Read the Gospels in 40 Days
13 Wakati huo, watu fulani walimwambia Yesu habari za Wagali laya ambao Pilato aliwaua na damu yao akaichanganya na damu ya sadaka waliyokuwa wakimtolea Mungu. 2 Yesu akawajibu, “Mnadhani Wagalilaya hao walikufa kifo cha namna hiyo kwa kuwa walikuwa na dhambi kuwazidi Wagalilaya wengine wote? 3 Sivyo hata kidogo. Ninyi pia msipoacha dhambi zenu mtaangamia vivyo hivyo. 4 Au wale watu kumi na wanane ambao walikufa walipoangukiwa na mnara huko Siloamu, mnadhani wao walikuwa waovu kuliko watu wote waliokuwa wanaishi Yerusalemu? 5 Nawaambieni, sivyo! Ninyi pia msipoacha dhambi zenu, mtaangamia vivyo hivyo.”
Mfano Wa Mti Usiozaa Matunda
6 Kisha Yesu akatoa mfano huu: “Mtu mmoja alikuwa na mtini uliopandwa katika shamba lake la mizabibu, akaenda kutafuta tini kwenye mti huo asipate hata moja. 7 Kisha akamwambia mtunza shamba:, ‘Kwa muda wa miaka mitatu sasa nimekuwa nikija kutafuta matunda kwenye mtini huu, sijawahi kupata hata moja. Ukate, sioni kwa nini uendelee kutumia ardhi bure!’ 8 Yule mtunza shamba akam jibu, ‘Bwana, tuuache tena kwa mwaka mmoja zaidi, niulimie, niuwekee mbolea. 9 Ukizaa matunda, vema; na usipozaa baada ya hapo, utaukata.”’ Yesu Amponya Mwanamke Siku Ya Sabato
10 Siku moja ya sabato, Yesu alikuwa akifundisha katika sinagogi mojawapo. 11 Na hapo alikuwapo mwanamke mmoja alikuwa ameugua kwa muda wa miaka kumi na minane kutokana na pepo ali yekuwa amemwingia. Hali hiyo ilimfanya mwanamke huyo apindike hata asiweze kusimama wima. 12 Yesu alipomwona, akamwita akam wambia, “Mama, uwe huru, umepona ugonjwa wako.” 13 Yesu akamwekea mikono, na mara akasimama wima, akamtukuza Mungu. 14 Mkuu wa sinagogi akakasirika kwa kuwa Yesu alikuwa ameponya mtu siku ya sabato. Kwa hiyo akawaambia watu, “Kuna siku sita ambazo watu wanapaswa kufanya kazi, katika siku hizo, njooni mpo nywe; msije kuponywa siku ya sabato!”
15 Lakini Bwana akamjibu, “Ninyi ni wanafiki! Kila mmoja wenu humfungulia ng’ombe wake au punda wake kutoka zizini akampeleka kumnywesha maji siku ya sabato. 16 Je, huyu mama, ambaye ni binti wa Ibrahimu aliyefungwa na shetani kwa miaka yote hii kumi na minane, hastahili kufunguliwa kutoka katika kifungo hicho siku ya sabato?” 17 Aliposema haya, wapinzani wake wakaona aibu lakini watu wakafurahi kwa ajili ya mambo ya ajabu aliyoyafanya. Mfano Wa Punje Ya Haradali
18 Kisha Yesu akauliza, “Ufalme wa Mungu ukoje? Nitaufanan isha na nini? 19 Umefanana na punje ndogo sana ya haradali ambayo mtu aliichukua akaipanda katika shamba lake, ikamea, ikawa mti na ndege wa angani wakatengeneza viota vyao kwenye matawi yake.”
Mfano Wa Hamira
20 Yesu akauliza tena, “Nitaufananisha na nini Ufalme wa Mungu? 21 Uko kama hamira ambayo mwanamke aliichukua na kuichan ganya kwenye vipimo vitatu vya unga wa ngano na wote ukaumuka.”
