Revised Common Lectionary (Complementary)
Kuteseka kwa kutenda haki
8 Hivyo ninyi nyote mnapaswa kuishi pamoja kwa amani. Mjitahidi kuelewana ninyi wenyewe. Mpendane kama kaka na dada na muwe wanyenyekevu na wema. 9 Msimfanyie uovu mtu yeyote ili kulipa kisasi kwa uovu aliowatendea. Msimtukane mtu yeyote ili kulipiza matusi aliyowatukana. Lakini mwombeni Mungu awabariki watu hao. Fanyeni hivyo kwa sababu ninyi wenyewe mliteuliwa kupokea baraka, 10 Maandiko yanasema:
“Anayetaka kufurahia maisha ya kweli
na kuwa na siku nyingi njema tu,
aepuke kusema chochote kinachoumiza,
na asiruhusu uongo utoke kwenye kinywa yake.
11 Aache kutenda uovu, na atende mema.
Atafute amani, na fanya kila analoweza ili kuwasaidia watu kuishi kwa amani.
12 Bwana huwaangalia wale watendao haki,
na husikia maombi yao.
Lakini yu kinyume cha wale watendao uovu.”(A)
© 2017 Bible League International