Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Revised Common Lectionary (Semicontinuous)

Daily Bible readings that follow the church liturgical year, with sequential stories told across multiple weeks.
Duration: 1245 days
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Version
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Prov for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Warumi 3:9-20

Je, sisi Wayahudi ni bora kuliko wengine? Hapana, nimekwishaonyesha kuwa watu wote, wawe Wayahudi au wasio Wayahudi, wako chini ya nguvu ya dhambi.

Watu Wote Wana Hatia

10 Kama Maandiko yanavyosema,

“Hakuna atendaye haki,
    hakuna hata mmoja.
11 Hakuna hata mmoja anayeelewa,
    hakuna anayetaka kumfuata Mungu.
12 Wote wamegeuka na kumwacha,
    na hawana manufaa kwa yeyote.
Hakuna atendaye mema,
    hakuna hata mmoja.”(A)
13 “Maneno yao ni ya hatari kama kaburi lililo wazi.
    Wanatumia ndimi zao kwa kusema uongo.”(B)
“Maneno yao ni kama sumu ya nyoka.”(C)
14     “Midomo yao imejaa maneno ya laana na hasira.”(D)
15 “Nyakati zote wako tayari kuua mtu.
16     Kila wanakokwenda wanasababisha matatizo na uharibifu.
17 Hawajui jinsi ya kuishi kwa amani.”(E)
18     “Hawamheshimu wala kumcha Mungu.”(F)

19 Tunajua ya kwamba, kile ambacho sheria inasema ni kwa ajili ya wale waliopewa sheria. Hii inamaanisha kuwa watu wote, Wayahudi na wasio Wayahudi, hawana udhuru kwa matendo yao. Hivyo ulimwengu wote unasimama mbele za Mungu na lazima ujibu kwake. 20 Kwa sababu kufuata sheria hakumfanyi mtu akahesabiwa haki mbele za Mungu.[a] Sheria inatuonyesha dhambi zetu tu.

Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)

© 2017 Bible League International