Mlango Mwembamba
22 Yesu akapita katika miji na vijiji akifundisha wakati akisafiri kwenda Yerusalemu. 23 Mtu mmoja akamwuliza, “Bwana, ni watu wachache tu watakaookolewa?” 24 Akajibu, “Jitahidini kuingia kwa kupitia mlango mwembamba; kwa maana, nawaambia, wengi watataka kuingia na hawataweza. 25 Wakati mwenye nyumba ataka poamka na kufunga mlango, mtasimama nje mkigonga mlango na kusema, ‘Bwana utufungulie!’ Atawajibu, ‘Sijui mtokako!’ 26 Nanyi mtamjibu, ‘Tulikula na kunywa pamoja nawe, ulifundisha katika mitaa yetu!’ 27 Lakini yeye atawajibu, ‘Sijui mtokako. Ondokeni kwangu ninyi watenda maovu!’ 28 Ndipo kutakuwapo na kilio na kusaga meno mtakapomwona Ibrahimu, Isaka na Yakobo na manabii wote wakiwa katika Ufalme wa Mungu, wakati ninyi mkiwa mmetupwa nje. 29 Watu watakuja kutoka mashariki na magharibi na kaskazini na kusini na wataketi kwenye sehemu walizoandaliwa kar amuni katika Ufalme wa Mungu. 30 Hakika wapo watu ambao sasa wako mwisho watakaokuwa wa kwanza, na wengine walio wa kwanza sasa watakaokuwa wa mwisho.” Yesu Aomboleza Juu Ya Yerusalemu
31 Wakati huo huo baadhi ya Mafarisayo wakamwendea Yesu wakamwambia, “Ondoka hapa uende mahali pengine kwa maana Herode anataka kukuua.” 32 Yesu akawajibu, “Nendeni mkamwambie yule mbweha: ninafukuza pepo na kuponya wagonjwa leo na kesho, na siku ya tatu nitakamilisha kazi yangu. 33 Sina budi kuendelea na safari yangu leo, kesho na kesho kutwa, kwa maana haiwezekani nabii kufa mahali pengine isipokuwa Yerusalemu.
34 “Ewe Yerusalemu, Yerusalemu, wewe uwauaye manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetamani kuwa kusanya watoto wako pamoja kama kuku akusanyavyo vifaranga vyake chini ya mbawa zake, lakini hukuniruhusu! 35 Sasa nyumba yako inaachwa tupu. Ninakuambia, hutaniona tena mpaka wakati ule uta kaposema, ‘Amebarikiwa yeye ajaye katika jina la Bwana.”’
14 Siku moja ya sabato Yesu alipokuwa amekwenda kula chakula kwa mmoja wa viongozi wa Mafarisayo, watu walikuwa wakimtazama kwa makini. 2 Mtu mmoja mwenye ugonjwa wa kuvimba miguu na mikono akaja mbele yake. 3 Yesu akawauliza walimu wa sheria na Mafari sayo, “Je, sheria inaruhusu kumponya mtu siku ya sabato au hairuhusu?” 4 Wakakaa kimya. Basi Yesu akamshika yule mgonjwa akamponya, akamruhusu aende zake. 5 Kisha akawauliza, “Kama mmoja wenu angekuwa na mtoto au ng’ombe wake ambaye ametumbukia katika kisima siku ya sabato, hamtamvuta mara moja na kumtoa?” 6 Hawakuwa na la kujibu.
7 Alipoona jinsi wageni walioalikwa walivyokuwa wakichagua viti vya wageni wa heshima, akawaambia mfano huu: 8 “Mtu akiku alika harusini, usikae kwenye kiti cha mgeni wa heshima. Inaweze kana kuwa amealika mheshimiwa akuzidiye, 9 na yule aliyewaalika ninyi wawili akaja kukuambia, ‘Tafadhali mpishe huyu bwana.’ Ndipo kwa aibu utalazimika kwenda kukaa katika kiti cha nyuma kabisa. 10 Badala yake, unapoalikwa, chagua kiti cha nyuma; na mwenyeji wako akikuona atakuja akuambie, ‘Rafiki yangu, njoo kwe nye nafasi ya mbele zaidi.’ Kwa jinsi hii utakuwa umepewa heshima mbele ya wageni wote. 11 Kwa maana kila mtu anayejitukuza atash ushwa naye ajishushaye atatukuzwa.”
