Luka 24
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yesu Amefufuka Kutoka Mauti
(Mt 28:1-10; Mk 16:1-8; Yh 20:1-10)
24 Asubuhi mapema sana siku ya Jumapili, wanawake walikwenda kaburini ulikolazwa mwili wa Yesu. Walibeba manukato yanayonukia vizuri waliyoyaandaa. 2 Walikuta jiwe kubwa lililokuwa limeziba mlango wa kaburi limevingirishwa kutoka kwenye mlango wa kaburi. 3 Waliingia kaburini, lakini hawakuuona mwili wa Bwana Yesu. 4 Hawakulielewa hili. Walipokuwa wangali wanashangaa, watu wawili waliovaa mavazi yaliyong'aa walisimama pembeni mwao. 5 Wanawake waliogopa sana. Waliinama nyuso zao zikaelekea chini. Wale watu wakawaambia, “Kwa nini mnamtafuta aliye hai hapa? Hapa ni mahali pa waliokufa. 6 Yesu hayuko hapa. Amefufuka kutoka kwa wafu. Mnakumbuka alivyosema alipokuwa Galilaya? 7 Alisema kwamba, ‘Mwana wa Adamu lazima atatolewa kwa mamlaka ya watu wenye dhambi, lazima atauawa msalabani na kufufuka kutoka kwa wafu siku ya tatu.’” 8 Ndipo wanawake wakakumbuka Yesu alivyosema.
9 Wanawake wakaondoka kaburini na kurudi kwa mitume kumi na mmoja na wafuasi wengine. Waliwaeleza kila kitu kilichotokea kaburini. 10 Wanawake hawa walikuwa Mariamu Magdalena, Yoana, na Mariamu, mama yake Yakobo na wanawake wengine. Waliwaambia mitume kila kitu kilichotokea. 11 Lakini mitume hawakuamini yale waliyosema. Ilionekana kama upuuzi. 12 Lakini Petro alinyanyuka na kukimbia kwenda kaburini kuona. Alitazama ndani, lakini aliona nguo tu iliyotumika kuufunga mwili wa Yesu. Petro aliondoka kwenye kaburi akarudi nyumbani alikokuwa anakaa, akijiuliza nini kilichotokea.[a]
Njiani Kwenda Emausi
(Mk 16:12-13)
13 Siku hiyo hiyo, wafuasi wawili[b] wa Yesu walikuwa wanakwenda kwenye mji mdogo uitwao Emausi, uliokuwa yapata kilomita kumi na mbili[c] kutoka Yerusalemu. 14 Walikuwa wanazungumza kuhusu mambo yote yaliyotokea. 15 Walipokuwa wakizungumza, wakijadiliana juu ya mambo haya, Yesu mwenyewe aliwasogelea na akawa anatembea nao. 16 Lakini hawakuruhusiwa kumtambua. 17 Yesu akawauliza, “Ni mambo gani ninayosikia mnajadiliana mnapotembea?”
Wale wafuasi wawili wakasimama, sura zao zilionekana zenye huzuni. 18 Mmoja wao, aliyeitwa Kleopa akasema, “Lazima wewe ni mtu pekee katika Yerusalemu ambaye hujui yaliyotokea huko.”
19 Yesu akasema, “Unasema kuhusu nini?”
Wakasema, “Ni kuhusu Yesu, kutoka Nazareti, alikuwa nabii mkuu mbele za Mungu na watu wote. Alisema na kutenda mambo makuu mengi. 20 Lakini viongozi wetu na viongozi wa makuhani walimtoa ili ahukumiwe na kuuawa. Wakampigilia msalabani. 21 Tulitegemea kuwa ndiye atakayeiweka huru Israeli. Lakini sasa haya yote yametokea.
Na sasa kitu kingine: Imekuwa ni siku tatu tangu alipouawa, 22 lakini leo baadhi ya wanawake kutoka kwenye kundi letu walituambia jambo la kushangaza. Mapema asubuhi hii walikwenda kaburini ambako mwili wa Yesu ulilazwa. 23 Lakini hawakuuona mwili wake pale. Walikuja na kutuambia kuwa wamewaona malaika. Malaika waliwaambia Yesu yu hai! 24 Hivyo baadhi ya watu walio katika kundi letu walikwenda kaburini pia. Ilikuwa kama wanawake walivyosema. Waliliona kaburi, lakini hawakumwona Yesu.”
