Print Page Options Listen to Mark 10-11
Previous Prev Day Next DayNext

Beginning

Read the Bible from start to finish, from Genesis to Revelation.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Marko 10-11

Yesu Afundisha Kuhusu Talaka

10 Yesu akaondoka mahali pale akavuka mto wa Yordani, akaenda sehemu ya Yudea. Umati wa watu ukamfuata tena na kama kawaida yake akawafundisha.

Baadhi ya Mafarisayo wakamjia wakitaka kumtega, wakamwul iza, “Ni halali mtu kumwacha mke wake?”

Yesu akawajibu, “Musa aliwaamuruje?” Wakamjibu, “Musa aliruhusu kwamba mume anaweza kumwandikia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”

Yesu akawaambia, “Musa aliwaandikia sheria hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu. Lakini tangu mwanzo wa uumbaji, ‘Mungu aliwaumba mume na mke. Na kwa sababu hii mume atamwacha baba yake na mama yake na hao wawili, watakuwa mwili mmoja.’ Kwa hiyo hawatakuwa wawili tena bali mwili mmoja. Basi, alichokiun ganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”

10 Baadaye waliporudi nyumbani , wanafunzi wa Yesu walimwul iza kuhusu jambo hili.

11 Akawajibu, “Mtu ye yote anayempa mkewe talaka na kuoa mke mwingine, anazini kwa yule mke aliyempa talaka. 12 Na mwa namke anayempa mumewe talaka na kuolewa na mume mwingine, anazini pia.”

Yesu Anawabariki Watoto Wadogo

13 Watu walikuwa wakimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse lakini wanafunzi wake wakawakemea. 14 Yesu alipoona yaliyokuwa yakitokea alichukizwa, akawaambia wanafunzi wake, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa watu kama hawa! 15 Ninawahakikishieni kwamba, mtu ye yote ambaye hataukubali Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.” 16 Akawakumbatia wale watoto wadogo, akaweka mikono yake juu yao, akawabariki.

Mtu Tajiri

17 Yesu alipoanza tena safari yake, mtu mmoja akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake akamwuliza, “Mwalimu mwema, nifanye nini niurithi Ufalme wa milele?”

18 Yesu akamwambia, “Mbona unaniita mwema? Hakuna ali yemwema isipokuwa Mungu peke yake. 19 Unazifahamu amri ‘Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, Usidanganye. Waheshimu baba yako na mama yako .”’

20 Akamjibu, “Mwalimu, amri hizi zote nimezishika tangu nikiwa mtoto.”

21 Yesu akamtazama kwa moyo wa upendo akamwambia, “Umepun gukiwa na kitu kimoja tu. Nenda ukauze vitu vyote ulivyo navyo uwape maskini fedha utakazopata, nawe utakuwa na utajiri mbin guni; kisha njoo, unifuate.”

22 Yule mtu aliposikia hayo, alisikitika sana, akaondoka kwa huzuni kwa sababu alikuwa tajiri sana.

23 Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Itakuwa vigumu sana kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa

Mungu!”

24 Wanafunzi wake wakashtushwa sana na maneno hayo. Lakini Yesu akasema tena, “Wanangu, ni vigumu sana kuingia katika Ufalme wa Mungu. 25 Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”

26 Wanafunzi wake wakashangaa mno. Wakaulizana wao kwa wao, “Ni nani basi anaweza kuokolewa?”

27 Yesu akawatazama akawaambia, “Kwa wanadamu haiwezekani, lakini kwa Mungu si hivyo. Mambo yote yanawezekana kwa Mungu.” 28 Petro akaanza kumwambia, “Sisi tumeacha kila kitu tukakufu ata!”

29 Yesu akajibu, “Ninawaambieni hakika, hakuna mtu ye yote aliyeacha nyumba, kaka, dada, mama, baba, watoto au shamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya kuitangaza Habari Njema, 30 ambaye hatalipwa katika ulimwengu huu mara mia zaidi: nyumba, kaka, dada, mama, watoto, mashamba na mateso pia; na kupewa uzima wa milele katika ulimwengu ujao. 31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho na wa mwisho watakuwa wa kwanza.”

