Revised Common Lectionary (Semicontinuous)
23 Paulo na Wayahudi walichagua siku kwa ajili ya mkutano. Siku hiyo Wayahudi wengi walikutana na Paulo katika nyumba yake. Aliwaambia kwa siku nzima, akawafafanulia kuhusu ufalme wa Mungu. Alitumia Sheria ya Musa na maandishi ya manabii kuwashawishi kumwamini Yesu. 24 Baadhi ya Wayahudi waliamini alichosema, lakini wengine hawakuamini. 25 Walibishana wao wenyewe na wakaanza kuondoka. Lakini aliwaambia kitu kimoja zaidi: “Roho Mtakatifu aliwaambia ukweli baba zenu kupitia nabii Isaya, aliposema,
26 ‘Nenda kwa watu hawa na uwaambie:
Mtasikiliza na kusikiliza,
lakini hamtaelewa.
Mtatazama na kutazama,
lakini hakika hamtaona.
27 Watu hawa hawawezi kuelewa.
Masikio yao yamezibwa.
Na macho yao yamefumbwa.
Hivyo hawawezi kuona kwa macho yao,
au kusikia kwa masikio yao;
au kuelewa kwa akili zao;
au kuelewa kwa akili zao.
Ikiwa wangeelewa, wangeweza kunirudia,
na ningewaponya.’(A)
28 Ninataka ninyi Wayahudi mjue kuwa Mungu ameupeleka wokovu wake kwa watu wasio Wayahudi. Watasikia!” 29 [a]
30 Paulo alikaa katika nyumba yake mwenyewe aliyopanga kwa miaka miwili kamili. Aliwakaribisha watu wote waliokuja kumtembelea. 31 Aliwaambia kuhusu ufalme wa Mungu na kuwafundisha kuhusu Bwana Yesu Kristo. Alikuwa na ujasiri sana, na hakuna aliyejaribu kumzuia asizungumze.
© 2017 Bible League International