25 Ndipo Yesu akawaambia, “Ninyi ni wajinga na wazito wa kuyakubali yale waliyoandika manabii. 26 Manabii waliandika kwamba Masihi lazima ateseke kwa mambo haya kabla hajaingia katika utukufu wa ufalme wake.” 27 Kisha akaanza kufafanua kila kitu walichosema manabii kuhusu yeye. Alianzia katika vitabu vya Musa na kusema yale waliyosema manabii kuhusu yeye.
28 Wakakaribia mji wa Emausi, na Yesu akafanya kama vile alikuwa anaendelea mbele. 29 Lakini walimtaka akae, wakamsihi: “Kaa nasi. Tayari ni usiku. Mchana unakaribia kwisha.” Hivyo aliingia ndani kukaa nao.
30 Alipokuwa mezani pamoja nao ili kula chakula cha usiku, Yesu akachukua mkate na kushukuru. Kisha akaumega na kuwapa. 31 Baada ya kufanya hivyo, wafuasi wale wawili wakaruhusiwa kumtambua. Lakini walipojua yeye ni nani, alitoweka. 32 Wakasemezana, “Alivyokuwa anazungumza nasi tulipokuwa barabarani, tulijisikia kama moto unawaka ndani yetu. Ilitusisimua sana alipotufafanulia maana halisi ya Maandiko!”
33 Hivyo wafuasi wale wawili wa Bwana Yesu wakasimama na kurudi Yerusalemu haraka. Walipofika Yerusalemu waliwakuta mitume kumi na mmoja wamekusanyika pamoja na wafuasi wengine wa Bwana Yesu. 34 Kundi likawaambia wale wafuasi wawili, “Hakika Bwana amefufuka kutoka kwa wafu! Alimtokea Simoni.”
35 Ndipo wafuasi wawili wakaeleza kilichotokea barabarani. Wakaeleza jinsi walivyomtambua Yesu aliposhiriki mkate pamoja nao.
Yesu Awatokea Wafuasi Wake
(Mt 28:16-20; Mk 16:14-18; Yh 20:19-23; Mdo 1:6-8)
36 Wakati wafuasi wawili wakiwa bado wanawaeleza mambo haya wafuasi wengine, Yesu mwenyewe akaja na kusimama katikati yao. Akawaambia, “Amani iwe kwenu.”
37 Wafuasi walishituka na wakaogopa. Walidhani wanaona mzimu. 38 Lakini Yesu akasema, “Kwa nini mnaogopa? Na kwa nini mnakitilia mashaka kile mnachokiona? 39 Angalieni mikono na miguu yangu. Hakika ni mimi. Niguseni. Mtaweza kuona kuwa nina mwili wenye nyama na mifupa; mzimu hauna mwili kama huu.”
40 Mara baada ya Yesu kusema haya, aliwaonesha mikono na miguu yake. 41 Wafuasi walishangaa na kufurahi sana walipoona kuwa Yesu alikuwa hai. Kwa kuwa bado walikuwa hawaamini wanachokiona, akawaambia, “Mna chakula chochote hapa?” 42 Wakampa kipande cha samaki aliyepikwa. 43 Wafuasi wake wakiwa wanaangalia akakichukua na kukila.
44 Yesu akawaambia, “Mnakumbuka nilipokuwa pamoja nanyi? Nilisema kila kitu kilichoandikwa kuhusu mimi katika Sheria ya Musa, vitabu vya manabii na Zaburi lazima kitimilike.”
45 Kisha Yesu akawafafanulia Maandiko ili waelewe maana yake halisi. 46 Yesu akawaambia, “Imeandikwa kuwa Masihi atauawa na atafufuka kutoka kwa wafu siku ya tatu. 47-48 Mliona mambo haya yakitokea, ninyi ni mashahidi. Na maandiko yanasema inawapasa mwende na kuwahubiri watu kuwa ni lazima wabadilike na kumgeukia Mungu, ili awasamehe. Ni lazima mwanzie Yerusalemu na mhubiri ujumbe huu kwa jina langu kwa watu wa mataifa yote. 49 Kumbukeni kwamba nitamtuma kwenu yule ambaye Baba yangu aliahidi. Kaeni jijini mpaka mtakapopewa nguvu hiyo kutoka mbinguni.”
