Add parallel Print Page Options

Yesu Awatuma Kazi Mitume Wake

(Mk 3:13-19; 6:7-13; Lk 6:12-16; 9:1-6)

10 Yesu aliwaita pamoja wafuasi wake kumi na mbili. Akawapa uwezo juu ya pepo wabaya ili waweze kuwafukuza na pia kuponya kila aina ya magonjwa na maradhi. Haya ni majina ya mitume kumi na wawili:

Simoni (ambaye pia aliitwa Petro),

Andrea, kaka yake Petro,

Yakobo, mwana wa Zebedayo,

Yohana, kaka yake Yakobo,

Filipo,

Bartholomayo,

Thomaso,

Mathayo, mtoza ushuru,

Yakobo, mwana wa Alfayo,

Thadayo,

Simoni Mzelote,

Yuda Iskariote (yule ambaye baadaye alimsaliti Yesu).

Yesu aliwatuma mitume hawa kumi na wawili pamoja na maelekezo haya: “Msiende kwa watu wasio Wayahudi. Na msiingie katika miji ambako Wasamaria wanaishi. Lakini nendeni kwa watu wa Israeli. Wako kama kondoo waliopotea. Mtakapokwenda, waambieni hivi: ‘Ufalme wa Mungu umekaribia.’ Waponyeni wagonjwa. Fufueni waliokufa. Waponyeni watu wenye magonjwa mabaya sana ya ngozi. Na toeni mashetani kwa watu. Ninawapa nguvu hii bure, hivyo wasaidieni wengine bure. Msibebe pesa pamoja nanyi; dhahabu au fedha au shaba nyekundu. 10 Msibebe mikoba. Chukueni nguo na viatu mlivyovaa tu. Na msichukue fimbo ya kutembelea. Mfanyakazi anastahili kupewa anachohitaji.

11 Mnapoingia katika mji, tafuteni kwa makini hadi mumpate mtu anayefaa na mkae katika nyumba yake mpaka mtakapoondoka mjini. 12 Mtakapoingia katika nyumba hiyo, semeni, ‘Amani iwe kwenu.’ 13 Ikiwa watu katika nyumba hiyo watawakaribisha, wanastahili amani yenu. Wapate amani mliyowatakia. Lakini ikiwa hawatawakaribisha, hawastahili amani yenu. Ichukueni amani mliyowatakia. 14 Na ikiwa watu katika nyumba au mji watakataa kuwapokea au kuwasikiliza, basi ondokeni mahali hapo na mkung'ute mavumbi kutoka katika miguu yenu. 15 Ninaweza kuwathibitishia kuwa siku ya hukumu itakuwa vibaya sana kwa mji huo kuliko watu wa Sodoma na Gomora.[a]

Yesu Aonya Kuhusu Matatizo

(Mk 13:9-13; Lk 21:12-17)

16 Sikilizeni! Ninawatuma, nanyi mtakuwa kama kondoo katikati ya mbwa mwitu. Hivyo muwe na akili kama nyoka. Lakini pia muwe kama njiwa na msimdhuru yeyote. 17 Muwe waangalifu! Wapo watu watakaowakamata na kuwapeleka ili kuwashitaki mbele ya mabaraza ya mijini. Watawachapa ndani ya masinagogi yao. 18 Mtasimamishwa mbele ya magavana na wafalme. Watu watawafanyia ninyi hivi kwa sababu mnanifuata. Mtakuwa mashahidi wangu mbele za wafalme na magavana hao na kwa watu wa mataifa mengine. 19 Mtakapokamatwa, msisumbuke kuhusu nini mtakachosema au namna gani mtakavyosema. Katika wakati huo mtapewa maneno ya kusema. 20 Si ninyi mtakaoongea; Roho wa Baba Mungu wenu atakuwa anaongea kupitia ninyi.

21 Ndugu watakuwa kinyume cha ndugu zao wenyewe na kuwapeleka kwenda kuuawa. Baba watawapeleka watoto wao wenyewe kuuawa. Watoto watapigana kinyume na wazazi wao na watawapeleka kuuawa. 22 Kila mtu atawachukia kwa sababu mnanifuata mimi. Lakini atakayekuwa mwaminifu mpaka mwisho ataokolewa. 23 Mnapotendewa vibaya katika mji mmoja, nendeni katika mji mwingine. Ninawaahidi kuwa hamtamaliza kwenda katika miji ya Israeli kabla Mwana wa Adamu hajarudi.

