Beginning
Yesu Alisha Watu Elfu Nne
8 Muda si mrefu baadaye, umati mkubwa wa watu ulikusanyika tena. Kwa kuwa walikuwa hawana chakula, Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia, 2 “Ninawaonea huruma hawa watu. Wamekuwa nami kwa muda wa siku tatu sasa na hawana chakula. 3 Nikiwaruhusu waende bila kula, watazimia njiani na baadhi yao wametoka mbali.”
4 Wanafunzi wake wakamjibu, “Lakini hapa nyikani tutapata wapi chakula cha kutosha kuwalisha?”
5 Yesu akawauliza, “Mna mikate mingapi?” Wakajibu, “Saba.”
6 Akawaambia watu wakae chini. Kisha akaichukua ile mikate saba na baada ya kushukuru akaimega, akawapa wanafunzi wake wawa gawie watu. Wanafunzi wake wakafanya hivyo. 7 Walikuwa pia na visamaki vichache, Yesu akavibariki, akawaamuru wanafunzi wake wawagawie watu. 8 Watu walikula wakatosheka na baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia wakajaza vikapu saba. 9 Na watu waliokula walikuwa wapata elfu nne. Baada ya kuwaaga, 10 aliin gia kwenye mashua pamoja na wanafunzi wake akaenda sehemu za Dal manutha.
11 Mafarisayo wakaja, wakaanza kumhoji Yesu. Ili kumtega, wakamwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni. 12 Akahuzunika moyoni, akawaambia, “Kwa nini kizazi hiki kinataka ishara? Nawaambieni kweli, hakitapewa ishara yo yote.” 13 Kisha aka waacha, akarudi kwenye mashua, akavuka hadi ng’ambo ya pili.
Chachu Ya Mafarisayo Na Ya Herode
14 Wanafunzi walikuwa wamesahau kuleta mikate ya kutosha. Walikuwa na mkate mmoja tu kwenye mashua. 15 Yesu akawaonya: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo na ya Herode.”
16 Wakaanza kujadiliana wao kwa wao wakasema,“Anasema hivi kwa kuwa hatukuleta mikate.”
17 Yesu alifahamu majadiliano yao, akawauliza: “Mbona mna zungumzia kuhusu kutokuwa na mikate? Bado hamtambui wala kuelewa? Je, mbona mioyo yenu ni migumu kiasi hicho? 18 Mbona mna macho lakini mnashindwa kuona, na masikio lakini mnashindwa kusikia? Je hamkumbuki? 19 Nilipoimega mikate mitano kuwalisha watu elfu tano, mlikusanya mabaki vikapu vingapi?” Wakamjibu, “Kumi na viwili.” 20 “Na nilipomega mikate saba kuwalisha watu elfu nne mlikusanya mabaki vikapu vingapi?” Wakamjibu, “Saba.” 21 Aka wauliza, “Je, bado tu hamwelewi?”
Yesu Amponya Kipofu Huko Bethsaida
22 Wakafika Bethsaida na baadhi ya watu wakamleta kipofu mmoja wakamsihi Yesu amguse. 23 Yesu akamshika mkono huyo kipofu akampeleka nje ya kijiji. Baada ya kuyatemea mate macho ya yule kipofu na kumwekea mikono, Yesu akamwuliza, “Unaona cho chote?”
24 Yule kipofu akaangalia, akasema, “Ninaona watu; wanaonekana kama miti ikitembea.”
25 Yesu akamwekea tena mikono machoni. Ndipo akaona vizuri. Macho yake yakapona kabisa akaweza kuona kila kitu sawa sawa.
26 Yesu akamruhusu aende nyumbani kwake akisema, “Hata kijijini usipitie.”
27 Yesu na wanafunzi wake wakaondoka kwenda katika vijiji vya Kaisaria Filipi. Walipokuwa njiani Yesu akawauliza, “Watu husema mimi ni nani?”
28 Wakamjibu, “ Baadhi husema wewe ni Yohana Mbatizaji; wengine husema ni Eliya na wengine husema wewe ni mmojawapo wa manabii.”
29 Akawauliza, “Na ninyi je, mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, ‘ ‘Wewe ndiye Kristo.”
30 Akawaonya wasim wambie mtu ye yote habari zake.
Yesu Azungumza Juu Ya Kifo Chake
31 Akaanza kuwafundisha wanafunzi wake kuwa yeye, Mwana wa Adamu, atapata mateso mengi na kukataliwa na wazee, na makuhani wakuu na walimu wa sheria; na kwamba atauawa na baada ya siku tatu atafufuka. 32 Aliyasema haya wazi wazi. Ndipo Petro akam chukua kando akaanza kumkemea. 33 Lakini Yesu alipogeuka na kuwatazama wanafunzi wake alimkaripia Petro akamwambia, “Ondoka mbele yangu, shetani! Mawazo yako hayako upande wa Mungu bali upande wa wanadamu.”