Yesu Arudi Mbinguni
(Mk 16:19-20; Mdo 1:9-11)
50 Yesu akawaongoza wafuasi wake kutoka nje ya Yerusalemu hadi karibu na Bethania. Akanyenyua mikono yake na kuwabariki wafuasi wake. 51 Alipokuwa anawabariki, alitenganishwa nao na kuchukuliwa mbinguni. 52 Wafuasi wake walimwabudu, kisha wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha sana. 53 Walikuwa katika Hekalu wakati wote, wakimsifu Mungu.
Footnotes
- 24:12 Nakala chache za Kiyunani hazina mstari huu.
- 24:13 wafuasi wawili Kwa maana ya kawaida, “Miongoni mwa wafuasi”. Ni wazi kutokana na simulizi kuwa wote wawili ni wafuasi wa Yesu, lakini mmoja wao tu ndiye anayetajwa jina (mstari wa 18). Inawezekana akawa ndiye Kleopa, anayeelezwa katika Yh 19:25 kama mume wa mmoja wa wanawake anayeitwa Mariamu. Inawezekama mfuasi wa pili anayezungumzwa hapa ndiye huyu Mariamu.
- 24:13 kilomita kumi na mbili Kwa Kiyunani umbali huo ni sawa na “stadia 60”.
Luke 24
New International Version
Jesus Has Risen(A)
24 On the first day of the week, very early in the morning, the women took the spices they had prepared(B) and went to the tomb. 2 They found the stone rolled away from the tomb, 3 but when they entered, they did not find the body of the Lord Jesus.(C) 4 While they were wondering about this, suddenly two men in clothes that gleamed like lightning(D) stood beside them. 5 In their fright the women bowed down with their faces to the ground, but the men said to them, “Why do you look for the living among the dead? 6 He is not here; he has risen! Remember how he told you, while he was still with you in Galilee:(E) 7 ‘The Son of Man(F) must be delivered over to the hands of sinners, be crucified and on the third day be raised again.’ ”(G) 8 Then they remembered his words.(H)
9 When they came back from the tomb, they told all these things to the Eleven and to all the others. 10 It was Mary Magdalene, Joanna, Mary the mother of James, and the others with them(I) who told this to the apostles.(J) 11 But they did not believe(K) the women, because their words seemed to them like nonsense. 12 Peter, however, got up and ran to the tomb. Bending over, he saw the strips of linen lying by themselves,(L) and he went away,(M) wondering to himself what had happened.
On the Road to Emmaus
13 Now that same day two of them were going to a village called Emmaus, about seven miles[a] from Jerusalem.(N) 14 They were talking with each other about everything that had happened. 15 As they talked and discussed these things with each other, Jesus himself came up and walked along with them;(O) 16 but they were kept from recognizing him.(P)
17 He asked them, “What are you discussing together as you walk along?”
They stood still, their faces downcast. 18 One of them, named Cleopas,(Q) asked him, “Are you the only one visiting Jerusalem who does not know the things that have happened there in these days?”
19 “What things?” he asked.
“About Jesus of Nazareth,”(R) they replied. “He was a prophet,(S) powerful in word and deed before God and all the people. 20 The chief priests and our rulers(T) handed him over to be sentenced to death, and they crucified him; 21 but we had hoped that he was the one who was going to redeem Israel.(U) And what is more, it is the third day(V) since all this took place. 22 In addition, some of our women amazed us.(W) They went to the tomb early this morning 23 but didn’t find his body. They came and told us that they had seen a vision of angels, who said he was alive. 24 Then some of our companions went to the tomb and found it just as the women had said, but they did not see Jesus.”(X)
25 He said to them, “How foolish you are, and how slow to believe all that the prophets have spoken! 26 Did not the Messiah have to suffer these things and then enter his glory?”(Y) 27 And beginning with Moses(Z) and all the Prophets,(AA) he explained to them what was said in all the Scriptures concerning himself.(AB)
28 As they approached the village to which they were going, Jesus continued on as if he were going farther. 29 But they urged him strongly, “Stay with us, for it is nearly evening; the day is almost over.” So he went in to stay with them.
30 When he was at the table with them, he took bread, gave thanks, broke it(AC) and began to give it to them. 31 Then their eyes were opened and they recognized him,(AD) and he disappeared from their sight. 32 They asked each other, “Were not our hearts burning within us(AE) while he talked with us on the road and opened the Scriptures(AF) to us?”
