Revised Common Lectionary (Complementary)
Wokovu Wetu ni Mkuu Kuliko Sheria
2 Hivyo tunapaswa kuwa makini zaidi kuzingatia yale tuliyofundishwa. Tunapaswa kuwa makini ili tusiondolewe polepole kutoka katika njia iliyo ya kweli. 2 Fundisho kwamba Mungu alizungumza kupitia malaika limedhihirishwa kuwa ni la kweli. Na kila mara watu wake walipotenda jambo kinyume na fundisho lake, waliadhibiwa kwa yale waliyofanya. Waliadhibiwa walipoacha kutii fundisho hilo. 3 Hivyo kwa hakika hata nasi tutaadhibiwa kama hatutauzingatia wokovu mkuu tulionao. Alikuwa ni Bwana Yesu aliyewaambia watu kwa mara ya kwanza juu ya wokovu huo. Na wale waliomsikiliza walithibitisha kwetu kuwa yale mambo yalikuwa ni kweli. 4 Mungu alithibitisha hayo pia kwa kutumia ishara, maajabu, na aina zingine zote za miujiza. Na alithibitisha hayo kwa kuwapa watu vipawa tofauti kwa njia ya Roho Mtakatifu kwa namna ile aliyotaka.
Kristo Akawa Kama Watu Ili Awaokoe
5 Mungu hakuwachagua malaika wawe watawala juu ya ulimwengu mpya unaokuja. Ulimwengu huo ujao ni ndiyo ambao tumekuwa tukiuzungumzia. 6 Imeandikwa mahali fulani katika Maandiko:
“Kwa nini watu ni muhimu sana kwako?
Kwa nini hata unafikiri juu yao?
Kwa nini unamjali mwana wa mwanadamu?[a]
Je, yeye ni muhimu kiasi hicho?
7 Kwa muda mfupi ulimfanya awe chini kuliko malaika.
Ukamvisha taji yenye utukufu na heshima.
8 Ukaweka kila kitu chini ya udhibiti wake.”[b](A)
Kama Mungu aliweka vitu vyote chini ya udhibiti wake, basi hakikuwepo chochote kilichoachwa ambacho hakukitawala. Lakini bado hatujamwona akitawala juu ya vyote. 9 Kwa kipindi kifupi Yesu aliwekwa chini kuliko malaika, lakini sasa tunamwona akiwa amevaa taji ya utukufu na heshima kwa sababu aliteseka na kufa. Kwa sababu ya neema ya Mungu, Yesu alikufa kwa ajili ya kila mmoja.
© 2017 Bible League International