Revised Common Lectionary (Semicontinuous)
12 Ninawaandikia, ninyi watoto wapendwa,
kwa sababu dhambi zenu zimesamehewa kwa njia ya Kristo.
13 Ninawaandikia, ninyi akina baba,
kwa sababu mnamjua yeye aliyekuwepo tangu mwanzo.
Ninawaandikia, ninyi vijana,
kwa sababu mmemshinda yule mwovu.
14 Ninawaandikia ninyi watoto,
kwa sababu mnamjua Baba.
Ninawaandikia ninyi, akina baba,
kwa sababu mnamfahamu yeye aliyekuwepo tangu mwanzo.
Ninawaandikia ninyi, vijana,
kwa sababu mna nguvu.
Mafundisho ya Neno la Mungu yimo ndani yenu,
na mmemshinda yule mwovu.
15 Msiipende dunia hii ya uovu wala mambo yaliyomo ndani yake. Kama mkiipenda dunia, upendo wa baba haumo ndani yenu. 16 Yote yaliyomo katika dunia: yaani, tamaa halisi za kibinadamu, tamaa kwa yale mabaya tunayoyaona, na kiburi cha vitu tulivyonavyo. Lakini hakuna hata mojawapo ya haya litokalo kwa Baba. Yote yanatoka katika dunia. 17 Dunia inapita, na mambo yote ambayo watu wanayataka kutoka katika dunia nayo yanapita. Lakini yeyote atendaye mambo ambayo Mungu anayataka ataishi milele.
© 2017 Bible League International