34 Ndipo akawaita wale watu pamoja na wanafunzi wake aka waambia, “Mtu ye yote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwe nyewe, auchukue msalaba wake, anifuate. 35 Kwa maana mtu ye yote aipotezaye nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya kuitangaza Habari Njema, ataiokoa. 36 Mtu atafaidi nini kama atapata ulimwengu wote lakini akayaangamiza maisha yake? 37 Au mtu atatoa nini apate tena maisha yake? 38 Mtu ye yote atakayenionea aibu mimi na maneno yangu katika kizazi hiki kiovu na kisichomjali Mungu, na mimi, Mwana wa Adamu, nitamwonea aibu wakati nitakapokuja katika utu kufu wa Baba yangu na malaika watakatifu.”
9 Yesu akaendelea kuwaambia, ‘ ‘Ninawahakikishia kuwa wapo watu hapa ambao hawatakufa kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu ukija kwa nguvu.”
Yesu Ageuka Sura
2 Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohana akawapeleka juu ya mlima mrefu ambapo walikuwa faraghani, peke yao. Na huko, wakiwa wanamtazama, Yesu akageuka sura. 3 Mavazi yake yakametameta kwa weupe, yakang’aa, yakawa meupe kuliko ambavyo dobi ye yote duniani angaliweza kuyang’aarisha. 4 Musa na Eliya wakawatokea nao walikuwa wakizungumza na Yesu.
5 Petro akamwambia Yesu , “Mwalimu, ni vizuri kwamba sisi tuko hapa. Tutengeneze vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Musa na kingine cha Eliya.” 6 Petro hakujua aseme nini kwa maana yeye na wenzake walikuwa wameogopa sana.
7 Ndipo pakatokea wingu, likawafunika, na sauti kutoka katika wingu hilo ikasema, “Huyu ni mwanangu nimpendaye, msikilizeni yeye.” 8 Mara walipotazama huku na huku hawakuona mtu mwingine tena isipokuwa Yesu.
9 Walipokuwa wakiteremka mlimani, Yesu akawakataza wasim wambie mtu ye yote mambo waliyoona, mpaka yeye Mwana wa Mungu atakapofufuka kutoka kwa wafu. 10 Wakatii agizo hilo, lakini wakawa wanajadiliana kati yao maana ya ‘Kufufuka kutoka kwa wafu.’ 11 Wakamwuliza, “Kwa nini walimu wa sheria husema kwamba ni lazima Eliya aje kwanza kabla mambo haya hayajatokea?’ ’ 12 Yesu akawajibu, “Ni kweli, Eliya anakuja kwanza kusawazisha mambo yote. Hata hivyo, mbona imeandikwa kwamba Mimi, Mwana wa Adamu ni lazima niteseke sana na kudharauliwa? 13 Lakini nina waambia, Eliya amekwisha kuja na wamemtendea walivyopenda, kama Maandiko yasemavyo juu yake.”
Yesu Amponya Mvulana Mwenye Pepo
14 Walipowafikia wale wanafunzi wengine, waliwakuta wame zungukwa na umati mkubwa wa watu na baadhi ya walimu wa sheria wakibishana nao. 15 Mara wale watu walipomwona Yesu, walistaaj abu sana, wakamkimbilia, wakamsalimu. 16 Akawauliza wanafunzi wake, “Mnabishana nini nao?”
17 Mtu mmoja katika ule umati wa watu akajibu, “Mwalimu, nimemleta kwako mtoto wangu wa kiume kwa maana amepagawa na pepo ambaye amemfanya kuwa bubu. 18 Kila mara pepo huyo amwingiapo mwanangu, humwangusha chini na kumfanya atokwe povu mdomoni na kusaga meno, kisha mwili wake hukauka. Nimewaomba wanafunzi wako wamtoe pepo huyo, lakini hawakuweza.”
