Mfano Wa Karamu Ya Harusi

22 Yesu akazungumza nao tena kwa kutumia mifano, akasema, “Ufalme wa mbinguni unaweza kufananishwa na mfalme mmoja ali yemwandalia mwanae karamu ya harusi. Akawatuma watumishi wake wakawaite wageni walioalikwa lakini wakakataa kuja. Akawatuma watumishi wengine akisema, ‘Waambieni waalikwa kwamba karamu iko tayari, nimekwisha chinja fahali wangu na ng’ombe wanono kwa ajili yenu, karibuni karamuni.’ Lakini waalikwa wakadharau, mmoja akaenda shambani kwake, mwingine akaenda kwenye miradi yake, na wengine wakawakamata wale watumishi wakawatendea mambo ya aibu na kuwaua.

“Yule mfalme akakasirika, akapeleka jeshi lake likawaanga miza wale wauaji na kuteketeza mji wao. Kisha akawaambia watum ishi wake, ‘Karamu ya harusi ni tayari, lakini wale niliowaalika hawakustahili kuja karamuni. Kwa hiyo nendeni katika njia panda mkawaalike harusini wote mtakaowakuta.’ 10 Wale watumishi wakaenda mabarabarani wakawakusanya wote waliowakuta, wema na wabaya. Ukumbi wa sherehe ya harusi ukajaa wageni.

11 “Lakini mfalme alipoingia kutazama wageni, alimwona mle ndani mtu mmoja ambaye hakuwa amevaa vazi la harusi. 12 Mfalme akamwuliza, ‘Rafiki, umeingiaje humu bila vazi la harusi?’ Yule mtu hakuwa na la kusema. 13 Basi mfalme akawaambia watumishi wake, ‘Mfungeni mikono na miguu mkamtupe nje kwenye giza. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.’ 14 Kwa maana walioitwa ni wengi lakini walioteuliwa ni wachache.”

Kuhusu Kulipa Kodi

15 Mafarisayo walifanya mbinu za kumtega Yesu katika mafundi sho yake. 16 Wakatuma wanafunzi wao pamoja na Maherode wakam wambie, “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu wa haki na unafundisha njia za Mungu kwa uaminifu bila kumjali mtu, kwa maana cheo si kitu kwako. 17 Basi tuambie, wewe unaonaje? Ni halali, au si halali kulipa kodi kwa Kaisari?”

18 Yesu alifahamu hila yao kwa hiyo akawaambia, “Ninyi wanafiki, kwa nini mnajaribu kunitega? 19 Nionyesheni sarafu mnayolipia kodi.” Wakamletea sarafu. 20 Yesu akawauliza, “Picha hii na sahihi hii ni za nani?” 21 Wakamjibu, “Ni za Kaisari.” Basi Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari yaliyo ya Kais ari; na ya Mungu mpeni Mungu.”

22 Waliposikia haya wakashangaa; wakamwacha, wakaondoka.

Ufufuo Wa Wafu

23 Siku hiyo hiyo Masadukayo, wale wanaoamini kwamba wafu hawafufuki, walikuja kwa Yesu wakamwuliza, 24 “Mwalimu, Musa alitufundisha kwamba mtu akifariki pasipo kupata watoto, ndugu yake amwoe huyo mjane ili ampatie kaka yake watoto. 25 Hapa kwetu walikuwapo ndugu saba. Wa kwanza alioa mke, kisha akafariki na kwa kuwa hakuwa na watoto, yule mjane alichukuliwa na ndugu yake. 26 Ikatokea hivyo hivyo kwa yule ndugu wa pili hadi wote saba wakamwoa huyo mjane bila kupata watoto. 27 Baadaye, yule mjane naye akafariki. 28 Sasa tuambie, siku ile ya ufufuo, ata hesabiwa kuwa ni mke wa nani? Maana aliolewa na wote saba!”

29 Yesu akawajibu, “Mnakosea kwa sababu hamjui Maandiko wala uwezo wa Mungu. 30 Wakati wa ufufuo, watu hawataoa wala kuolewa; kwa maana watakuwa kama malaika wa mbinguni. 31 Na kuhusu ufufuo wa wafu, hamjasoma Mungu alivyowaambia kwamba, 32 ‘Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo’? Yeye si Mungu wa wafu bali ni Mungu wa walio hai.”

33 Ule umati wa watu waliposikia hayo, walishangazwa sana na mafund isho yake.

Amri Kuu Kuliko Zote

34 Mafarisayo waliposikia kwamba Yesu alikuwa amewanyamazi sha Masadukayo, walikutana wakamjia pamoja. 35 Mmoja wao, mtaalamu wa sheria akajaribu kumtega kwa kumwuliza, 36 “Mwali mu, ni amri ipi iliyo kuu kuliko zote?”

37 Yesu akamjibu, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote.’ 38 Hii ndio amri kuu, tena ni ya kwanza. 39 Na ya pili inafanana nayo, nayo ni hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’ 40 Amri hizi mbili ndio msingi wa sheria zote na Maandiko ya manabii.”

Kristo Ni Mwana Na Bwana Wa Daudi

41 Mafarisayo walipokuwa pamoja Yesu aliwauliza, 42 “Mnaonaje kuhusu Kristo? Yeye ni mwana wa nani?” Wakamjibu, “Yeye ni mwana wa Daudi.”

