Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Revised Common Lectionary (Semicontinuous)

Daily Bible readings that follow the church liturgical year, with sequential stories told across multiple weeks.
Duration: 1245 days
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Version
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Isa for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Waebrania 10:32-39

Endeleeni na Ujasiri na Uvumilivu Mlionao

32 Zikumbukeni siku za kwanza mlipojifunza kweli. Mlikuwa na mashindano magumu pamoja na mateso mengi, lakini mkaendelea kuwa imara. 33 Mara zingine watu waliwasemea mambo ya chuki na kuwatesa hadharani. Na nyakati zingine mliwasaidia wengine waliokuwa wakitendewa vivyo hivyo. 34 Ndiyo, mliwasaidia magerezani na kushiriki katika mateso yao. Na bado mlikuwa na furaha wakati kila kitu mlichokimiliki kilipochukuliwa kutoka kwenu. Mkaendelea kufurahi, kwa sababu mlijua kwamba mnacho kitu kilicho bora zaidi; kitu kitakachoendelea milele.

35 Hivyo msipoteze ujasiri mliokuwa nao zamani. Ujasiri wenu utalipwa sana. 36 Mnahitajika kuwa na subira. Baada ya kufanya yale anayotaka Mungu, mtapata aliyowaahidi.

37 “Karibu sana sasa, yeye ajaye
    atakuja wala hatachelewa.
38 Mtu aliye sahihi mbele zangu
    ataishi akiniamini mimi.
Lakini sitafurahishwa na yule
    anayegeuka nyuma kwa ajili ya woga.”(A)

39 Lakini sisi siyo wale wanaogeuka nyuma na kuangamia. Hapana, sisi ni watu walio na imani na tunaokolewa.

Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)

© 2017 Bible League International