Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Revised Common Lectionary (Semicontinuous)

Daily Bible readings that follow the church liturgical year, with sequential stories told across multiple weeks.
Duration: 1245 days
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Version
Luka 1:68-79

68 “Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli,
    kwa kuwa amekuja kuwasaidia
    watu wake na kuwaweka huru.
69 Na ametuletea sisi Mwokozi Mwenye Nguvu,
    kutoka katika ukoo wa mtumishi wake Daudi.
70 Hivi ndivyo alivyoahidi
    kupitia manabii wake watakatifu tangu zamani.
71 Aliahidi kwa Agano kuwa atatuokoa na adui zetu
    na milki za wote wanaotuchukia.
72 Ili kuonesha rehema kwa baba zetu,
    na kulikumbuka agano lake takatifu aliloagana nao.
73 Agano hili ni kiapo alichomwapia
    baba yetu Ibrahimu.
74 Alipoahidi kutuokoa kutoka katika nguvu za adui zetu,
    ili tuweze kumwabudu Yeye bila hofu.
75 Katika namna iliyo takatifu na yenye haki
    mbele zake siku zote za maisha yetu.

76 Sasa wewe, mtoto mdogo,
    utaitwa nabii wa Mungu Aliye Juu Sana,
kwa sababu utamtangulia Bwana
    kuandaa njia yake.
77 Utawaambia watu wake kwamba wataokolewa
    kwa kusamehewa dhambi zao.

78 Kwa rehema ya upendo wa Mungu wetu,
    siku mpya[a] itachomoza juu yetu kutoka mbinguni.
79 Kuwaangazia wale wanaoishi katika giza,
    kwa hofu ya mauti,
na kuongoza hatua zetu
    katika njia ya amani.”

Error: Book name not found: Mal for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Wafilipi 1:12-18

Matatizo Ya Paulo Yesaidia Kazi ya Bwana

12 Ndugu zangu, ninataka mjue kwamba yote yaliyonipata yamesaidia katika kusambaza Habari Njema, ingawa ninyi mnaweza kuwa mlitarajia kinyume chake. 13 Walinzi wote wa Kirumi na wengine wote hapa wanafahamu kuwa nimefungwa kwa sababu ninamtumikia Kristo. 14 Kufungwa kwangu gerezani kumesababisha waamini walio wengi hapa kuweka tumaini lao kwa Bwana, na kuhubiri ujumbe wa Mungu kwa ujasiri mwingi pasipo woga.

15 Baadhi ya watu wanahubiri ujumbe wa Kristo kwa sababu wananionea wivu na wanataka watu wawafuate wao badala yangu. Wengine wanahubiri kwa sababu wanataka kusaidia. 16 Wanahubiri kwa sababu ya upendo. Wanafahamu kuwa Mungu ameniweka humu gerezani ili kuitetea Habari Njema. 17 Lakini wengine wanahubiri kuhusu Kristo kwa sababu wanataka kujikweza wenyewe. Chachu yao si safi. Wanafanya hivi kwa kudhani kuwa itanisababishia uchungu mwingi niwapo gerezani. 18 Lakini hiyo haijalishi. Kitu cha muhimu ni kuwa wanawahubiri watu kuhusu Kristo, wakiwa na chachu safi au isiyo safi. Ninafurahi wanafanya hivyo.

Nitaendelea kufurahi,

Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)

© 2017 Bible League International