12 Kisha Yesu akamwambia yule aliyewaalika, “Uandaapo kar amu ya chakula cha mchana au jioni, usialike rafiki zako au ndugu zako au jamaa zako au majirani zako tajiri; ukifanya hivyo wao nao watakualika kwao na hivyo utakuwa umelipwa kwa kuwaalika. 13 Bali ufanyapo karamu, waalike maskini, vilema na vipofu; 14 nawe utapata baraka kwa sababu hawa hawana uwezo wa kukulipa.
Mfano Wa Karamu Ya Ufalme Wa Mbinguni
15 Mmoja wa wale waliokuwa mezani pamoja naye aliposikia maneno haya akamwambia, “Ana heri mtu atakayepata nafasi ya kula katika karamu ya Ufalme wa Mbinguni!” 16 Yesu akamjibu, ‘ ‘Mtu mmoja alikuwa anaandaa karamu kubwa, akaalika watu wengi. 17 Wakati wa sherehe ulipofika, akamtuma mtumishi wake akawaam bie walioalikwa, ‘Karibuni, kila kitu ni tayari sasa.’ 18 Lakini wote, mmoja mmoja, wakaanza kutoa udhuru. Wa kwanza akasema, ‘ Nimenunua shamba, lazima niende kuliona. Tafadhali niwie radhi.’ 19 Mwingine akasema, ‘Nimenunua ng’ombe wa kulimia, jozi tano; nimo njiani kwenda kuwajaribu, tafadhali niwie radhi.’ 20 Na mwingine akasema, ‘Nimeoa mke, kwa hiyo siwezi kuja.’
21 “Yule mtumishi akarudi, akampa bwana wake taarifa. Ndipo yule mwenye nyumba akakasirika, akamwambia mtumishi wake, ‘Nenda upesi kwenye mitaa na vichochoro vya mjini uwalete maskini, vilema, vipofu na viwete.’
22 “Baadaye yule mtumishi akamwambia ‘Bwana, yale uliyon iagiza nimefanya, lakini bado ipo nafasi.’ 23 Ndipo yule bwana akamwambia mtumishi wake, ‘Nenda kwenye barabara na njia zilizoko nje ya mji uwalazimishe watu waje mpaka nafasi zote zijae. 24 Ninawaambia, hakuna hata mmoja wa wale niliowapelekea mwaliko rasmi atakayeionja karamu yangu.”
Gharama Ya Kuwa Mfuasi Wa Yesu
25 Wakati mmoja umati mkubwa wa watu ulipokuwa ukifuatana na Yesu, yeye aligeuka, akawaambia, 26 “Mtu ye yote anayekuja kwangu hawezi kuwa mfuasi wangu kama hatanipenda mimi zaidi ya baba yake na mama yake, mke wake na watoto, kaka zake na dada zake; naam, hata maisha yake mwenyewe. 27 Na ye yote asiyebeba msalaba wake na kunifuata hawezi kuwa mfuasi wangu.
28 “Ni nani kati yenu ambaye kama anataka kujenga, hatakaa kwanza na kufanya makisio ya gharama aone kama ana fedha za kutosha kukamilisha ujenzi? 29 Kwa maana ikiwa atajenga msingi halafu ashindwe kuendelea, wote watakaouona watamcheka 30 wakisema, ‘Mtu huyu alianza kujenga lakini ameshindwa kumal iza!’
31 “Au tuseme mfalme mmoja anataka kwenda vitani kupigana na mfalme mwingine: si atakaa kwanza ajishauri kama yeye na jeshi lake lenye watu elfu kumi ataweza kupigana na yule anayekuja na watu elfu ishirini? 32 Kama hawezi, basi itambidi apeleke wajumbe wakati yule mfalme mwingine bado yuko mbali na kuomba masharti ya amani. 33 Hali kadhalika, hakuna mtu atakayeweza kuwa mfuasi wangu kama hataacha vyote alivyo navyo.”
Chumvi Isiyofaa
34 “Chumvi ni kitu kizuri. Lakini chumvi ikiwa imepoteza ladha yake, haiwezi kuwa chumvi tena. 35 Haifai kuwa udongo wala kuwa mbolea; watu huitupa nje. Mwenye nia ya kusikia na asikie!” Mfano Wa Kondoo Aliyepotea
Copyright © 1989 by Biblica