Malaika Mwenye Hati Ndogo

10 Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa amevaa wingu, na upinde wa mvua kich wani. Uso wake uling’aa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto. Mkononi mwake alikuwa ameshika hati ndogo iliyokuwa imefunguliwa. Mguu wake wa kulia aliuweka juu ya bahari na mguu wake wa kushoto aliuweka juu ya nchi kavu. Naye akaita kwa sauti kuu kama simba anayenguruma. Alipopaza sauti, ngurumo saba ziliitikia kwa kishindo. Na zile ngurumo saba zilipokwisha kuitikia, nilitaka kuanza kuandika, lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Funga hayo yaliyosemwa na ngurumo hizo saba, ni siri; usiyaandike.”

Kisha yule malaika aliyekuwa amesimama juu ya bahari na nchi kavu akainua mkono wake wa kulia juu mbinguni, akaapa kwa jina la Mungu aishiye milele na milele, aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote vilivyomo, na bahari na vyote vilivy omo, akasema, “Wakati wa kungoja umekwisha. Lakini katika siku ambazo yule malaika wa saba atakaribia kupiga tarumbeta yake, siri ya Mungu itatimizwa kama alivyowatangazia watumishi wake manabii.”

Ndipo ile sauti niliyokuwa nimeisikia pale mwanzoni ikasema nami tena, “Nenda, kachukue ile hati iliyoko mkononi mwa yule malaika aliyesimama juu ya bahari na nchi kavu.”

Basi nikaenda, nikamwomba yule malaika anipe ile hati ndogo. Akaniambia, “Ichukue uile. Itakuwa chungu tumboni mwako, lakini mdomoni mwako itakuwa tamu kama asali.” 10 Basi nikaichukua ile hati ndogo kutoka mkononi mwa yule malaika nikaila. Ilikuwa tamu kama asali mdomoni mwangu lakini nili poimeza, ikawa chungu tumboni mwangu. 11 Kisha nikaambiwa, “Inakubidi kutoa unabii tena kuhusu watu wengi, na mataifa, lugha na wafalme.”

The Angel and the Little Scroll

10 Then I saw another mighty angel(A) coming down from heaven.(B) He was robed in a cloud, with a rainbow(C) above his head; his face was like the sun,(D) and his legs were like fiery pillars.(E) He was holding a little scroll,(F) which lay open in his hand. He planted his right foot on the sea and his left foot on the land,(G) and he gave a loud shout like the roar of a lion.(H) When he shouted, the voices of the seven thunders(I) spoke. And when the seven thunders spoke, I was about to write;(J) but I heard a voice from heaven(K) say, “Seal up what the seven thunders have said and do not write it down.”(L)

Then the angel I had seen standing on the sea and on the land(M) raised his right hand to heaven.(N) And he swore(O) by him who lives for ever and ever,(P) who created the heavens and all that is in them, the earth and all that is in it, and the sea and all that is in it,(Q) and said, “There will be no more delay!(R) But in the days when the seventh angel is about to sound his trumpet,(S) the mystery(T) of God will be accomplished, just as he announced to his servants the prophets.”(U)

Then the voice that I had heard from heaven(V) spoke to me once more: “Go, take the scroll(W) that lies open in the hand of the angel who is standing on the sea and on the land.”

So I went to the angel and asked him to give me the little scroll. He said to me, “Take it and eat it. It will turn your stomach sour, but ‘in your mouth it will be as sweet as honey.’[a](X) 10 I took the little scroll from the angel’s hand and ate it. It tasted as sweet as honey in my mouth,(Y) but when I had eaten it, my stomach turned sour. 11 Then I was told, “You must prophesy(Z) again about many peoples, nations, languages and kings.”(AA)

Notas al pie

  1. Revelation 10:9 Ezek. 3:3