Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Book of Common Prayer

Daily Old and New Testament readings based on the Book of Common Prayer.
Duration: 861 days
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Version
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Sir for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Sir for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Waefeso 4:1-16

Umoja wa Mwili wa Kristo

Hivyo, mimi niliye mfungwa kwa ajili ya Bwana nawasihi mwishi kwa jinsi inavyowapasa watu wa Mungu, kwa sababu aliwachagua muwe wake. Iweni wanyenyekevu na wapole siku zote. Mvumiliane na kuchukuliana ninyi kwa ninyi katika upendo. Mmeunganishwa pamoja kwa amani na Roho. Jitahidini mwezavyo kudumu kuutunza umoja huo, mkiunganishwa pamoja kwa amani. Kuna mwili mmoja na Roho moja, na Mungu aliwachagua ili muwe na tumaini moja. Kuna Bwana mmoja, imani moja, na ubatizo mmoja. Mungu ni mmoja na ni Baba wetu sote, anayetawala juu ya kila mtu. Hutenda kazi kupitia kwetu sote na ndani yetu sote.

Kristo alimpa kila mmoja wetu karama. Kila mmoja alipokea kwa jinsi alivyopenda yeye kuwapa. Ndiyo maana Maandiko yanasema,

“Alipaa kwenda mahali pa juu sana;
    aliwachukua wafungwa pamoja naye,
    na akawapa watu vipawa.”(A)

Inaposema, “Alipaa juu,” inamaanisha nini? Inamaanisha kuwa kwanza alikuja chini duniani. 10 Hivyo Kristo alishuka chini, na ndiye aliyekwenda juu. Alikwenda juu ya mbingu za juu zaidi ili avijaze vitu vyote pamoja naye. 11 Na Kristo huyo huyo aliwapa watu hawa vipawa: aliwafanya wengine kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine kwenda na kuhubiri Habari Njema, na wengine kuwa wachungaji[a] ili wawafundishe watu wa Mungu. 12 Mungu aliwapa hao ili kuwaandaa watakatifu wa Mungu kwa ajili ya kazi ya huduma, kuufanya imara mwili wa Kristo. 13 Kazi hii inabidi iendelee hadi wote tutakapounganishwa pamoja katika lile tunaloliamini na tunalolijua kuhusu Mwana wa Mungu. Lengo letu ni kufanana na mtu mzima aliyekomaa na kuwa kama Kristo tukiufikia ukamilifu wake wote.

14 Ndipo tutakapokuwa si kama watoto wachanga. Hatutakuwa watu ambao nyakati zote hubadilika kama meli inayochukuliwa na mawimbi huku na kule. Hatutaweza kuathiriwa na fundisho lolote jipya tutakalosikia kutoka kwa watu wanaojaribu kutudanganya. Hao ni wale wanaoweka mipango ya ujanja na kutumia kila aina ya mbinu kuwadanganya wengine waifuate njia iliyopotoka. 15 Hapana, tunapaswa kusema ukweli kwa upendo. Tutakua na kuwa kama Kristo katika kila njia. Yeye ni kichwa, 16 na mwili wote unamtegemea yeye. Viungo vyote vya mwili vimeunganishwa na kushikanishwa pamoja, huku kila kiungo kikitenda kazi yake. Hili huufanya mwili wote ukue na kujengeka katika upendo.

Yohana 1:1-18

Yesu ni Neno la Mungu la Milele

Mwanzoni Kabla ulimwengu haujaumbwa
    alikuwepo Neno.[a]
Huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu,
    na Neno alikuwa Mungu.
Alikuwepo pamoja na Mungu
    toka mwanzo.
Kila kitu kilifanyika kupitia kwake.
    Hakuna chochote katika uumbaji wa Mungu
    kilichofanyika bila yeye.
Ndani yake Neno kulikuwemo na uzima,
    na uzima huo ulikuwa nuru
    kwa ajili ya watu wa ulimwenguni.
Nuru[b] hiyo yamulika gizani,
    na giza halikuishinda.[c]

Alikuwepo mtu aliyeitwa Yohana, aliyetumwa na Mungu. Alikuja kuwaambia watu kuhusu nuru. Ili kupitia kwake watu wote waweze kusikia kuhusu yule aliye nuru na wamwamini. Yohana mwenyewe hakuwa nuru. Lakini alikuja kuwaambia watu kuhusu nuru.

Nuru ya kweli,
    anayeleta mwangaza kwa watu wote,
    alikuwa tayari kuonekana kwa ulimwengu.
10 Huyo Neno alikuwapo tayari ulimwenguni.
    Ulimwengu uliumbwa kupitia yeye,
    lakini ulimwengu haukumkubali.
11 Alikuja kwa ulimwengu ulio wake,
    na watu wake mwenyewe hawakumkubali.
12 Lakini baadhi ya watu walimkubali wakamwamini
    na akawapa haki ya kuwa watoto wa Mungu.
13 Ndiyo, walikuwa watoto wa Mungu,
    lakini si kwa kuzaliwa kimwili.
Haikuhusisha matamanio
    ya kibinadamu.
Mungu mwenyewe aliwafanya
    kuwa watoto wake.
14 Neno akafanyika kuwa mwanadamu
    na akaishi pamoja nasi.
Tuliouna ukuu wa uungu wake;
    utukufu alionao Mwana pekee wa Baba.

15 Yohana alizungumza kuhusu yeye alipopaza sauti na kusema, “Huyu ndiye niliyemzungumzia habari zake niliposema, ‘Anayekuja baada yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa sababu alikuwepo mwanzoni, zamani kabla sijazaliwa.’”

16 Alikuwa amejaa neema na kweli ya Mungu,
    tulipokea kutoka baraka moja
    baada ya nyingine[d] kutoka kwake.
17 Hiyo ni kusema kuwa,
    sheria ililetwa kwetu kupitia Musa.
Lakini neema na kweli imekuja
    kupitia Yesu Kristo.
18 Hakuna aliyewahi kumwona Mungu
    isipokuwa Mwana peke yake,
ambaye yeye mwenyewe ni Mungu,
    ametuonesha jinsi Mungu alivyo.
Yuko karibu sana na Baba
    kiasi kwamba tunapomwona,
    tumemwona Mungu.

Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)

© 2017 Bible League International