Print Page Options Listen to Luke 4-5
Previous Prev Day Next DayNext

Beginning

Read the Bible from start to finish, from Genesis to Revelation.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Luka 4-5

Yesu Ajaribiwa Na Shetani

Kisha Yesu, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akarudi kutoka Yordani akaongozwa hadi jangwani. Alikaa huko jangwani siku arobaini akijaribiwa na shetani. Siku zote hizo hakula cho chote , kwa hiyo baada ya muda huo aliona njaa.

Shetani akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”

Yesu akamjibu, “Imeandikwa katika maandiko, ‘mtu haishi kwa chakula tu.’ ”

Kisha shetani akamchukua hadi juu ya mlima mrefu akamwo nyesha kwa mara moja milki zote za dunia. 6-7 Akamwambia, “Uki piga magoti na kuniabudu, nitakupa uwezo juu ya milki zote hizi na fahari yake; maana ni zangu na ninaweza kumpa ye yote nita kaye.” Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na kumtumikia yeye peke yake.’ ”

9-11 Ndipo shetani akamfikisha Yerusalemu, akampand isha juu ya mnara wa Hekalu, akamwambia: “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kwani imeandikwa, ‘Mungu ataamrisha mal aika wake wakulinde

12 Yesu akamwambia, “Pia imeandikwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’ ”

Mungu wako.’ ”

13 Basi Shetani alipomaliza majaribu yote, akamwacha Yesu kwa muda.

Yesu Ahubiri Galilaya

14 Kisha Yesu akarudi Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu. Habari zake zikaenea katika sehemu zote za wilaya ile. 15 Alifundisha katika masinagogi yao na wote wakamsifu.

Yesu Akataliwa Na Watu Wa Nazareti

16 Baadaye Yesu akaenda Nazareti, mahali alipokulia. Siku ya sabato alikwenda katika sinagogi kama kawaida yake. Akasimama ili asome Maandiko. 17 Akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifun gua mahali palipoandikwa: 18-19 “Roho wa Bwana yu juu yangu. Amenichagua kuwahubiria maskini Habari Njema. Amenituma kuwatan gazia wafungwa kuwa wako huru, kuwaambia vipofu kuwa wanaweza kuona tena; na kuwaweka huru wanaoonewa, na nitangaze mwaka ambao Bwana atawabariki watu wake.” 20 Akakifunga kitabu, akamrud ishia mtumishi, akaketi; na watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho. 21 Ndipo akasema: “Maandiko haya mliyosikia nikisoma, leo yametimia.”

22 Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake mazuri, wakaulizana, “Je, huyu si yule mtoto wa Yusufu?” 23 Lakini akawajibu, “Bila shaka mtaniambia, ‘Daktari, jiponye! Mbona hutendi hapa kijijini kwako miujiza tuliyosikia kuwa umeifanya kule Kapernaumu?’ 24 Ningependa mfahamu ya kwamba hakuna nabii anayekubaliwa na watu kijijini kwake. 25 Nawahakik ishieni kwamba walikuwepo wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mvua ilipoacha kunyesha kwa miaka mitatu na nusu, pakawepo na njaa kuu nchi nzima. 26 Lakini Eliya hakutumwa kumwokoa hata mmojawapo wa hawa wajane, isipokuwa alitumwa kwa mjane mmoja wa kijiji cha Sarepta katika nchi ya Sidoni. 27 Na pia wakati wa nabii Elisha, walikuwepo wakoma wengi katika Israeli; lakini hakumtakasa hata mmoja wao, ila Naamani ambaye alikuwa raia wa Siria.”

Siria.”

28 Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, waka kasirika sana. 29 Wakasimama wote wakamtoa nje ya mji hadi kwe nye kilele cha mlima ambapo mji huo ulijengwa ili wamtupe chini kwenye mteremko mkali. 30 Lakini yeye akapita katikati yao akaenda zake. Yesu Afukuza Pepo Mchafu

31 Kisha akaenda Kapernaumu, mji ulioko wilaya ya Galilaya, na siku ya sabato akawafundisha watu katika sinagogi. 32 Walis taajabishwa na mafundisho yake, maana maneno yake yalikuwa na mamlaka. 33 Alikuwepo mtu mmoja katika sinagogi aliyekuwa ame pagawa na pepo mchafu, naye alianza kupiga kelele kwa nguvu akisema, 34 “Unataka kutufanya nini, Wewe Yesu wa Nazareti? Ume kuja kutuangamiza? Nakufahamu wewe ni nani. Wewe ni Mtakatifu wa Mungu.” 35 Yesu akamwamuru yule pepo: “Nyamaza! Mtoke!” Yule pepo akamwangusha chini yule mtu mbele yao, akamtoka pasipo kumd huru. 36 Watu wote wakashangaa wakaambiana, “Mafundisho ya mtu huyu ni ya ajabu. Anawaamuru pepo wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka! 37 Habari zake zikaenea pote katika mkoa ule.

