Revised Common Lectionary (Semicontinuous)
15 Hivyo Kristo huwaletea watu wake agano jipya kutoka kwa Mungu. Huleta agano hili ili wale walioteuliwa na Mungu waweze kuzipata baraka ambazo Mungu aliwaahidi, baraka zinazodumu milele. Hili laweza kutokea tu kwa sababu Kristo alikufa ili awaweke huru watu kutokana na dhambi zilizotendwa dhidi ya amri za agano la kwanza.
16 Mtu anapofariki na akaacha usia, ni lazima uwepo uthibitisho kwamba yule aliyeandika usia amefariki. 17 Usia haumaanishi chochote wakati aliyeuandika bado yuko hai. Unaweza kutumika mara tu baada ya kifo cha mtu huyo. 18 Ndiyo sababu ili kuthibitisha kifo damu ilihitajika ili kuanza agano la kwanza baina ya Mungu na watu wake. 19 Kwanza, Musa aliwaeleza watu kila agizo katika sheria. Kisha akachukua damu ya ndama dume[a] na kuichanganya na maji. Alitumia sufu nyekundu na tawi la hisopo kunyunyiza damu na maji katika kitabu cha sheria na kwa watu. 20 Kisha akasema, “Hii ni damu inayoweka agano liwe zuri agano ambalo Mungu aliwaagiza mlifuate.”(A) 21 Kwa jinsi hiyo hiyo, Musa alinyunyiza damu katika Hema Takatifu. Aliinyunyiza damu juu ya kila kitu kilichotumika katika ibada. 22 Sheria inasema kwamba karibu kila kitu kinapaswa kutakaswa kwa damu. Dhambi haziwezi kusamehewa bila sadaka ya damu.
Yesu Kristo ni Dhabihu yetu kwa Ajili ya Dhambi
23 Mambo haya ni nakala ya mambo halisi yaliyoko mbinguni. Nakala hizi zinapaswa kutakaswa kwa sadaka ya wanyama. Lakini mambo halisi yaliyoko mbinguni yanapaswa kuwa na sadaka zilizo bora zaidi. 24 Kristo alienda katika Patakatifu pa Patakatifu. Lakini hapakuwa mahali palipotengenezwa na mwanadamu, ambapo ni nakala tu ya ile iliyo halisi. Alienda katika mbingu, na yuko huko sasa mbele za Mungu ili atusaidie sisi.
© 2017 Bible League International