24 Wanafunzi si wazuri kuliko mwalimu wao. Watumwa si wazuri kuliko bwana wao. 25 Inatosha kwa wanafunzi kuwa kama walimu wao na watumwa kuwa kama bwana wao. Iwapo watu hao wananiita ‘mtawala wa pepo’, na mimi ni kiongozi wa familia, basi ni dhahiri kwa kiasi gani watawatukana ninyi, mlio familia yangu!

Mwogopeni Mungu, Siyo Watu

(Lk 12:2-7)

26 Hivyo msiwagope watu hao. Kila kitu kilichofichwa kitaoneshwa. Kila kilicho siri kitajulikana. 27 Ninayowaambia ninyi faraghani myaseme hadharani. Kila ninachowanong'oneza nawataka mkiseme kwa sauti kila mtu asikie.

28 Msiwaogope watu. Wanaweza kuua mwili, lakini hawawezi kuiua roho. Mnapaswa kumwogopa Mungu, anayeweza kuuharibu mwili na roho jehanamu. 29 Ndege wanapouzwa, ndege wawili wadogo hugharimu senti moja tu. Lakini hakuna hata mmoja wa ndege hao wadogo anaweza kufa bila Baba yenu kufahamu. 30 Mungu anafahamu idadi ya nywele katika vichwa vyenu. 31 Hivyo msiogope. Mna thamani kuliko kundi kubwa la ndege.

Msiionee Haya Imani Yenu

(Lk 12:8-9)

32 Iwapo mtawaambia watu wengine kuwa mnaniamini, nitamwambia Baba yangu aliye mbinguni kuwa ninyi ni wangu. 33 Lakini ikiwa mtasimama mbele ya wengine na kusema kuwa hamniamini, nitamwambia Baba yangu aliye mbinguni kuwa ninyi si wangu.

Kumfuata Yesu Kunaleta Matatizo

(Lk 12:51-53; 14:26-27)

34 Msidhani kuwa nilikuja duniani kuleta amani. Sikuja kuleta amani. Nilikuja kuleta vita. 35 Nimekuja ili hili litokee:

‘Mwana atamgeuka baba yake.
    Binti atamgeuka mama yake.
Binti mkwe atamgeuka mama mkwe wake.
36     Hata watu wa familia zenu watakuwa adui zenu.’(A)

37 Wale wanaowapenda baba zao au mama zao kuliko wanavyonipenda mimi hawana thamani kwangu. Na wale wanaowapenda wana wao au binti zao kuliko wanavyonipenda mimi hawastahili kuwa wafuasi wangu. 38 Wale ambao hawataupokea msalaba waliopewa wanaponifuata hawastahili kuwa wanafunzi wangu na kunifuata. 39 Wale wanaojaribu kuyatunza maisha waliyonayo, watayapoteza. Lakini wale wanaoyaacha maisha yao kwa ajili yangu watapata uzima halisi.

Mungu Atawabariki Wanaowakaribisha Ninyi

(Mk 9:41)

40 Yeyote anayewakubali ninyi ananikubali mimi. Na yeyote anayenikubali anamkubali yule aliyenituma. 41 Yeyote anayemkubali nabii kwa sababu ni nabii atapata ujira wa nabii. Na yeyote anayemkubali mwenye haki kwa sababu ni mwenye haki atapata ujira anaoupata mwenye haki. 42 Yeyote anayemsaidia mmoja wa wafuasi wangu hawa wanyenyekevu kwa sababu ni wafuasi wangu hakika atapata ujira, hata ikiwa wanawapa tu kikombe cha maji baridi.”

Footnotes

  1. 10:15 Sodoma na Gomora Miji ambayo Mungu aliiangamiza kwa sababu watu waliokuwa wakiishi pale walikuwa waovu sana. Tazama Mwa 19.

