Revised Common Lectionary (Semicontinuous)
Sisi ni Hekalu la Mungu
14 Ninyi hamko sawa na wale wasioamini. Hivyo msifungwe nira pamoja nao. Wema na ubaya havikai pamoja. Nuru na giza haviwezi kukaa pamoja katika chumba kimoja. 15 Itawezekanaje kuwe na mapatano kati ya Kristo na beliali?[a] Je, mwamini anashirika gani na asiye amini? 16 Hekalu la Mungu halina mapatano yoyote na sanamu, na sisi tu hekalu la Mungu aliye hai. Kama Mungu anavyosema,
“Nitakaa kati yao
na kutembea nao;
Nitakuwa Mungu wao,
na watakuwa watu wangu.”(A)
17 “Hivyo tokeni nje kati yao
na jitengeni nao, asema Bwana.
Msishike chochote kilicho kichafu,
nami nitawakaribisha.”(B)
18 “Nitakuwa baba yenu,
nanyi mtakuwa wana wangu na binti zangu,
asema Bwana Mwenyezi.”(C)
7 Rafiki wapendwa, tuna ahadi hizi toka kwa Mungu. Hivyo tujitakase maisha yetu na kuwa huru kutoka kwa kila kinachofanya miili yetu ama roho zetu kuwa najisi. Heshima yetu kwa Mungu itufanye tujaribu kuwa watakatifu kabisa kwa namna tunavyoishi.
© 2017 Bible League International