Yesu Awaponya Wengi

38 Alipotoka katika sinagogi Yesu alikwenda nyumbani kwa Simoni na alipofika huko alimkuta mama mkwe wa Simoni ana homa kali. Wakamwomba sana amponye. 39 Basi Yesu akasimama kando ya kitanda chake akaiamuru ile homa imtoke. Homa ikamtoka yule mama. Akaamka mara moja akaanza kuwahudumia. 40 Jua lilipokuwa likichwa, wote waliokuwa na wagonjwa wenye maradhi mbalimbali waliwaleta kwa Yesu. Akamgusa kila mgonjwa, akawaponya wote. 41 Pepo wachafu pia waliwatoka watu wengi, nao walipokuwa wakitoka wakapiga kelele wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea na kuwazuia wasiseme, kwa maana walifahamu kuwa yeye ni Kristo.

42 Kesho yake, kulipopambazuka, Yesu alikwenda mahali pa faragha. Watu wengi wakawa wanamtafuta kila mahali, na walipom wona wakajaribu kumzuia asiondoke. 43 Lakini yeye akawaambia, “Ninao wajibu wa kuhubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu sehemu nyingine pia. Hii ndio sababu nilitumwa.” 44 Kwa hiyo akaende lea kuhubiri katika masinagogi ya Yudea. Yesu Awachagua Wanafunzi Wa Kwanza

Siku moja Yesu alipokuwa amesimama akihubiri karibu na ziwa la Genesareti, watu wengi walimsonga ili wapate kusikia neno la Mungu. Akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa, lakini wenye mashua walikuwa wakiosha nyavu zao. Akaingia katika mashua moja, akamwomba mwenye mashua, ambaye jina lake lilikuwa Simoni, aisogeze zaidi katika maji. Kisha akakaa kwenye mashua, akaanza kuwafundisha.

Alipokwisha zungumza na watu akamwambia Simoni, “Sasa ipe leke mashua hadi mahali penye kina kirefu, kisha mshushe nyavu zenu nanyi mtapata samaki.”

Simoni akamjibu, “Bwana, tumekesha usiku kucha tukivua na hatukuambulia kitu cho chote. Lakini, kwa kuwa wewe umesema, tutazishusha nyavu.” Nao walipofanya kama Yesu alivyowaagiza, nyavu zao zikajaa samaki, zikaanza kuchanika! Wakawaashiria wavuvi wa ile mashua nyingine waje kuwasaidia. Mashua zote mbili zikajaa samaki hata karibu kuzama.

Simoni Petro alipoona yaliyotokea alipiga magoti mbele ya Yesu akamwambia, “Bwana,tafadhali uniache kwa maana mimi ni mwe nye dhambi.” Kwa kuwa yeye na wavuvi wenzake walikuwa wamesh angazwa sana na wingi wa samaki waliopata. 10 Hali kadhalika wavuvi wa ile mashua nyingine, Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo walishangazwa pia. Ndipo Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope; tangu sasa utakuwa mvuvi wa watu.”

11 Nao walipokwisha fikisha mashua yao nchi kavu, wakaacha vyote, wakamfuata Yesu. Yesu Amponya Mwenye Ukoma

12 Siku moja Yesu alipokuwa katika mji fulani alitokea mtu mwenye ukoma mwili mzima. Alipomwona Yesu alijitupa chini kwa kunyenyekea akamsihi akisema, “Bwana, ukitaka unaweza kunita kasa!” 13 Yesu akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Ndio, nataka upone; takasika!” Wakati huo huo, ukoma wote ukamtoka . 14 Yesu akamwambia, “Usimweleze mtu ye yote jinsi ulivyopata kupona bali nenda moja kwa moja hadi kwa kuhani ili aone kuwa kweli umepona. Kisha utoe sadaka ya shukrani, kama she ria ya Musa inavyoagiza, ili kuthibitisha kuwa umetakasika.”

