Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Book of Common Prayer

Daily Old and New Testament readings based on the Book of Common Prayer.
Duration: 861 days
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Version
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Sir for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Ufunuo 7:1-8

Watu 144,000 wa Israeli

Baada ya hili kutokea, niliwaona malaika wanne wamesimama kwenye pembe nne za dunia wakiwa wamezishikilia pepo nne za dunia. Walikuwa wanazuia upepo kupuliza katika nchi au katika bahari au kwenye mti wowote. Kisha nikaona malaika mwingine akija akitokea upande wa mashariki. Malaika huyu alikuwa na muhuri wa Mungu aliye hai. Malaika akawaita kwa sauti kuu malaika wale wanne. Malaika hawa wanne walikuwa malaika ambao Mungu amewapa mamlaka ya kuidhuru dunia na bahari. Malaika akawaambia, “Msiidhuru nchi au bahari au miti kabla hatujawawekea alama kwenye vipaji vya nyuso zao wale wanaomtumikia Mungu wetu.”

Kisha nikasikia idadi ya watu wenye alama ya Mungu kwenye vipaji vya nyuso zao. Walikuwa watu 144,000. Walitoka katika kila kabila la Israeli:

Kutoka katika kabila la Yuda walikuwa elfu kumi na mbili

Kutoka katika kabila la Rubeni walikuwa elfu kumi na mbili

Kutoka katika kabila la Gadi walikuwa elfu kumi na mbili

Kutoka katika kabila la Asheri walikuwa elfu kumi na mbili

Kutoka katika kabila la Naftali walikuwa elfu kumi na mbili

Kutoka katika kabila la Manasse walikuwa elfu kumi na mbili

Kutoka katika kabila la Simeoni walikuwa elfu kumi na mbili

Kutoka katika kabila la Lawi walikuwa elfu kumi na mbili

Kutoka katika kabila la Isakari walikuwa elfu kumi na mbili

Kutoka katika kabila la Zabuloni walikuwa elfu kumi na mbili

Kutoka katika kabila la Yusufu walikuwa elfu kumi na mbili

Kutoka katika kabila la Benjamini walikuwa elfu kumi na mbili.

Luka 9:51-62

Katika Mji wa Samaria

51 Wakati ulikuwa unakaribia ambapo Yesu alikuwa aondoke na kurudi mbinguni. Hivyo aliamua kwenda Yerusalemu. 52 Alituma baadhi ya watu kumtangulia. Waliondoka na kwenda katika mji mmoja wa Samaria, ili kumwandalia mahali pa kufikia. 53 Lakini watu katika mji huo hawakumkaribisha Yesu kwa sababu alikuwa anakwenda Yerusalemu. 54 Wafuasi wake; Yakobo na Yohana walipoona hayo, wakasema, “Bwana, unataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni na kuwateketeza watu hawa?”[a]

55 Lakini Yesu aligeuka na akawakemea baada ya wao kusema hivi.[b] 56 Kisha Yesu na wanafunzi wake wakaondoka wakaenda katika mji mwingine.

Kumfuata Yesu

(Mt 8:19-22)

57 Walipokuwa wakisafiri pamoja njiani, mtu mmoja akamwambia Yesu, “Nitakufuata kokote utakakokwenda.”

58 Yesu akamwambia, “Mbweha wana mapango na ndege wa angani wana viota. Lakini Mwana wa Adamu hana mahali pa kulaza kichwa chake.”

59 Yesu akamwambia mtu mwingine, “Nifuate!”

Lakini mtu yule akamwambia, “Bwana, niache nikamzike baba yangu kwanza.”

60 Lakini Yesu akamwambia, “Waache waliokufa wawazike wafu wao. Ni lazima uende kuhubiri kuhusu Ufalme wa Mungu.”

61 Mtu mwingine pia akamwambia, “Nitakufuata Bwana, lakini niruhusu kwanza nikaiage familia yangu.”

62 Yesu akamwambia, “Mtu yeyote anayeanza kulima, kisha akaangalia nyuma hajajiandaa kwa ajili ya Ufalme wa Mungu.”

Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)

© 2017 Bible League International