Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Old/New Testament

Each day includes a passage from both the Old Testament and New Testament.
Duration: 365 days
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Version
Error: Book name not found: 2Kgs for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yohana 1:1-28

Yesu ni Neno la Mungu la Milele

Mwanzoni Kabla ulimwengu haujaumbwa
    alikuwepo Neno.[a]
Huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu,
    na Neno alikuwa Mungu.
Alikuwepo pamoja na Mungu
    toka mwanzo.
Kila kitu kilifanyika kupitia kwake.
    Hakuna chochote katika uumbaji wa Mungu
    kilichofanyika bila yeye.
Ndani yake Neno kulikuwemo na uzima,
    na uzima huo ulikuwa nuru
    kwa ajili ya watu wa ulimwenguni.
Nuru[b] hiyo yamulika gizani,
    na giza halikuishinda.[c]

Alikuwepo mtu aliyeitwa Yohana, aliyetumwa na Mungu. Alikuja kuwaambia watu kuhusu nuru. Ili kupitia kwake watu wote waweze kusikia kuhusu yule aliye nuru na wamwamini. Yohana mwenyewe hakuwa nuru. Lakini alikuja kuwaambia watu kuhusu nuru.

Nuru ya kweli,
    anayeleta mwangaza kwa watu wote,
    alikuwa tayari kuonekana kwa ulimwengu.
10 Huyo Neno alikuwapo tayari ulimwenguni.
    Ulimwengu uliumbwa kupitia yeye,
    lakini ulimwengu haukumkubali.
11 Alikuja kwa ulimwengu ulio wake,
    na watu wake mwenyewe hawakumkubali.
12 Lakini baadhi ya watu walimkubali wakamwamini
    na akawapa haki ya kuwa watoto wa Mungu.
13 Ndiyo, walikuwa watoto wa Mungu,
    lakini si kwa kuzaliwa kimwili.
Haikuhusisha matamanio
    ya kibinadamu.
Mungu mwenyewe aliwafanya
    kuwa watoto wake.
14 Neno akafanyika kuwa mwanadamu
    na akaishi pamoja nasi.
Tuliouna ukuu wa uungu wake;
    utukufu alionao Mwana pekee wa Baba.

15 Yohana alizungumza kuhusu yeye alipopaza sauti na kusema, “Huyu ndiye niliyemzungumzia habari zake niliposema, ‘Anayekuja baada yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa sababu alikuwepo mwanzoni, zamani kabla sijazaliwa.’”

16 Alikuwa amejaa neema na kweli ya Mungu,
    tulipokea kutoka baraka moja
    baada ya nyingine[d] kutoka kwake.
17 Hiyo ni kusema kuwa,
    sheria ililetwa kwetu kupitia Musa.
Lakini neema na kweli imekuja
    kupitia Yesu Kristo.
18 Hakuna aliyewahi kumwona Mungu
    isipokuwa Mwana peke yake,
ambaye yeye mwenyewe ni Mungu,
    ametuonesha jinsi Mungu alivyo.
Yuko karibu sana na Baba
    kiasi kwamba tunapomwona,
    tumemwona Mungu.

Yohana Azungumza Juu ya Kristo

(Mt 3:1-12; Mk 1:1-8; Lk 3:1-9,15-17)

19 Viongozi wa Kiyahudi kule Yerusalemu walituma baadhi ya makuhani na Walawi kwa Yohana kumwuliza, “Wewe ni nani?” Yohana akawaeleza kweli. 20 Akajibu kwa wazi bila kusitasita, “Mimi siyo Masihi.”

21 Wakamwuliza, “Sasa wewe ni nani? Je, wewe ni Eliya?”

Yohana akawajibu, “Hapana, mimi siye Eliya.”

Wakamwuliza tena, “Je, wewe ni Nabii?”[e]

Naye akawajibu, “Hapana, mimi siyo nabii.”

22 Kisha wakamwuliza, “Wewe ni nani basi? Tueleze habari zako. Tupe jibu la kuwaambia wale waliotutuma. Unajitambulisha mwenyewe kuwa nani?”

23 Yohana akawaambia maneno ya nabii Isaya:

“‘Mimi ni mtu anayeipaza sauti yake toka nyikani:
    Nyoosheni njia kwa ajili ya Bwana.’”(A)

24 Wale Wayahudi walitoka kwa Mafarisayo. 25 Wakamwambia Yohana, “Unasema kuwa wewe siyo Masihi. Na unasema kuwa wewe siyo Eliya wala nabii. Sasa kwa nini unawabatiza watu?”

26 Yohana akajibu, “Nawabatiza watu kwa maji. Lakini yupo mtu hapa kati yenu ambaye ninyi hamumjui. 27 Yeye ndiye yule anayekuja baada yangu. Nami sina sifa za kuwa mtumwa anayefungua kamba za viatu vyake.”

28 Mambo haya yote yalitokea Bethania iliyokuwa upande mwingine wa Mto Yordani. Hapa ndipo Yohana alipowabatiza watu.

Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)

© 2017 Bible League International