43 Akawaambia, “Inakuwaje basi kwamba Daudi anapozungumza kwa Roho anamwita Kristo ‘Bwana,’ kwa kusema, 44 ‘Bwana alimwam bia Bwana wangu: keti upande wangu wa kulia mpaka nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.’ 45 Kama Daudi anamwita ‘Bwana 46 Hakuna aliyeweza kumjibu Yesu hata neno moja. Na tangu siku hiyo hakuna aliyethubutu tena kum wuliza maswali.

The Parable of the Wedding Feast

22 And again Jesus (A)spoke to them in parables, saying, (B)“The kingdom of heaven may be compared to a king who gave (C)a wedding feast for his son, and (D)sent his servants[a] to call those who were invited to the wedding feast, but they would not come. (E)Again he sent other servants, saying, ‘Tell those who are invited, “See, I have prepared my (F)dinner, (G)my oxen and my fat calves have been slaughtered, and everything is ready. Come to the wedding feast.”’ But (H)they paid no attention and went off, one to his farm, another to his business, while the rest seized his servants, (I)treated them shamefully, and (J)killed them. The king was angry, and he sent his troops and (K)destroyed those murderers and burned their city. Then he said to his servants, ‘The wedding feast is ready, but those invited were not (L)worthy. Go therefore to the main roads and invite to the wedding feast as many as you find.’ 10 And those servants went out into the roads and (M)gathered all whom they found, both bad and good. So the wedding hall was filled with guests.

11 “But when the king came in to look at the guests, he saw there (N)a man who had no wedding garment. 12 And he said to him, (O)‘Friend, how did you get in here without a wedding garment?’ And he was speechless. 13 Then the king said to the attendants, ‘Bind him hand and foot and (P)cast him into the outer darkness. In that place (Q)there will be weeping and gnashing of teeth.’ 14 For many are (R)called, but few are (S)chosen.”

Paying Taxes to Caesar

15 (T)Then the Pharisees went and plotted how (U)to entangle him in his words. 16 And they sent (V)their disciples to him, along with (W)the Herodians, saying, “Teacher, (X)we know that you are true and teach (Y)the way of God truthfully, and you do not care about anyone's opinion, for (Z)you are not swayed by appearances.[b] 17 Tell us, then, what you think. Is it lawful to pay (AA)taxes to (AB)Caesar, or not?” 18 But Jesus, aware of their malice, said, “Why (AC)put me to the test, you hypocrites? 19 Show me the coin for the tax.” And they brought him a denarius.[c] 20 And Jesus said to them, “Whose likeness and inscription is this?” 21 They said, “Caesar's.” Then he said to them, (AD)“Therefore render to Caesar the things that are Caesar's, and to God the things that are God's.” 22 When they heard it, they marveled. And they (AE)left him and went away.

Sadducees Ask About the Resurrection

23 The same day (AF)Sadducees came to him, (AG)who say that there is no resurrection, and they asked him a question, 24 saying, “Teacher, Moses said, (AH)‘If a man dies having no children, his brother must marry the widow and raise up offspring for his brother.’ 25 Now there were seven brothers among us. The first married and died, and having no offspring left his wife to his brother. 26 So too the second and third, down to the seventh. 27 After them all, the woman died. 28 In the resurrection, therefore, of the seven, whose wife will she be? For they all had her.”

29 But Jesus answered them, “You are wrong, (AI)because you know neither the Scriptures nor (AJ)the power of God. 30 For in the resurrection they neither (AK)marry nor (AL)are given in marriage, but are like angels in heaven. 31 And as for the resurrection of the dead, (AM)have you not read what was said to you by God: 32 (AN)‘I am the God of Abraham, and the God of Isaac, and the God of Jacob’? He is not God of the dead, but of the living.” 33 And when the crowd heard it, (AO)they were astonished at his teaching.

The Great Commandment

34 (AP)But when the Pharisees heard that he had silenced (AQ)the Sadducees, they gathered together. 35 (AR)And one of them, (AS)a lawyer, asked him a question (AT)to test him. 36 “Teacher, which is the great commandment in the Law?” 37 And he said to him, (AU)“You shall love the Lord your God with all your heart and with all your soul and with all your mind. 38 This is the great and first commandment. 39 And (AV)a second is like it: (AW)You shall love your neighbor as yourself. 40 (AX)On these two commandments depend (AY)all the Law and the Prophets.”

Whose Son Is the Christ?

41 (AZ)Now while the Pharisees (BA)were gathered together, Jesus asked them a question, 42 saying, “What do you think about (BB)the Christ? Whose son is he?” They said to him, (BC)“The son of David.” 43 He said to them, “How is it then that David, (BD)in the Spirit, calls him Lord, saying,

44 (BE)“‘The Lord said to my Lord,
“Sit at my right hand,
    until I put your enemies under your feet”’?

45 If then David calls him Lord, (BF)how is he his son?” 46 (BG)And no one was able to answer him a word, (BH)nor from that day did anyone dare to ask him any more questions.

Footnotes

  1. Matthew 22:3 Or bondservants; also verses 4, 6, 8, 10
  2. Matthew 22:16 Greek for you do not look at people's faces
  3. Matthew 22:19 A denarius was a day's wage for a laborer