19 Yesu akawaambia, “Ninyi kizazi kisicho na imani! Nita kuwa nanyi mpaka lini? Nitawavumilia mpaka lini? Mleteni huyo mtoto kwangu!” 20 Wakamleta. Yule pepo alipomwona Yesu, alimtia yule mvulana kifafa, akaanguka chini akajiviringisha viringisha huku akitokwa na povu mdomoni. 21 Yesu akamwuliza baba yake, “Mwanao amekuwa na hali hii tangu lini?” Akamjibu, “Tangu utoto wake. 22 Na mara nyingi huyo pepo amemwangusha kwenye moto au kwenye maji ili kuangamiza maisha yake. Lakini kama wewe unaweza kufanya cho chote, tafadhali tuonee huruma, utusaidie.” 23 Yesu akasema, “Kama unaweza! Kila kitu kinawezekana kwa mtu mwenye imani.” 24 Ndipo yule baba akasema kwa sauti, “Ninaamini. Nisaidie niweze kuamini zaidi!” 25 Naye Yesu ali poona umati wa watu unazidi kusongana kuja hapo walipokuwa, akam kemea yule pepo mchafu akisema, “Wewe pepo bubu na kiziwi, naku amuru umtoke, usimwingie tena!” 26 Yule pepo akapiga kelele, akamtia kifafa kwa nguvu kisha akatoka. Yule mvulana alionekana kama amekufa; kwa hiyo watu wengi wakasema, “Amekufa.” 27 Lakini Yesu akamshika mkono akamwinua, naye akasimama.
28 Walipokwisha kuingia ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamwuliza wakiwa peke yao, “Mbona sisi hatukuweza kumtoa huyo pepo?” 29 Yesu akawajibu, “Pepo wa aina hii hawezi kutoka isi pokuwa kwa maombi.”
Yesu Azungumzia Tena Kifo Chake
30 Wakaondoka mahali hapo, wakapitia Galilaya. Yesu haku taka mtu ye yote afahamu walipokuwa 31 kwa maana alikuwa anawa fundisha wanafunzi wake. Alikuwa akiwaambia, “Mimi Mwana wa Adamu nitasalitiwa mikononi mwa watu ambao wataniua, lakini siku ya tatu baada ya kuuawa, nitafufuka.” 32 Lakini wao hawakuelewa alichokuwa akisema na waliogopa kumwuliza.
Mabishano Kuhusu Aliye Mkuu
33 Basi wakafika Kapernaumu na baada ya kuingia nyumbani akawauliza, “Mlikuwa mnabishana nini njiani?” 34 Lakini hawa kumjibu, kwa sababu njiani walikuwa wakibishana kuhusu nani kati yao alikuwa mkuu zaidi.
35 Akaketi chini, akawaita wote kumi na wawili akawaambia: “Mtu anayetaka kuwa kiongozi hana budi kuwa wa chini kuliko wote na kuwa mtumishi wa wote.” 36 Kisha akamchukua mtoto mdogo akamweka mbele yao, akamkumbatia akawaambia, 37 “Mtu ye yote amkaribishaye mmoja wa hawa watoto wadogo, ananikaribisha mimi. Na ye yote anayenikaribisha mimi anamkaribisha Baba yangu ali yenituma.”
Kutumia Jina La Yesu
38 Yohana akamwambia, “Mwalimu, tumemwona mtu akitoa pepo kwa jina lako tukamzuia kwa sababu yeye si mmoja wetu.” 39 Yesu akasema, “Msimzuie, ye yote atendaye miujiza kwa jina langu kwani hawezi kunigeuka mara moja na kunisema vibaya. 40 Kwa maana ye yote ambaye si adui yetu yuko upande wetu. 41 Ninawahakikishia kwamba mtu atakayewapa japo maji ya kunywa kwa kuwa ninyi ni wafuasi wangu, atapewa tuzo.”
Kuhusu Kuwakwaza Wengine
42 “Na mtu atakayesababisha mmojawapo wa hawa wadogo waniaminio kupoteza imani yake, ingalikuwa nafuu kama mtu huyo angefungiwa jiwe kubwa shingoni akatupwa ziwani. 43 Kama mkono wako ukikusababisha utende dhambi, ukate. Ni afadhali kuingia katika uzima ukiwa na mkono mmoja kuliko kuwa na mikono miwili ukaingia katika moto usiozimika. [ 44 Huko funza hawafi wala moto hauzimiki.] 45 Na kama mguu wako ukikusababisha utende dhambi, ukate. Ni afadhali kuingia katika uzima ukiwa kiwete kuliko kuwa na miguu miwili ukaingia katika moto usiozimika. [ 46 Huko funza hawafi wala moto hauzimiki.] 47 Na kama jicho lako litakusababisha utende dhambi, ling’oe. Ni afadhali kuwa chongo ukaingia katika Ufalme wa Mungu kuliko kuwa na macho mawili ukatupwa Jehena. 48 Huko funza hawafi wala moto hauzimiki. 49 Wote watatiwa chumvi kwa moto. 50 “Chumvi ni nzuri, lakini ikipoteza ladha yake utafanya nini ili iweze kukolea tena? Muwe na chumvi ndani yenu. Muishi pamoja kwa amani.”
Copyright © 1989 by Biblica