Revised Common Lectionary (Semicontinuous)
Yesu Achagua Wanafunzi Wake Kumi na Wawili
(Mt 10:1-4; Mk 3:13-19)
12 Siku chache baadaye, Yesu alikwenda mlimani kuomba. Alikaa huko usiku kucha akimwomba Mungu. 13 Asubuhi iliyofuata aliwaita wafuasi wake, akachagua kumi na wawili miongoni mwao na kuwaita Mitume. Nao ni:
14 Simoni (ambaye Yesu alimwita Petro),
Andrea aliyekuwa kaka yake Petro,
Yakobo,
Yohana,
Filipo,
Bartholomayo,
15 Mathayo na
Tomaso,
Yakobo mwana wa Alfayo,
Simoni aliyeitwa Mzelote,
16 Yuda mwana wa Yakobo,
na Yuda Iskariote (yule ambaye baadaye alimsaliti Yesu).
Yesu Afundisha na Kuponya Watu
(Mt 4:23-25; 5:1-12)
17 Yesu na mitume wakatelemka kutoka mlimani. Yesu akasimama mahali tambarare. Kundi kubwa la wafuasi wake lilikuwa pale. Walikuwepo pia watu wengi waliotoka sehemu zote za Uyahudi, Yerusalemu, na maeneo ya pwani karibu na Tiro na Sidoni. 18 Wote walikuja kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao. Aliwaponya watu waliokuwa wanasumbuliwa na mapepo. 19 Kila mtu alijaribu kumgusa, kwa sababu uweza ulikuwa unamtoka. Yesu aliwaponya wote.
© 2017 Bible League International