33 They got up and returned at once to Jerusalem. There they found the Eleven and those with them, assembled together 34 and saying, “It is true! The Lord(AG) has risen and has appeared to Simon.”(AH) 35 Then the two told what had happened on the way, and how Jesus was recognized by them when he broke the bread.(AI)
Jesus Appears to the Disciples
36 While they were still talking about this, Jesus himself stood among them and said to them, “Peace be with you.”(AJ)
37 They were startled and frightened, thinking they saw a ghost.(AK) 38 He said to them, “Why are you troubled, and why do doubts rise in your minds? 39 Look at my hands and my feet. It is I myself! Touch me and see;(AL) a ghost does not have flesh and bones, as you see I have.”
40 When he had said this, he showed them his hands and feet. 41 And while they still did not believe it because of joy and amazement, he asked them, “Do you have anything here to eat?” 42 They gave him a piece of broiled fish, 43 and he took it and ate it in their presence.(AM)
44 He said to them, “This is what I told you while I was still with you:(AN) Everything must be fulfilled(AO) that is written about me in the Law of Moses,(AP) the Prophets(AQ) and the Psalms.”(AR)
45 Then he opened their minds so they could understand the Scriptures. 46 He told them, “This is what is written: The Messiah will suffer(AS) and rise from the dead on the third day,(AT) 47 and repentance for the forgiveness of sins will be preached in his name(AU) to all nations,(AV) beginning at Jerusalem.(AW) 48 You are witnesses(AX) of these things. 49 I am going to send you what my Father has promised;(AY) but stay in the city until you have been clothed with power from on high.”
The Ascension of Jesus
50 When he had led them out to the vicinity of Bethany,(AZ) he lifted up his hands and blessed them. 51 While he was blessing them, he left them and was taken up into heaven.(BA) 52 Then they worshiped him and returned to Jerusalem with great joy. 53 And they stayed continually at the temple,(BB) praising God.
Footnotes
- Luke 24:13 Or about 11 kilometers
Luke 24
New King James Version
He Is Risen(A)
24 Now (B)on the first day of the week, very early in the morning, they, [a]and certain other women with them, came to the tomb (C)bringing the spices which they had prepared. 2 (D)But they found the stone rolled away from the tomb. 3 (E)Then they went in and did not find the body of the Lord Jesus. 4 And it happened, as they were [b]greatly perplexed about this, that (F)behold, two men stood by them in shining garments. 5 Then, as they were afraid and bowed their faces to the earth, they said to them, “Why do you seek the living among the dead? 6 He is not here, but is risen! (G)Remember how He spoke to you when He was still in Galilee, 7 saying, ‘The Son of Man must be (H)delivered into the hands of sinful men, and be crucified, and the third day rise again.’ ”
8 And (I)they remembered His words. 9 (J)Then they returned from the tomb and told all these things to the eleven and to all the rest. 10 It was Mary Magdalene, (K)Joanna, Mary the mother of James, and the other women with them, who told these things to the apostles. 11 (L)And their words seemed to them like [c]idle tales, and they did not believe them. 12 (M)But Peter arose and ran to the tomb; and stooping down, he saw the linen cloths [d]lying by themselves; and he departed, marveling to himself at what had happened.
The Road to Emmaus(N)
13 (O)Now behold, two of them were traveling that same day to a village called Emmaus, which was [e]seven miles from Jerusalem. 14 And they talked together of all these things which had happened. 15 So it was, while they conversed and reasoned, that (P)Jesus Himself drew near and went with them. 16 But (Q)their eyes were restrained, so that they did not know Him.
17 And He said to them, “What kind of conversation is this that you have with one another as you [f]walk and are sad?”
18 Then the one (R)whose name was Cleopas answered and said to Him, “Are You the only stranger in Jerusalem, and have You not known the things which happened there in these days?”
19 And He said to them, “What things?”
So they said to Him, “The things concerning Jesus of Nazareth, (S)who was a Prophet (T)mighty in deed and word before God and all the people, 20 (U)and how the chief priests and our rulers delivered Him to be condemned to death, and crucified Him. 21 But we were hoping (V)that it was He who was going to redeem Israel. Indeed, besides all this, today is the third day since these things happened. 22 Yes, and (W)certain women of our company, who arrived at the tomb early, astonished us. 23 When they did not find His body, they came saying that they had also seen a vision of angels who said He was alive. 24 And (X)certain of those who were with us went to the tomb and found it just as the women had said; but Him they did not see.”
