Revised Common Lectionary (Complementary)
Watu Wamsifu Mungu Mbinguni
19 Baada ya hili nikasikia kitu kilichosikika kama kundi kubwa la watu mbinguni. Walikuwa wakisema:
“Haleluya![a]
Ushindi, utukufu na nguvu ni vyake Mungu wetu.
2 Hukumu zake ni za kweli na za haki.
Mungu wetu amemwadhibu kahaba.
Ndiye aliyeiharibu dunia kwa uzinzi wake.
Mungu amemwadhibu kahaba kulipa kisasi cha vifo vya watumishi wake.”
3 Pia, watu hawa walisema:
“Haleluya!
Anaungua na moshi wake utasimama milele na milele.”
4 Ndipo wazee ishirini na nne na viumbe wenye uhai wanne wakaanguka chini kusujudu wakamwabudu Mungu, akaaye kwenye kiti cha enzi. Wakasema:
“Amina! Haleluya!”
5 Sauti ikatoka kwenye kiti cha enzi na kusema:
“Msifuni Mungu wetu,
ninyi nyote mnaomtumikia!
Msifuni Mungu wetu,
ninyi nyote mlio wadogo na wakubwa mnaomheshimu!”
6 Kisha nikasikia kitu kilichosikika kama kundi kubwa la watu. Kilikuwa na kelele kama mawimbi ya bahari au radi. Watu walikuwa wakisema:
“Haleluya!
Bwana Mungu wetu anatawala.
Ndiye Mwenye Nguvu, Mungu Mwenyezi.
7 Tushangilie na kufurahi na
kumpa Mungu utukufu!
Mpeni Mungu utukufu, kwa sababu arusi ya Mwanakondoo imewadia.
Na bibi arusi wa Mwanakondoo amekwisha jiandaa.
8 Nguo ya kitani safi ilitolewa kwa bibi arusi ili avae.
Kitani ilikuwa safi na angavu.”
(Kitani safi inamaanisha mambo mazuri ambayo watakatifu wa Mungu waliyatenda.)
© 2017 Bible League International