Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni, ikasema, “Liandike hili: Kuanzia sasa heri wale wanaokufa wakiwa wa Bwana.” Roho Mtakatifu anasema, “Ndiyo, hilo ni kweli. Watapumzika kutokana na kazi yao ngumu. Yale waliyotenda yatakaa pamoja nao.”
Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika haya: Wamebarikiwa watu ambao tangu sasa wanakufa wakiwa ndani ya Bwana.” “Naam,” asema Roho, “watapumzika baada ya taabu zao, kwa kuwa matendo yao yatawafuata.”