Font Size
Warumi 8:34-36
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Warumi 8:34-36
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
34 Ni nani anaweza kuwahukumu watu wa Mungu kuwa wana hatia? Hayupo! Kristo Yesu alikufa kwa ajili yetu na alifufuliwa kutoka kwa wafu. Na sasa ameketi upande wa kulia wa Mungu na anazungumza na Mungu kwa ajili yetu. 35 Je, kuna kitu chochote kinachoweza kututenga na upendo wa Kristo? Je, ni matatizo au shida au mateso? Ikiwa hatuna chakula au mavazi au tunakabiliwa na hatari au kifo, je mambo hayo yatatutenga sisi kutoka katika upendo wake? 36 Kama Maandiko yanavyosema,
“Kwa ajili yako, tunakabiliana na kifo wakati wote.
Watu wanadhani hatuna thamani kama kondoo wanaowachinja.”(A)
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International