitawala. Lakini bado hatujamwona akitawala juu ya vyote. 9 Kwa kipindi kifupi Yesu aliwekwa chini kuliko malaika, lakini sasa tunamwona akiwa amevaa taji ya utukufu na heshima kwa sababu aliteseka na kufa. Kwa sababu ya neema ya Mungu, Yesu alikufa kwa ajili ya kila mmoja.
10 Mungu aliyeumba vitu vyote na ambaye kwa utukufu wake vitu vyote vipo; alitaka watu wengi wawe watoto wake na kuushiriki utukufu wake. Hivyo alifanya yale aliyohitaji kuyafanya. Alimkamilisha yeye anayewaongoza watu hao kuuelekea wokovu. Kwa njia ya mateso yake Mungu alimfanya Yesu kuwa Mwokozi mkamilifu.
9 Nuru ya kweli,
anayeleta mwangaza kwa watu wote,
alikuwa tayari kuonekana kwa ulimwengu.
10 Huyo Neno alikuwapo tayari ulimwenguni.
Ulimwengu uliumbwa kupitia yeye,
lakini ulimwengu haukumkubali.
11 Alikuja kwa ulimwengu ulio wake,
na watu wake mwenyewe hawakumkubali.
12 Lakini baadhi ya watu walimkubali wakamwamini
na akawapa haki ya kuwa watoto wa Mungu.
13 Ndiyo, walikuwa watoto wa Mungu,
lakini si kwa kuzaliwa kimwili.
Haikuhusisha matamanio
ya kibinadamu.
Mungu mwenyewe aliwafanya
kuwa watoto wake.
14 Neno akafanyika kuwa mwanadamu
na akaishi pamoja nasi.
Tuliouna ukuu wa uungu wake;
utukufu alionao Mwana pekee wa Baba.
© 2017 Bible League International