Yesu Azungumzia Tena Kifo Chake

32 Walikuwa njiani kuelekea Yerusalemu na Yesu alikuwa ame tangulia. Wanafunzi wake walikuwa wamejawa na hofu, na watu wal iowafuata walikuwa wanaogopa. Yesu akawachukua tena wale wana funzi wake kumi na wawili kando akawaambia yatakayompata. 33 Akasema, “Tunakwenda Yerusalemu, na Mimi Mwana wa Adamu nitapelekwa kwa makuhani wakuu na walimu wa sheria; nao watanihu kumu adhabu ya kifo na kunikabidhi kwa mataifa. 34 Wao watanid hihaki na kunitemea mate na kunipiga na kuniua. Baada ya siku tatu, nitafufuka.”

Ombi La Yakobo Na Yohana

35 Yakobo na Yohana wana wa Zebedayo wakamwendea Yesu wakamwambia, “Bwana, kuna jambo moja tungependa kukuomba.”

36 Akawauliza, “Mngependa niwafanyie jambo gani?”

37 Wakamjibu, “ Tunakuomba utakapoketi katika ufalme wako wa utukufu, uturuhusu tuketi pamoja nawe, mmoja wetu mkono wako wa kulia na mwingine mkono wako wa kushoto.”

38 Yesu akawaambia, “Hamjui mnaloliomba. Mko tayari kunywea kikombe cha mateso nitakachokunywa? Mnaweza kubatizwa ubatizo nitakaobatizwa?”

39 Wakamjibu, “ Tunaweza.” Yesu akawaambia, “Mtakunywa katika kikombe nitakachokunywa na kubatizwa ubatizo nitakaobati zwa. 40 Lakini kuhusu kuketi mkono wangu wa kulia au wa kushoto si juu yangu mimi kuwaruhusu. Mungu atatoa nafasi hizo kwa watu aliowaandalia.”

41 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, waliwaka sirikia Yakobo na Yohana. 42 Yesu akawaita wanafunzi wake wote pamoja akawaambia, “Mnafahamu kwamba watu wanaotawala watu wa mataifa hutumia mabavu, na viongozi wa vyeo vya juu hupenda kuon yesha wana madaraka! 43 Lakini haipasi kuwa hivyo kati yenu. Badala yake, anayetaka kuwa mkuu kati yenu hana budi kuwa mtum ishi wenu, 44 na ye yote anayetaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa mtumishi wa wote. 45 Kwa maana hata mimi Mwana wa Adamu sikuja ili nitumikiwe, bali nilikuja ili niwe mtumishi na kutoa maisha yangu yawe fidia kwa ajili ya watu wengi.”

Yesu Amponya Kipofu Bartimayo

46 Wakafika Yeriko. Na Yesu alipokuwa akiondoka pamoja na Wanafunzi wake na umati wa watu, kipofu mmoja, jina lake Barti mayo, mwana wa Timayo, alikuwa ameketi kando kando ya njia, akiomba.

47 Aliposikia kuwa Yesu wa Nazareti alikuwa akipita, akaanza kupiga kelele, “Yesu, Mwana wa Daudi, nionee huruma!”

48 Watu wengi wakamkemea, wakamwambia akae kimya. Lakini yeye alipiga kelele zaidi, “Mwana wa Daudi, nionee huruma!”

49 Yesu akasimama akawaambia, “Mwiteni.” Wakamwita wakamwambia, “Changamka! Usimame, anakuita.”

50 Akatupa vazi lake kando, akaruka juu, akamwendea Yesu. 51 Yesu akamwuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akajibu, “Mwalimu, nataka kuona tena.” 52 Yesu akamwambia, “Nenda, imani yako imekuponya.” Wakati huo huo akaweza kuona, akamfuata Yesu njiani.

Yesu Aingia Yerusalemu

11 Walipokaribia Yerusalemu, wakiwa katika miji ya Bethfage na Bethania katika mlima wa Mizeituni, Yesu aliwatuma wanafunzi wake wawili watangulie. Akawaagiza, “Nendeni kwenye kijiji kile kilichoko mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtam wona mwana punda amefungwa, ambaye hajawahi kupandwa na mtu ye yote. Mfungueni mumlete hapa. Kama mtu atawauliza, ‘Mbona mnam fungua?’ Mwambieni, ‘Bwana anamhitaji na atamrudisha mara moja.’ ” 4-5 Wakaenda, wakamkuta mwana punda mmoja kando ya barabara, akiwa amefungwa kwenye mlango wa nyumba. Walipokuwa wakimfungua, watu waliokuwa wamesimama karibu wakauliza, “Mbona mnamfungua huyo mwanapunda?” Wakawajibu kama Yesu alivyokuwa amewaagiza, na wale watu wakawaruhusu.