25 Then He said to them, “O foolish ones, and slow of heart to believe in all that the prophets have spoken! 26 (Y)Ought not the Christ to have suffered these things and to enter into His (Z)glory?” 27 And beginning at (AA)Moses and (AB)all the Prophets, He [g]expounded to them in all the Scriptures the things concerning Himself.
The Disciples’ Eyes Opened
28 Then they drew near to the village where they were going, and (AC)He [h]indicated that He would have gone farther. 29 But (AD)they constrained Him, saying, (AE)“Abide with us, for it is toward evening, and the day is far spent.” And He went in to stay with them.
30 Now it came to pass, as (AF)He sat at the table with them, that He took bread, blessed and broke it, and gave it to them. 31 Then their eyes were opened and they knew Him; and He vanished from their sight.
32 And they said to one another, “Did not our heart burn within us while He talked with us on the road, and while He opened the Scriptures to us?” 33 So they rose up that very hour and returned to Jerusalem, and found the eleven and those who were with them gathered together, 34 saying, “The Lord is risen indeed, and (AG)has appeared to Simon!” 35 And they told about the things that had happened on the road, and how He was [i]known to them in the breaking of bread.
Jesus Appears to His Disciples(AH)
36 (AI)Now as they said these things, Jesus Himself stood in the midst of them, and said to them, “Peace to you.” 37 But they were terrified and frightened, and supposed they had seen (AJ)a spirit. 38 And He said to them, “Why are you troubled? And why do doubts arise in your hearts? 39 Behold My hands and My feet, that it is I Myself. (AK)Handle Me and see, for a (AL)spirit does not have flesh and bones as you see I have.”
40 [j]When He had said this, He showed them His hands and His feet. 41 But while they still did not believe (AM)for joy, and marveled, He said to them, (AN)“Have you any food here?” 42 So they gave Him a piece of a broiled fish [k]and some honeycomb. 43 (AO)And He took it and ate in their presence.
The Scriptures Opened
44 Then He said to them, (AP)“These are the words which I spoke to you while I was still with you, that all things must be fulfilled which were written in the Law of Moses and the Prophets and the Psalms concerning Me.” 45 And (AQ)He opened their understanding, that they might comprehend the Scriptures.
46 Then He said to them, (AR)“Thus it is written, [l]and thus it was necessary for the Christ to suffer and to rise from the dead the third day, 47 and that repentance and (AS)remission of sins should be preached in His name (AT)to all nations, beginning at Jerusalem. 48 And (AU)you are witnesses of these things. 49 (AV)Behold, I send the Promise of My Father upon you; but tarry in the city [m]of Jerusalem until you are endued with power from on high.”
The Ascension(AW)
50 And He led them out (AX)as far as Bethany, and He lifted up His hands and blessed them. 51 (AY)Now it came to pass, while He blessed them, that He was parted from them and carried up into heaven. 52 (AZ)And they worshiped Him, and returned to Jerusalem with great joy, 53 and were continually (BA)in the temple [n]praising and blessing God. [o]Amen.
Footnotes
- Luke 24:1 NU omits and certain other women with them
- Luke 24:4 NU omits greatly
- Luke 24:11 nonsense
- Luke 24:12 NU omits lying
- Luke 24:13 Lit. 60 stadia
- Luke 24:17 NU walk? And they stood still, looking sad.
- Luke 24:27 explained
- Luke 24:28 acted as if
- Luke 24:35 recognized
- Luke 24:40 Some printed New Testaments omit v. 40. It is found in nearly all Gr. mss.
- Luke 24:42 NU omits and some honeycomb
- Luke 24:46 NU that the Christ should suffer and rise
- Luke 24:49 NU omits of Jerusalem
- Luke 24:53 NU omits praising and
- Luke 24:53 NU omits Amen.
© 2017 Bible League International
Holy Bible, New International Version®, NIV® Copyright ©1973, 1978, 1984, 2011 by Biblica, Inc.® Used by permission. All rights reserved worldwide.
NIV Reverse Interlinear Bible: English to Hebrew and English to Greek. Copyright © 2019 by Zondervan.
Scripture taken from the New King James Version®. Copyright © 1982 by Thomas Nelson. Used by permission. All rights reserved.

