Malaika akapaza sauti akasema: “Ameteketezwa! Mji mkuu Babeli umeteketezwa! Umekuwa nyumba ya mapepo. Mji ule umekuwa najisi. Mji uliojaa kila aina ya ndege najisi. Ni mahali ambapo kila mnyama najisi na anayechukiwa anaishi.
Naye akasema kwa sauti kuu, “Ameanguka, Babiloni mkuu, ameanguka! Amekuwa maskani ya mashetani, makazi ya kila roho mchafu, kiota cha kila ndege mchafu na wa kuchukiza.