Jesus Sends Out the Twelve(A)(B)(C)(D)(E)

10 Jesus called his twelve disciples to him and gave them authority to drive out impure spirits(F) and to heal every disease and sickness.(G)

These are the names of the twelve apostles: first, Simon (who is called Peter) and his brother Andrew; James son of Zebedee, and his brother John; Philip and Bartholomew; Thomas and Matthew the tax collector; James son of Alphaeus, and Thaddaeus; Simon the Zealot and Judas Iscariot, who betrayed him.(H)

These twelve Jesus sent out with the following instructions: “Do not go among the Gentiles or enter any town of the Samaritans.(I) Go rather to the lost sheep of Israel.(J) As you go, proclaim this message: ‘The kingdom of heaven(K) has come near.’ Heal the sick, raise the dead, cleanse those who have leprosy,[a] drive out demons. Freely you have received; freely give.

“Do not get any gold or silver or copper to take with you in your belts(L) 10 no bag for the journey or extra shirt or sandals or a staff, for the worker is worth his keep.(M) 11 Whatever town or village you enter, search there for some worthy person and stay at their house until you leave. 12 As you enter the home, give it your greeting.(N) 13 If the home is deserving, let your peace rest on it; if it is not, let your peace return to you. 14 If anyone will not welcome you or listen to your words, leave that home or town and shake the dust off your feet.(O) 15 Truly I tell you, it will be more bearable for Sodom and Gomorrah(P) on the day of judgment(Q) than for that town.(R)

16 “I am sending you out like sheep among wolves.(S) Therefore be as shrewd as snakes and as innocent as doves.(T) 17 Be on your guard; you will be handed over to the local councils(U) and be flogged in the synagogues.(V) 18 On my account you will be brought before governors and kings(W) as witnesses to them and to the Gentiles. 19 But when they arrest you, do not worry about what to say or how to say it.(X) At that time you will be given what to say, 20 for it will not be you speaking, but the Spirit of your Father(Y) speaking through you.

21 “Brother will betray brother to death, and a father his child; children will rebel against their parents(Z) and have them put to death.(AA) 22 You will be hated by everyone because of me,(AB) but the one who stands firm to the end will be saved.(AC) 23 When you are persecuted in one place, flee to another. Truly I tell you, you will not finish going through the towns of Israel before the Son of Man comes.(AD)

24 “The student is not above the teacher, nor a servant above his master.(AE) 25 It is enough for students to be like their teachers, and servants like their masters. If the head of the house has been called Beelzebul,(AF) how much more the members of his household!

26 “So do not be afraid of them, for there is nothing concealed that will not be disclosed, or hidden that will not be made known.(AG) 27 What I tell you in the dark, speak in the daylight; what is whispered in your ear, proclaim from the roofs. 28 Do not be afraid of those who kill the body but cannot kill the soul. Rather, be afraid of the One(AH) who can destroy both soul and body in hell. 29 Are not two sparrows sold for a penny? Yet not one of them will fall to the ground outside your Father’s care.[b] 30 And even the very hairs of your head are all numbered.(AI) 31 So don’t be afraid; you are worth more than many sparrows.(AJ)

32 “Whoever acknowledges me before others,(AK) I will also acknowledge before my Father in heaven. 33 But whoever disowns me before others, I will disown before my Father in heaven.(AL)

34 “Do not suppose that I have come to bring peace to the earth. I did not come to bring peace, but a sword. 35 For I have come to turn

“‘a man against his father,
    a daughter against her mother,
a daughter-in-law against her mother-in-law(AM)
36     a man’s enemies will be the members of his own household.’[c](AN)

37 “Anyone who loves their father or mother more than me is not worthy of me; anyone who loves their son or daughter more than me is not worthy of me.(AO) 38 Whoever does not take up their cross and follow me is not worthy of me.(AP) 39 Whoever finds their life will lose it, and whoever loses their life for my sake will find it.(AQ)

40 “Anyone who welcomes you welcomes me,(AR) and anyone who welcomes me welcomes the one who sent me.(AS) 41 Whoever welcomes a prophet as a prophet will receive a prophet’s reward, and whoever welcomes a righteous person as a righteous person will receive a righteous person’s reward. 42 And if anyone gives even a cup of cold water to one of these little ones who is my disciple, truly I tell you, that person will certainly not lose their reward.”(AT)

Footnotes

  1. Matthew 10:8 The Greek word traditionally translated leprosy was used for various diseases affecting the skin.
  2. Matthew 10:29 Or will; or knowledge
  3. Matthew 10:36 Micah 7:6