Wakamleta huyo mwana punda kwa Yesu wakamtandikia mavazi yao, akaketi juu yake. 8-10 Watu wengi wakatandaza nguo zao barabarani na wengine wakatandaza matawi waliyokata mashambani. Na wote waliotangulia na wale waliofuata wakapaza sauti zao wakasema: “Hosana! Mungu apewe sifa! Mungu ambariki yeye anayekuja kwa jina la Bwana! Ubarikiwe Ufalme unaokuja wa baba yetu Daudi! Mungu asifiwe!”

11 Yesu akaingia Yerusalemu, akaenda Hekaluni akaangalia kila kitu. Lakini kwa kuwa ilikuwa jioni, akaenda Bethania na wale wanafunzi kumi na wawili.

Yesu Alaani Mtini Usiozaa

12 Kesho yake walipokuwa wanaondoka Bethania, Yesu alikuwa na njaa. 13 Alipouona mtini kwa mbali, alikwenda kuangalia kama ulikuwa na matunda. Alipoufikia, alikuta una majani tu kwa kuwa hayakuwa majira ya tini. 14 Yesu akauambia ule mti, “Hakuna mtu atakayekula tini kutoka kwako tena.” Wanafunzi wake walimsikia akisema hayo.

Yesu Afukuza Wafanya Biashara Hekaluni

15 Walipofika Yerusalemu, Yesu aliingia Hekaluni akaanza kuwafukuza watu waliokuwa wakifanya biashara humo. Akapindua meza za waliokuwa wakibadilisha fedha na viti vya watu waliokuwa wakiuza njiwa. 16 Hakuruhusu mtu ye yote kuchukua bidhaa kupi tia ukumbi wa Hekalu. 17 Akawafundisha akisema, “Je, haikuan dikwa katika Maandiko kuwa: ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa watu wote’? Mbona ninyi mmeigeuza kuwa pango la wany ang’anyi?”

18 Makuhani wakuu na walimu wa sheria wakapata habari. Wakatafuta njia ya kumwangamiza. Walimwogopa kwa sababu watu wal ikuwa wamevutiwa sana na mafundisho yake.

19 Ilipofika jioni, Yesu na wanafunzi wake walikwenda nje ya mji.

Fundisho Kuhusu Ule Mtini Uliolaaniwa

20 Asubuhi yake walipokuwa wakipita, wakauona ule mtini ume nyauka kutoka juu hadi kwenye mizizi yake. 21 Petro alikumbuka, akamwambia Yesu, “Mwalimu, tazama! Ule mtini ulioulaani umeny auka!”

22 Yesu akamjibu, “Mwamini Mungu. 23 Nawaambieni hakika, mtu akiuambia mlima huu, ‘Ondoka hapo nenda kajitupe baharini,’ akiamini pasipo kuwa na mashaka yo yote kwamba anayosema yata tendeka, atatimiziwa maombi yake. 24 Kwa hiyo nawaambieni, lo lote mnaloomba katika sala, aminini kwamba mmekwisha kulipokea nanyi mtapewa. 25 Nanyi mnaposimama kusali, sameheni kila mtu aliyewakosea ili Baba yenu wa mbinguni apate kuwasamehe ninyi makosa yenu.” [ 26 Lakini msipowasamehe wengine, basi makosa mliyofanya ninyi hayatasamehewa na Baba yenu wa mbinguni.]

Yesu Aulizwa Kuhusu Mamlaka Yake

27 Wakafika tena Yerusalemu. Wakati Yesu alipokuwa akitem bea Hekaluni, makuhani wakuu, walimu wa sheria pamoja na wazee wakamjia 28 wakamwuliza, “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?

Na ni nani aliyekupa mamlaka hayo?”

29 Yesu akawajibu, “Nitawauliza swali mmoja. Mkinijibu, mimi pia nitawaeleza ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya. 30 Niambieni, mamlaka aliyotumia Yohana kubatiza watu, yalitoka kwa Mungu au kwa watu?”

31 Wakaanza kubishana, “Tukisema, ‘Yalitoka kwa Mungu’ atatuuliza, ‘Mbona hamkumwamini?’ 32 Je, tunaweza kusema ‘Yali toka kwa watu’? - Waliogopa watu kwa sababu kila mtu aliamini kwamba Yohana Mbatizaji alikuwa nabii. 33 Kwa hiyo wakamjibu, “Hatujui.” Na Yesu akawaambia, “Mimi pia sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.”

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica