Font Size
Luka 9:1-6
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Luka 9:1-6
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yesu Awatuma Kazi Mitume Wake
(Mt 10:5-15; Mk 6:7-13)
9 Yesu aliwaita mitume wake kumi na wawili pamoja, akawapa nguvu kuponya magonjwa na kutoa pepo kwa watu. 2 Akawatuma kwenda kuhubiri kuhusu Ufalme wa Mungu na kuponya wagonjwa. 3 Akawaambia, “Mnaposafiri, msibebe kitu chochote: msichukue fimbo ya kutembelea, msibebe mkoba, chakula au fedha. Chukueni nguo mlizovaa tu kwa ajili ya safari yenu. 4 Mkiingia katika nyumba; kaeni katika nyumba hiyo mpaka mtakapokuwa mnatoka katika mji huo. 5 Ikiwa watu katika mji mtakaoingia hawatawakaribisha, nendeni nje ya mji na kuyakung'uta mavumbi miguuni mwenu kama onyo kwao.”
6 Hivyo mitume wakaondoka. Walisafiri katika miji yote. Walihubiri Habari Njema na kuponya wagonjwa kila mahali.
Read full chapter
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International