Book of Common Prayer
12 Ndipo kundi lote likawa kimya. Waliwasikiliza Paulo na Barnaba walipokuwa wanaeleza kuhusu ishara na maajabu ambayo kupitia wao Mungu aliwatendea watu wasio Wayahudi. 13 Walipomaliza kusema, Yakobo akasema, “Ndugu zangu, nisikilizeni. 14 Simoni Petro ametueleza namna ambavyo siku za mwanzoni Mungu alilionyesha pendo lake kwa watu wasio Wayahudi, kwa kuwakubali na kuwafanya kuwa watu wake. 15 Maneno ya manabii yanakubaliana na hili:
16 ‘Nitarudi baada ya hili.
Nitaijenga nyumba ya Daudi tena.
Imeanguka chini.
Nitazijenga tena sehemu za nyumba yake zilizoangushwa chini.
Nitaifanya nyumba yake kuwa mpya.
17 Kisha wanadamu wengine wote,
watu niliowachagua kutoka mataifa mengine,
watataka kunifuata mimi, Bwana.
Hivi ndivyo Bwana anasema,
naye ndiye afanyaye mambo haya yote.’(A)
18 ‘Haya yote yalijulikana tangu zamani.’[a]
19 Hivyo nadhani tusiyafanye mambo kuwa magumu kwa wasio Wayahudi waliomgeukia Mungu. 20 Badala yake, tuwatumie barua kuwaambia mambo ambayo hawapaswi kutenda:
Wasile chakula kilichotolewa kwa sanamu maana chakula hiki huwa najisi.[b]
Wasijihusishe na dhambi ya zinaa.
Wasile nyama inayotokana na wanyama walionyongwa au nyama ambayo bado ina damu ndani yake.
21 Wasitende mojawapo ya mambo haya, kwa sababu bado kuna watu katika kila mji wanaofundisha Sheria ya Musa. Maneno ya Musa yamekuwa yakisomwa katika masinagogi kila siku ya Sabato kwa miaka mingi.”
30 Yesu hakuwa amefika kijijini. Alikuwa bado yupo pale pale Martha alipomkuta. 31 Wayahudi waliokuwepo nyumbani hapo wakimfariji Mariamu walimwona akiinuka na kuondoka ghafla. Walifikiri alikuwa anaenda kaburini kuomboleza. Hivyo wakamfuata. 32 Mariamu alienda pale Yesu alipokuwa. Naye baada ya kumwona, aliinama miguuni pake Yesu na kusema, “Bwana, kama ungekuwa hapa, kaka yangu asingekufa.”
33 Ndipo Yesu alipomwona Mariamu na watu waliokuwa pamoja naye wakilia, akahuzunika na kusikitika sana. 34 Akawauliza, “Mmemweka wapi?”
Wakasema, “Bwana, njoo uone.”
35 Yesu akalia na kutoa machozi.
36 Na Wayahudi wakasema, “Angalia! Alikuwa anampenda sana Lazaro!”
37 Lakini wengine wao wakasema, “Yesu aliyeyaponya macho ya yule mtu asiyeona kwa nini hakumsaidia Lazaro na kumzuia asife?”
Yesu Amfufua Lazaro Kutoka Mautini
38 Akiwa bado ana uchungu na kusikitika sana, Yesu akaenda kaburini. Kaburi lenyewe lilikuwa ni pango lenye jiwe kubwa lililofunika pa kuingilia. 39 Yesu akasema, “Lisogezeni pembeni hilo jiwe.”
Martha akasema, “Lakini, Bwana, ni siku nne[a] sasa tangu Lazaro alipofariki. Kutakuwa na harufu mbaya.” Martha alikuwa ni dada wa marehemu.
40 Kisha Yesu akamwambia Martha, “Unakumbuka jinsi nilivyokuambia? Je, sikukuambia kwamba kama ukiamini, ungeuona utukufu wa Mungu?”
41 Kwa hiyo wakalisogeza lile jiwe kutoka kwenye sehemu ya kuingilia. Kisha Yesu akatazama juu na kusema, “Baba, Nakushukuru kwa kuwa ulinisikia. 42 Najua kuwa siku zote unanisikia. Lakini nimeyasema mambo haya kwa ajili ya watu walioko hapa. Nataka kwamba waweze kuamini kuwa ni wewe uliyenituma.” 43 Baada ya Yesu kusema hivi akaita kwa sauti kubwa, “Lazaro, toka nje!” 44 Yule mtu aliyekuwa amekufa akatoka nje, mikono na miguu yake ilikuwa imefungwa sanda. Uso wake ulikuwa umefunikwa kwa kitambaa.
Yesu akawaambia watu, “Mfungueni hizo sanda na kumwacha aende.”
© 2017 Bible League International