Revised Common Lectionary (Semicontinuous)
Endeleeni na Ujasiri na Uvumilivu Mlionao
32 Zikumbukeni siku za kwanza mlipojifunza kweli. Mlikuwa na mashindano magumu pamoja na mateso mengi, lakini mkaendelea kuwa imara. 33 Mara zingine watu waliwasemea mambo ya chuki na kuwatesa hadharani. Na nyakati zingine mliwasaidia wengine waliokuwa wakitendewa vivyo hivyo. 34 Ndiyo, mliwasaidia magerezani na kushiriki katika mateso yao. Na bado mlikuwa na furaha wakati kila kitu mlichokimiliki kilipochukuliwa kutoka kwenu. Mkaendelea kufurahi, kwa sababu mlijua kwamba mnacho kitu kilicho bora zaidi; kitu kitakachoendelea milele.
35 Hivyo msipoteze ujasiri mliokuwa nao zamani. Ujasiri wenu utalipwa sana. 36 Mnahitajika kuwa na subira. Baada ya kufanya yale anayotaka Mungu, mtapata aliyowaahidi.
37 “Karibu sana sasa, yeye ajaye
atakuja wala hatachelewa.
38 Mtu aliye sahihi mbele zangu
ataishi akiniamini mimi.
Lakini sitafurahishwa na yule
anayegeuka nyuma kwa ajili ya woga.”(A)
39 Lakini sisi siyo wale wanaogeuka nyuma na kuangamia. Hapana, sisi ni watu walio na imani na tunaokolewa.
© 2017 Bible League International