15 Lakini sifa za Yesu zikazidi sana kuenea. Watu wakamimi nika kwa wingi kutoka kila upande kuja kumsikiliza na kuponywa maradhi yao. 16 Ila mara kwa mara alitoka peke yake akaenda pasipo na watu akaomba.

Yesu Amponya Mwenye Kupooza

17 Siku moja Yesu alipokuwa akifundisha, Mafarisayo na wal imu wa sheria kutoka katika kila mji wa wilaya za Galilaya, Yudea na Yerusalemu walikuwepo. Na Yesu alikuwa amejaa nguvu ya Mungu ya kuponya wagonjwa.

18-19 Kisha wakaja watu wamembeba mgonjwa aliyepooza kwe nye kitanda. Wakajaribu kumpitisha ndani wamfikishe alipokuwa Yesu, lakini wakashindwa kwa sababu ya msongamano wa watu. Basi wakampandisha juu ya paa, wakaondoa baadhi ya vigae, wakapata nafasi ya kumteremsha yule mgonjwa pamoja na kitanda chake kwa kamba, hadi mbele ya Yesu. 20 Alipoona imani yao, Yesu alimwam bia yule mgonjwa, “Rafiki yangu, umesamehewa dhambi zako.” 21 Wale walimu wa sheria na Mafarisayo wakaanza kusemezana, “Mbona huyu anakufuru! Anadhani yeye ni nani? Hakuna awezae kusamehe dhambi ila Mungu peke yake.”

22 Yesu alifahamu mawazo yao kwa hiyo akawauliza, “Kwa nini mnafikiri mimi ninakufuru? 23 Je, ni lipi lililo rahisi zaidi, kumwambia huyu, ‘Umesamehewa dhambi zako’; au kusema, ‘Simama utembee?’ 24 Sasa nitawahakikishia kuwa mimi Mwana wa Adamu ninao uwezo wa kusamehe dhambi duniani.” Akamgeukia yule mgonjwa aliyepooza, akasema, “Nakuambia: Simama! Chukua kitanda chako uende nyumbani.” 25 Mara yule mtu aliyekuwa amepooza akasimama mbele yao wote, akachukua kitanda chake akaenda zake nyumbani, huku akimtukuza Mungu. 26 Wote waliokuwepo wakastaajabu sana. Wakajaa hofu. Wakamtukuza Mungu, wakasema, “Tumeona maajabu leo.”

Yesu Amwita Lawi

27 Baada ya haya Yesu alimwona afisa mmoja mtoza kodi jina lake Lawi akiwa ofisini mwake, akamwambia, “Njoo uwe mmoja wa wanafunzi wangu.” 28 Lawi akaacha vyote, akaondoka, akamfuata Yesu. 29 Baadaye Lawi akafanya karamu kubwa kumkaribisha Yesu nyumbani kwake. Watoza kodi wengi walikuwa miongoni mwa watu wal ioalikwa. 30 Basi baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria ambao walikuwa kundi moja wakawalalamikia wanafunzi wa Yesu wakisema, “Mbona mnakula na kunywa na wenye dhambi?” 31 Yesu akawajibu, “Wenye afya hawahitaji daktari, lakini wagonjwa wanamhitaji. 32 Sikuja kwa ajili ya wenye haki bali nimekuja kuwaita wenye dhambi ili watubu.”

Yesu Aulizwa Habari Za Kufunga

33 Baadhi ya watu wakamwuliza Yesu, “Wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo hufunga na kusali mara kwa mara. Mbona wanafunzi wako wanakula na kunywa tu?”

34 Yesu akawajibu, “Je, inawezekana wageni walioalikwa har usini kufunga wakati wakiwa na Bwana Harusi? 35 Lakini wakati utafika ambapo Bwana Harusi ataondolewa. Wakati huo ndipo wataka pofunga.

36 Yesu akawapa mfano akawaambia: “Hakuna mtu anayechana nguo mpya ili apate kiraka cha kuweka kwenye nguo kuu kuu. Akifa nya hivyo ataharibu ile nguo mpya na ile kuu kuu itaonekana mbaya zaidi ikiwa na kiraka kipya. 37 Wala watu hawaweki divai mpya katika viriba vilivyochakaa; ukifanya hivyo, hivyo viriba vitapa suka na divai yote itamwagika. 38 Divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya. 39 Na pia hakuna mtu anayependelea divai mpya baada ya kunywa divai iliyoiva vizuri. Kwa maana husema, ‘Hii divai iliyoiva siku nyingi ni bora zaidi.’ ”

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica