Revised Common Lectionary (Complementary)
Paulo Akiwa Efeso
19 Apolo alipokuwa katika mji wa Korintho, Paulo alikuwa anatembelea baadhi ya sehemu akiwa njiani kwenda Efeso. Alipofika Efeso waliwakuta baadhi ya wafuasi wa Bwana. 2 Akawauliza, “Mlimpokea Roho Mtakatifu mlipoamini?”
Wafuasi hao wakamwambia, “Hatujawahi hata kusikia kuhusu Roho Mtakatifu!”
3 Paulo akawauliza, “Kwa hiyo ni mlibatizwa kwa ubatizo gani?”
Wakasema, “Kwa ubatizo aliofundisha Yohana.”
4 Paulo akasema, “Yohana aliwaambia watu wabatizwe kuonesha kuwa walidhamiria kubadili maisha yao. Aliwaambia watu kuamini katika yule atakaye kuja baada yake, naye huyo ni Yesu.”
5 Wafuasi hawa waliposikia hili, wakabatizwa katika jina la Bwana Yesu. 6 Kisha Paulo akawawekea mikono, na Roho Mtakatifu akaja juu yao. Wakaanza kuzungumza na kutabiri katika lugha tofauti. 7 Walikuwepo wanaume kama kumi na mbili katika kundi hili.
8 Paulo akaingia katika sinagogi na akazungumza kwa ujasiri. Aliendelea kufanya hivi kwa miezi mitatu. Alizungumza na Wayahudi, akijaribu kuwashawishi kukubali alichokuwa anawaambia kuhusu ufalme wa Mungu. 9 Lakini baadhi yao wakawa wakaidi, wakakataa kuamini. Waliikashifu Njia[a] ya Bwana mbele ya kila mtu. Hivyo Paulo aliwaacha Wayahudi hawa na kuwachukua wafuasi wa Bwana pamoja naye. Alikwenda mahali ambapo mtu aitwaye Tirano alikuwa na shule. Hapo Paulo alizungumza na watu kila siku. 10 Alifanya hivi kwa miaka miwili na kila mtu aliyeishi Asia, Wayahudi na Wayunani alilisikia neno la Bwana.
© 2017 Bible League International