Revised Common Lectionary (Complementary)
Timotheo Afuatana na Paulo na Sila
16 Paulo alikwenda Derbe kisha Listra, ambako mfuasi wa Yesu aliyeitwa Timotheo aliishi. Mamaye Timotheo alikuwa mwamini wa Kiyahudi, lakini baba yake alikuwa Myunani. 2 Waamini katika miji ya Listra na Ikonia walimsifu Timotheo kwa mambo mema. 3 Paulo alitaka kusafiri pamoja na Timotheo, lakini Wayahudi wote walioishi katika eneo lile walijua kuwa baba yake alikuwa Myunani. Hivyo ikamlazimu Paulo amtahiri Timotheo ili kuwaridhisha Wayahudi.
4 Kisha Paulo na wale waliokuwa pamoja naye wakasafiri kupitia miji mingine. Wakawapa waamini kanuni na maamuzi yaliyofikiwa na mitume na wazee wa Yerusalemu. Wakawaambia wazitii kanuni hizo. 5 Hivyo makanisa yakawa yanaongezeka katika imani, na idadi ya waamini iliongezeka kila siku.
Paulo Aitwa Makedonia
6 Paulo na wale waliokuwa pamoja naye walisafiri kwa kupita katika maeneo ya Frigia na Galatia kwa sababu Roho Mtakatifu hakuwaruhusu kuzihubiri Habari Njema katika jimbo la Asia. 7 Walipofika kwenye mpaka wa Misia, walijaribu kwenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu kwenda huko. 8 Hivyo wakapita Misia na kwenda katika mji wa Troa.
© 2017 Bible League International